Katika dondoo za bbc. ..
[emoji117] Mgogoro wa ardhi wilayani Loliondo, Kaskazini mwa Tanzania umeendelea kukua baada ya mamlaka za uhifadhi wilayani humo kuendelea kuchoma nyumba za watu wa jamii ya Kimaasai.
[emoji117] Rais Donald Trump anatembelea Texas, wakati ambapo jimbo hilo likihangaika kukabiliana na madhara yaliyosababishwa na mvua nyingi.
[emoji117] Bunge jipya la Katiba nchini Venezuela limepiga kura kwa kauli moja kuunga mkono viongozi wa upinzani kushtakiwa kwa makosa ya uhaini
[emoji117] Wakati Kenya ikianza kutekeleza marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki,nchi ya Rwanda ilianza marufuku hiyo miaka 9 iliyopita na inajivunia kufanikiwa kutekeleza marufuku hiyo
[emoji117] Mkuu wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa-FAO-Jose Graziano da Silva ameanza ziara rasmi ya siku tatu nchini Uganda
[emoji117] Je waufahamu muziki wa mwambao?ni maarufu katika Pwani ya Afrika mashariki,kutokana na vionjo vyake ambavyo huleta Ladha na nakshi ya aina yake katika muziki huo