Makapuku Forum

5/Jeff Healey
Alizaliwa mwaka 1966 na kufariki dunia mwaka 2008 akiwa na umri wa miaka 41
Huyu alikuwa ni raia wa Canada mwenye vipaji kibao licha ya ulemavu wake wa mcho
Alikuwa ni Mwimbaji,mpiga gitaa na mcheza filamu mahiri huko Canada na Marekani Huyu alipambana na hali yake licha ya kubezwa hadi kufanikiwa kuwa mtu mashuhuri kwenye filamu na muziki kiasi cha kupiga pesa ya maana kwa kuutumia ulemavu wake bila kupiga watu assist kama za bwana yule wa Jf na akafanikiwa kumiliki bendi kibao cha Angel Eyes, ndio kilichotamba zaidi kiasi cha kukamata # 5 Billboard Hot 100 na kuuteka ulimwengu
Kaimba pia :
I Think I Love You Too Much
Stop Breaking Down
Hoochie Coochie Man
Like A Hurricane
......

 
4/Casey Harris Alizaliwa Januari 1987
Huyu naye alipambana na hali kuanzia utotoni hadi ujanani na kufanikiwa kutimiza ndoto zake za kimaisha
Ni memba wa kundi la X--Ambassadors Hawa wanatamba sana na nyimbo zao kibao tu
....
 
3/Ray Charles
Alizaliwa mwaka 1930 na kufariki dunia mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 73
Huyu alikuwa ni mwanamuziki mahiri wa nyimbo za injili,Jazz na Pop alikuwa pia na uwezo mkubwa wa kuandika nyimbo
Jamaa licha ya kuwa kipofu ila alikuwa ni bishoo wa kutupwa ujanani kuanzia nywele ,mapigo ya pamba hadi miwani nyeusi alichagua tu za kibishoo
Kaimba nyimbo kibao kama vile
Seven Spanish Angels
Georgia On My Mind
I Can't Stop Loving You
Hit The Road ,Jack
Seven Spanish Angels
.....
 
2/Andrea Bocelli
Alizaliwa Septemba 22 mwaka 1958
Huyu ni mwanamuziki mashuhuri wa Kitaluano
Sio tu mashuhuri jamaa ni mjanjamjanja anacheza hadi filamu licha ya kwamba haoni kawahi kutajwa kwenye orodha ya 50 Most Beautiful People na jarida moja mashuhuri duniani
Muziki wake pia ameimba na mastaa kibao akiwemo Celine Dion Pia kaimba
A Mio Padre
Because We Believe
.....
 
1/Stevie Wonder
Alizaliwa Mei 13 1950
Huyu wala sihitaji maneno mengi kumwelezea maana bado yupo masikioni na machoni kwa watu na muziki wake unajulikana vilivyo
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Shukrani kwa mliosapori mada
Niwatakie Usiku Mwema
Tukutane Jumatatu
Mwisho
............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…