[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji7]Tafasiri Unavyoweza: Nje Sawa, Ndani ya Box Unapajua?
Kama kumetokea msemo unaosikika sana katika miaka ya hivi karibuni ni huu unaosema fikiria nje ya box (Thinking outside the box). Huu ni msemo ambao ni maarufu sana katika nyanja za ujasiriamali. Ukihudhuria mafunzo ya wajasiriamli utausikia sana huu msemo. Ni msemo unaovutia kusikiliza na utashangaa unaambiwa kufikiria nje ya box wakati hakuna anayekuuliza ndani ya box ulilomo kuna nini. Tafasiri unavyoweza.
Labda nipunguze kuandika mengi, kufikiria nje ya box ni hali ya kuwa mbunifu, kutambua nguvu ulizonazo na madhaifu yako katika kutekeleza jambo mahsusi. Maana yake hapa ni kuwa huwezi kufikiri nje ya box kama hauko ndani ya box na kujua kilichomo ndani ya box ni kitu gani na ufanye nini kutatua changamoto za ndani ya box.
Ukishajua kilichomo ndani ya box, na si lazima mtu mwingine akwambie nini kilichomo ndani ya box unalilomo, unayajua yaliyomo yamo ndani ya box, ni jukumu lako kuyajua haya na si mtu mwingine ajitokeze na kukwambia ufikirie nje ya box. Ukishajua kilichomo ndani ya box sasa una haki ya kfikiri nje ya box na unawezaje kufikiri nje ya box, hili ndo suala sasa.
Unaweza kufanya mambo kadhaa ya msingi kama unataka kufikiri nje ya box, mfano, siku zote unanyoa toka juu kwenda chini, haya ni mazoea, hebu leo badili unaponyoa anzia chini kwenda juu, huku ndo kufikiria nje ya box. Tafuta maarifa na taarifa sahihi, fanya uthubutu na usidharau, tafuta ushauri kwa mtoto mdogo, wanajua ya kujua na anaweza kukwambia kitu ambacho hukutegemea. Jipe nafasi ya kuwa msafi, oga na vaa vizuri kila wakati.
Hivi unajua kuota ni moja ya njia nzuri ya kupanga mpango timamu! (Dreaming is a form of planning!!). Tafasiri unavyoweza.
[emoji106] [emoji106] [emoji106]Marhabaa
[emoji120] [emoji120] [emoji120] hatujambo binamu hbr ya Ntwara[/QUOT
Ntwara kuchele, asante kwa kuuliza.
kweli huu Uzi NI wa makapuku ..maaana sio kwa idadi ya hizo comment aiseeee
...salamu yako nimeipokea kwamoyo mkunjufu.
Hujambo wewe na wote walio karibu yako?
kweli huu Uzi NI wa makapuku ..maaana sio kwa idadi ya hizo comment aiseeee
Asante kamanda Obe.Muziki: Jumatano
Kwaresma inaendelea na kuna mahala inafika unatamani kula ambacho umeamua kufunga. Ninakusalimia kapuku na kukutakia usiku mwema
Asante kamanda Obe.
Binamuuuuu nakusalimiaa katika jina la fatuma cheupeeeMjomba Lyon Lee nakusalimia sana ndugu yangu wa hasara chache na faida nyingi.
Umemskia anko kawagombeza tra, inaweza kuwa na afadhari kwenye ile ishu?
Ahsante sana mtaasisi kwa kibao cha Loi toka kwa mkali wa zamani OlomideMuziki: Ukikunja Ngumi Hufikiri Sawasawa
...kufikiri ni mchakato/ process na si jambo linalohitaji nguvu ya mwili zaidi (physique-tamka fiz-eek) bali utambuzi, nguvu ya kuchambua mambo na zaidi nguvu ya akili timamu. Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukwambia tu it is almost Furahiday.
Siku nyingi sijaandika mengi hapa, naweka muziki tu na kuacha muziki uongee, si unamkumbuka Hamza Kalala na kile kibwagizo chake cha eee mamama tunakula miziki' ndo nilikuwa nafanya. Na huu ulikuwa ni ushauri wa anko wangu Lyon Lee ambaye kwa kweli amekuwa kwenye wakati mgumu sana kipindi hiki maana ukiacha safari zake za kanda ya kaskazini bado hata huku JF alikuwa akipambana na waandamanaji waliojipanga kimkakati kukaa wanamsifia aunt yangu.
Muziki, niseme tu Makapuku forum ni sehemu nzuri kuwepo na ukisoma kipenegele hiki utajijua wewe ni mtu muhimu namna gani humu Jukwaani.