Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Arfi) atupa kadi kikaoni, atishia kujiondoa chamani!

Viongozi wasiom na msimamo watemwe Chadema, mbona viongozi wengine wengi wameshatuhumiwa je nao walitupa kadi zao, viongozi uchwara wasitafute kisingizio waondoke tu wasitubabaishe sisi wenye nia dhabiti ya ukombozi wa nchi yetu.
 
Hawa vijana maslahi walioikuta CHADEMA imekuwa na inaheshimika wanatumika kama toilet paper kwa kuwadharau waasisi na waliojitolea kuijenga, huyu ni arfi kishafikia hapa kutaka kurudisha kadi, huyu ni mzee mwenye busara na hekima , lakini vijana masalahi wanamtukana na kumdhalilisha, hawa ndio wanashinda humu JF kuizika CHADEMA wakijidai wajuaji , ZZK anasakamwa kule na hutu tuvijana twa ovyo ovyo , wachumia tumbo huu mgogoro hautawaacha salama hata hao kina saaa nane na wenzao, pesa za kuwalipa zimetokana na kura za ubunge za akina arfi , ZZK na wabunge wote CHADEMA, watanzania wakishachoka, mtapata wabunge wawili na katu pesa ya kuwalipa hamtaiona tena.
Umesema ukweli,sisi yetu macho
 
pole sana makamu ,nimeanza kusikia unahujumiwa mda mrefu,nina ushahidi wakutosha kuwa kuna dada mmoja ambaye kajiunga chama mwezi wa tatu mwaka huu ndiye katumwa na kiongozi mtendaji wa juu wa chama kuja kukuhujumu uonekane haufai ili huyo dada ndiyo agombee ubunge mpanda 2015
wanasahau kwamba wewe ndio umekijenga chama mpanda mpaka kimefika hapo.
Makamu sikushauri ususie chama,wewe ni kiongozi na mbunge unapaswa kupambana mpaka mwisho kuhakikisha dhuluma na uonevu wowote kwenye chama unafika kikomo.
Askari bora ni yule asiyekimbia vita.
Okota silaha yako,mapambano yanaendelea.jipe moyo mkuu,yana mwisho.

Duh hujuma juu ya hujuma. Huyu anamhuju huyu na yule anamhujumu huyu, wanachama wanahujumiana, viongozi wanahujumiana. HUJUMA HUJUMA HUJUMA JUU YA HUJUMA.
 
Yakitokea CCM chama kina mpasuko...lakini kwa CHADEMA eti changamoto za kisiasa..!!!faraja za fedhehaaaa
 
Kama kuna mtu anamdharau Said Arfi huyo ni mshenzi. Hakuna asiyejua mchango wa huyu mzee katika kukijenga chama na hasa maeneno ya Rukwa. Tunahitaji kusimama imara wana-CHADEMA, kuna wahuni wanatafuta namna ya kupambana na CHADEMA.
 
...............Hakyanani naona watu wanafanya mchezo na kuimarisha upinzani nchini.... aidha baadhi ya watu wanajidanganya na wanajiona tayari upinzani uko katika kiwango cha juu Tanzania... huko ni kujidanganya.....wanasahau ni gharama gani imetumika kukifikisha chama hapo kilipo.....kama kawaida kutumia mabilioni kwa muda mfupi sio kazi kazi ni kuyatafuta hayo mabilioni........ popote penye neema hapakosi machafuko..... hata Yesu na wanafunzi wake ... wote hawakuwa makini... kuna waliomsaliti na wengine walichukua rushwa ili kumuua.....sasa mambo haya yanapotokea katika chama kinachojiita makini.... pasipo kufanyiwa kazi... watu watacha kuimarisha chama na kujiingiza katika migogoro ya kila kukicha..... Kumbukeni sana NCCR - Mageuzi na Mrema....watuwalikimbizana............. kiko wapi leo.......Bundi ni Bundi tu... akilia mjini watu lazima wajiulize kulikoni... ikumbukwe kuwa bila upinzania makini Nchini.......hata chama kilichopo madarakani kinakuwa hakina nguvu... kinadumaa na kujisahau
 
huyu mzee arfi naye nanatakiwa kujua siasa za sasa si za wananchi kuendelea kuwafuata watu maarufu tu imefika sehemu sasa inatakiwa watu tuwe wafuasi wa watu wenye dhamira zaidi sio watu maarufu hata huyu mzee arfi kwa kweli lengo lake katika mapambano mii silielewi bara bara
 
Sioni shida, chadema kina wanachama wasio na kadi wengi kuliko wenye kadi. Anayetishia kuhama chadema anajisumbua mwenyewe maana kwanza ndo kinazidi kupendwa! Naamini hakuna mtu mwenye akili anaweza kuhama chadema akaenda ccm!
 
Kumbe tatizo ni Uislam wao funguka kamanda....

Nifunguke nini hujaelewa tena mzee wa kulaza ubongo.Una fikra za kitumwa, upo standby kusikia tusi kw ausilam hadi unajikuta unatangaulia jiwekea mambo kabla hujasoma wala kusikia kitu.

NImekuwa wanaweka ambo fulani ktk line sana.Yaani kutoperform vyme kunapunguza idada ya watu wa matabaka walivyoweza pata viongozi wa mfano.Hii inawafanya hata watoto wadhani kuwa hawana vichwa kwa kwa business fulani,kwa vile ahata watu waliowika bado niw a hovyo tuu.

Ni kama hakuna watu wanaopoteza sana muda na taifa stars wakati kuna mechi za nje.Kwa viel hakuna role modal.
 
hii ndiyo sababu ccm imehakikisha watanzania tunabaki maskini ilhali wateule wao wananeemeka!! na kwamba wakiona mtu anachonga wanadondosha chenji kisha maskini wanaanza kudunguana mapanga wakizigombea!! hebu angalia huyo maskini wa BAVICHA ilivyojidhalilisha kisa Nape Jr. karusha chenji!!
 
Good bado Zitto & Co




Chanzo: Gazeti la Mwananchi

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezidi kuandamwa na migogoro baada ya jana kuibuka mwingine mkubwa katika kikao chake cha ndani mkoani Katavi kiasi cha kumfanya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Said Arfi, kutupa kadi yake ya uanachama.

Huu ni mgogoro wa pili mkubwa kuripotiwa katika kipindi cha juma moja lililopita baada ya ule wa wilayani Karatu ambako pamoja na mambo mengine uliishia kwa Kamati Kuu kuusimamisha uongozi wote wa chama hicho wilaya.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa Arfi ambaye ni Mbunge wa Mpanda Mjini, alitishia kujitoa Chadema jana, katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya chama hicho Mikoa ya Katavi na Rukwa kilichoketi Namanyere, Nkasi na kufikia uamuzi wa kumsimamisha Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Mkoa wa Rukwa, Laurent Mangweshi.

Katika kikao hicho, Arfi anadaiwa kuichukua kadi yake ya Chadema na kumtupia Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Rukwa, John Mallack akitangaza kuachia nyadhifa zote alizonazo, kisha kuondoka ukumbini, kabla ya kufuatwa na wazee wa chama hicho na kumsihi aichukue kadi yake hiyo.

Alifikia hatua hiyo baada ya kutokea sintofahamu kati ya wajumbe wa kikao hicho katika uamuzi huo uliofikiwa kwa kupiga kura za ndiyo na hapana.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vilifafanua kuwa Arfi alikerwa na kauli iliyotolewa na Mangweshi kuwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita, alipokea rushwa kutoka kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Vyanzo hivyo vya habari vimeeleza kuwa kutokana na hali hiyo, Arfi alipandwa na hasira na kuamua kumrushia kadi Mallack kisha kutoka nje ya ukumbi.

"Hatua hiyo ilifanya wajumbe wa kikao hicho nao kutoka nje ya ukumbi na kuanza kumbembeleza ili asichukue uamuzi huo na kisha wakamwekea kadi yake ya uanachama katika mfuko wake wa shati," alisema mmoja wa makada hao.

Arfi mwenyewe hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo baada ya simu ya mkononi kuita muda wote bila kupokewa na hata alipotumiwa ujumbe, hakujibu.

Mallack akizungumza na gazeti hili kwa simu alikiri Arfi kurusha kadi mezani kisha kutoka nje ya ukumbi, lakini akasema suala hilo lilishughulikiwa na wazee na kumalizwa.

"Ni kweli unajua huyu ni Makamu Mwenyekiti wetu wa Taifa, sasa inapotokea vijana wadogo wakamtuhumu kwa tuhuma za uongo na ambazo hazipo inatia hasira, ndiyo maana huyo kijana tumemvua uongozi," alisema Mallack.

Tuhuma za Mangweshi
Mangweshi alisimamishwa uongozi baada ya kutuhumiwa kwa mambo mbalimbali ya kiutendaji ndani ya chama hicho ikiwamo kumkashifu Arfi.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mallack alisema kuwa Magweshi amevuliwa uongozi baada ya chama hicho kujiridhisha kuwa alitenda makosa hayo.

Alisema kamati ya ushauri ilimwita ili kujibu tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikimkabili ikiwamo kutoa taarifa zisizo rasmi bila kufuata taratibu za chama.

"Pia amepatikana na hatia ya kuandika barua za kashfa na kuzipeleka makao makuu ya chama kumkashifu Arfi pamoja na viongozi wengine wa chama akiwamo Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa.

Katibu Mwenezi wa Chadema Mikoa ya Rukwa na Katavi, John Matongo alisema kabla ya kupewa adhabu ya kusimamishwa, amewahi kuonywa mara kadhaa lakini ameshindwa kujirekebisha.
 
Oh poor Tanzanians, what was expected to bring hope is now dying slowly and slowly. what shall they do this tough time tomorrow????????????????????.
 
Tatizo vijana wengi mnaoingiaa kwenye siasa mnataka kuruka hatua muhimu.Yaani mtoto hawezi tembea kabla ya kutambaa.
ONYO:Kuwa mpigania haki za watanzania inahitaji uvumilivu mkubwa sana.CHADEMA mbele daima.
 
pole sana makamu ,nimeanza kusikia unahujumiwa mda mrefu,nina ushahidi wakutosha kuwa kuna dada mmoja ambaye kajiunga chama mwezi wa tatu mwaka huu ndiye katumwa na kiongozi mtendaji wa juu wa chama kuja kukuhujumu uonekane haufai ili huyo dada ndiyo agombee ubunge mpanda 2015
wanasahau kwamba wewe ndio umekijenga chama mpanda mpaka kimefika hapo.
Makamu sikushauri ususie chama,wewe ni kiongozi na mbunge unapaswa kupambana mpaka mwisho kuhakikisha dhuluma na uonevu wowote kwenye chama unafika kikomo.
Askari bora ni yule asiyekimbia vita.
Okota silaha yako,mapambano yanaendelea.jipe moyo mkuu,yana mwisho.

Mh! Hawa lao ni moja na mikakati yao ni ya muda mrefu
 
Kama kuna mtu anamdharau Said Arfi huyo ni mshenzi. Hakuna asiyejua mchango wa huyu mzee katika kukijenga chama na hasa maeneno ya Rukwa. Tunahitaji kusimama imara wana-CHADEMA, kuna wahuni wanatafuta namna ya kupambana na CHADEMA.

Mkuu jaribu kufuatilia mambo yanavyoenda utajua tu, pro- CHADEMA wengi wanapenda watu na siyo chama. Kila siku humu humu viongozi awo wakidhalilishwa wanakuja juu. Leo Arfi analalamika kudhalilishwa hao hao watetezi wa chama wa siku nyingi wanamrushia makombora mengine.
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezidi kuandamwa na migogoro baada ya jana kuibuka mwingine mkubwa katika kikao chake cha ndani mkoani Katavi kiasi cha kumfanya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Said Arfi, kutupa kadi yake ya uanachama.


Huu ni mgogoro wa pili mkubwa kuripotiwa katika kipindi cha juma moja lililopita baada ya ule wa wilayani Karatu ambako pamoja na mambo mengine uliishia kwa Kamati Kuu kuusimamisha uongozi wote wa chama hicho wilaya.


Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa Arfi ambaye ni Mbunge wa Mpanda Mjini, alitishia kujitoa Chadema jana, katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya chama hicho Mikoa ya Katavi na Rukwa kilichoketi Namanyere, Nkasi na kufikia uamuzi wa kumsimamisha Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Mkoa wa Rukwa, Laurent Mangweshi.


Katika kikao hicho, Arfi anadaiwa kuichukua kadi yake ya Chadema na kumtupia Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Rukwa, John Mallack akitangaza kuachia nyadhifa zote alizonazo, kisha kuondoka ukumbini, kabla ya kufuatwa na wazee wa chama hicho na kumsihi aichukue kadi yake hiyo.


Alifikia hatua hiyo baada ya kutokea sintofahamu kati ya wajumbe wa kikao hicho katika uamuzi huo uliofikiwa kwa kupiga kura za ndiyo na hapana.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vilifafanua kuwa Arfi alikerwa na kauli iliyotolewa na Mangweshi kuwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita, alipokea rushwa kutoka kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


Vyanzo hivyo vya habari vimeeleza kuwa kutokana na hali hiyo, Arfi alipandwa na hasira na kuamua kumrushia kadi Mallack kisha kutoka nje ya ukumbi.


“Hatua hiyo ilifanya wajumbe wa kikao hicho nao kutoka nje ya ukumbi na kuanza kumbembeleza ili asichukue uamuzi huo na kisha wakamwekea kadi yake ya uanachama katika mfuko wake wa shati,” alisema mmoja wa makada hao.


Arfi mwenyewe hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo baada ya simu ya mkononi kuita muda wote bila kupokewa na hata alipotumiwa ujumbe, hakujibu.


Mallack akizungumza na gazeti hili kwa simu alikiri Arfi kurusha kadi mezani kisha kutoka nje ya ukumbi, lakini akasema suala hilo lilishughulikiwa na wazee na kumalizwa.
“Ni kweli unajua huyu ni Makamu Mwenyekiti wetu wa Taifa, sasa inapotokea vijana wadogo wakamtuhumu kwa tuhuma za uongo na ambazo hazipo inatia hasira, ndiyo maana huyo kijana tumemvua uongozi,” alisema Mallack.

Tuhuma za Mangweshi
Mangweshi alisimamishwa uongozi baada ya kutuhumiwa kwa mambo mbalimbali ya kiutendaji ndani ya chama hicho ikiwamo kumkashifu Arfi.


Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mallack alisema kuwa Magweshi amevuliwa uongozi baada ya chama hicho kujiridhisha kuwa alitenda makosa hayo.
Alisema kamati ya ushauri ilimwita ili kujibu tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikimkabili ikiwamo kutoa taarifa zisizo rasmi bila kufuata taratibu za chama.


“Pia amepatikana na hatia ya kuandika barua za kashfa na kuzipeleka makao makuu ya chama kumkashifu Arfi pamoja na viongozi wengine wa chama akiwamo Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa.


Katibu Mwenezi wa Chadema Mikoa ya Rukwa na Katavi, John Matongo alisema kabla ya kupewa adhabu ya kusimamishwa, amewahi kuonywa mara kadhaa lakini ameshindwa kujirekebisha

SOURCE: MWANANCHI
 
Back
Top Bottom