Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Kunuka Sio Kuoza

Unakumbuka mambo ya kuchanganua sentensi kwa njia ya matawi na njia nyingine, muda umepita sana lakini kujikumbusha ya zamani si mbaya na hasa kama yanakuongezea maarifa. Unaweza kulichambua neno/kitenzi kunuka utakavyo na ndiyo maana hiki kipengele kipo hapa, unatafasiri unavyoweza, na si lazima wote tuwe na tafasiri moja juu ya jambo au kitu fulani. Wengine tafasiri hutegemeana na mazingira, tafasiri ya juzi si ya jana na haiwezi kuwa na ulazima kuwa hivyo hivyo kesho na kesho kutwa, tafasiri unavyoweza.

Wengi wetu ni watumiaji wa bidhaa tunazonunua madukani au magengeni, baadhi ya bidhaa hizi huwa zimeandikwa muda wa matumizi ambao kwetu tumeupa umaarufu wa expire date. Leo nitakufanya utafasiri tofauti kidogo na hata ukibaki na tafasiri yako sio mbaya maana ndiyo lengo la makala haya. Hivi unajua kuna tofauti ya sell-by, use-by, best-by na expire date? Yes, nimeandika haya maneno kwa kiinglish maana ndiyo huwa tunaona kwenye bidhaa nyingi tunazonunua.

Tumekuwa na kawaida ya kutupa bidhaa tulizonunua baada ya kuona tarehe kwenye bidhaa husika ikionesha muda wake umepita. Hii inaweza kuwa ni sawa na au isiwe sawa, nitafafanunua;
Tumia kabla ya- hii ni ilani inayoonesha mnunuzi anaweza kuupata ubora wa bidhaa aliyonunua kwa kiwango kizuri kabisa (freshness) na tarahe ikipita haimaanishi kuwa bidhaa hiyo imeharibika. Uza kabla ya- hapa mlengwa ni muuzaji, auze bidhaa hii na muda ukiisha aitoe kwenye makabati na wauzaji wengine hu-markdown- kuuza kwa punguzo bidhaa husika, bidhaa kama mayai, maziwa, maua, ni maarufu kwa hili. Ubora kabla ya- hapa bidhaa unayonunua inatajwa kuwa ni bora kwa kipindi kilichooneswhwa kwenye karatasi.

Usitupe tu bidhaa kisa umeona maneno hayo hapo juu, ila ukiona imeandikwa expire date- basi hiyo tupa. Harufu ya nguru haimaanishi kuoza bali ndo ubora wake. tafasiri Unavyoweza
Shukrani binamu ...Thanks alout
 
Hahaha
Aki uko na kumbukumbu mob Sana!! Kama hukuvunjika ile siku hutokaa uvunjike tena love!!!
Hahahaa...

Unajua sijasahau kipindi kile uko kwa bibi yako huko kaskazini...

Kule hakuna netwek bhana, ila mtoto ukawa unapiga mguu na kilometre 12 kuja kutafuta netwek mjini ili uwasiliane na T..

Aki Mungu aendelee kukuweka tuu.
 
Muziki: Wiki Njema

Nikushukuru sana mjomba wangu Lyon Lee kwa kuongoza kipengele hiki Ijumaa, Asante sana na jukwaa hili ni zuri kwa sababu wewe upo, pamoja na kunisingizia mambo kweli lakini nitafanya nini sasa wakati wewe ndo anko wangu. Nikusalimie Kapuku mwenzangu na nikutakie wiki Njema , leo ni jtatu FYI.

Wikend kwangu ilikuwa poa sana, niliangalia movie mpya Black Panther , nikaipenda. Usidhani nilienda jumba la senema, la, mambo ya kudownload tu. Si unajua anko wangu kwake ana Wi-Fi so nikatake advantage wikend wakati alipoenda kusuluhisha mgogoro wake na mchepuko wake mpya.

Muziki sasa, nisikuchoshe ila itoshe tu kusema wewe kuwepo hapa pamoja na tofauti zetu, unalifanya MF kuwa sehemu Bora kabisa kuwepo


 

Similar Discussions

Back
Top Bottom