Makapuku Forum

Asante mdau kwa kutupia kumbukumbu hii humu.

Hongera kwa wanawake wote wa Makapuku Forum, nyie ni mashujaa (sheroes) na mnalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo
[emoji122]
 
Ahsante sana mtaasisi
 
Hii inaitwa bampa tu bampa
Ahsante mtaasisi kwa good music dedication to our mother's, sister's, nieces, aunt's and all women's in the world.



Leo kwenye weekend music tupigie kibao cha Peter and Andre kiitwacho Mystery girl maalumu kwa makapuku wote.
 
Tafasiri Unavyoweza: Hasira Itusaidie, Isiumize

....nilikuwa nikishangazwa sana na namna kamanda mmoja mstaafu wa jeshi la polisi ambaye kila akiongea alikuwa akionesha hasira hata kama taarifa anayotoa ilikuwa ni ya kuelezea jambo la kawaida sana kwenye nchi za kidemokrasia, maandamano. Hasira ni tabia ambayo kila binadamu anayo, wala usijisikie vibaya kuwa nayo, ila ujisikie vibaya pale hasira uliyonayo inakuwa na lengo la kuumiza, kuua na uharibifu kwa mwingine au vitu (hostile aggression). Hii ni hasira mbaya, haikusaidii wewe wala huyo/hicho unachonuia kukionesha upungufu wako. Tafasiri Unavyoweza

Hasira inaweza kukusaidia, ndiyo pale unapoifanya na kuitumia kufikia lengo jema kabisa kama kutia bidii darasani (instrumental aggresion). Hasira ya kufanya kazi kwa bidii, hasira ya kutimiza ahadi ulizoahidi na hasira ya kuwa mwananchi anayewajibika kwa jamii yake. Muangalie mwanajeshi kwa mfano akiwa vitani kwa lengo la kulinda mipaka ya nchi yake, hii ndo hasira unayopaswa kuwa nayo, mwangalie mwalimu anayeadhibu kwa kufundisha uelewe, jiangalie nawe unapojitahidi kufanya kazi kwa bidii kujipatia maisha yenye furaha.

Usiitumie hasira katili/ovu (hostile) popote pale iwe ni moja kwa moja au kificho (indirect aggression- ambapo unakaa kusambaza uongo na fitna kwa lengo la kuumiza au kuharibu taswira ya mtu au kitu). haikusaidii na wala haikufanyi ukaonekana una ujasiri au wewe ni wa kipekee zaidi inaonesha kuwa wewe ni mtu asiyekamilika, una mapungufu na si afya kwako na kwa wanaokuzunguka. Onesha tabia ya hasira inayojenga, na wala si kuwa chanzo cha kuleta utengano, onesha hasira yenye kuleta utangamano kwenye jamii. Tafasiri Unavyoweza

Uwe na weekend njema. Tukutane wakati mwingine tena. Nakupenda Kapuku
 


Usikonde mtaasisi mwenzangu, nitakirusha muda si mrefu
 
Muziki: Wikend Njema

Ninakusalimia na kukutakia weekend njema kapuku mheshimika. Pole kwa uchovu wa wiki nzima na leo ni furahiday. Jipe raha na nafasi ya kupumzika, usisahau kuwa na wakati angalau wa kunyoosha viungo vya mwili.

Muziki sasa, kwa niaba ya mtaasisi mwenzangu Nyagei tafadhari burudika na kibao hiki na tukutane Jumatatu tena

 
Binamu popote ulipo nakufataa huwezi kunikimbia kizembe ...@obe binamu kiroho swaaafiii puliiiiz puliiiiz letiii mii noooou weyaaaa yuaaa
 
Binamu shikamoo
Halaf kuna siku niliingia humu nikaomba nyimbo hivi hujaona post yangu au vipiii niliomba nyimbo ya tilda ya sweet mother

marhaba aunt yangu
....nadhani ilikuwa ni weekend, kama sikosei jumamosi au jumapili. Weekend napumzika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…