Makampuni ya Madini wanatulipa, hii pesa inaenda wapi?

Makampuni ya Madini wanatulipa, hii pesa inaenda wapi?

Sawa, lkn usinihusishe mimi na huo uchangiaji wako, sina haja ya kujua/kusikia mambo mengine zaidi ya haya niliyoyauliza!!
Utakoma leo kudadeki ! Nyie si mmeambiwa msifie tu bila hivyo hamtalipwa , sasa kiherehere cha kuhoji leo umekitoa wapi ?
 
makampuni ya madini yaonyehse mahesabu yao ijulikane hela sahihi inayopaswa kulipwa,,,wanalipwa hela kidogo sana
Utawasingizia Burr wale jamaa.Wale ni wafanyabiashara na ukipata fursa ya kufanya kazi mgodini utajua ile nayo so biashara rahisi tu,jamaa wanalazimika kununua his a kwenye makampuni yanayotengeza mitambo mikubwa ili wakinunua huko nao wamapata gawio.Vikitokea vifo mgodini kwa ajili ya uchimbaji,dhahabu yao inashuka being maana matajiri wazungu wanaiita dhahabu ya damu,ndiyo maana eanasisitiza sana usalama kazini.Pesa wanachangia nyingi ila tu kama hizi za Kahama zilikuwa zinaliwa na wahasibu wajanja
 
Kibaya ni kwamba kila aliepo madarakani anawaza akitoka ataonekanaje na atakuwa na nini ndo mana pesa aziwezi onekana ebu tujiulize duniani Tanzania ndo inaongoza kwa kutoa madini ya tanzanite lkn Kenya ndo inaitangaza Africa mashariki South Afrika ikiongoza Afrika mzima je c tupo wapi na faida yake nini?
 
Sawa natambua kwamba ni siyo nyingi lkn ni lazima ionekane mahali, yaani ni lazima itumike na ndicho ninachopenda kufahamu, hizo fedha zinatumikaje?
....
.....Mkuu huwamnajipritendi Vipofu eehh
 
Siyo kahama tu , umewahi kujiuliza serikali hii inalipwa bei gani kutokana na madini yake ? Na je hao waliolipa tsh 700 mil wao walipata bei gani ?

Wewe ni kati ya vi...ru..ka njia wa ccm hapa jf nadhani sasa umeanza kupata akili .
Kuwa chama fulani kunahusiana vipi na duku duku la mtu ama mnataka kuwazuia watu wasihoji na kuuliza kisa yeye ni Fulani? Hii nchi ni yetu sote na sote tuna mawazo huru juu ya hatima ya nchi yetu. Usifikiri ni watu walio upande wako tu ndo wana haki juu ya hatma ya Tz, Tz ipo kwa ajiri ya watanzania wote, kwa unaowapenda na hata wale unaowahanya ...jifunze na uelimike
 
Nimesoma kwenye blogu ya Michuzi kwamba mgodi wa Buzwagi umeilipa Halmashauri ya Wilaya ya Kahama shilingi Milioni 700, binafsi siyo mwenyeji wa Kahama na wala sipafamu lkn natambua kwamba hii siyo fedha ndogo, sasa swali ni Je kwa wakazi au watu wanaoifahamu Kahama, kuna mahali hii fedha inaonekana? Kwa maana siyo mara ya kwanza wao kulipwa fedha na mgodi wa Buzwagi, kuna chochote ambacho unaweza kusema ukifika Kahama utaona kwamba hii ni Halmashauri inayopokea Milioni 700 ktk kwa muwekezaji? Ninachomaanisha wanaiwekeza wapi? Ni kwenye Elimu, Miundo mbinu, Maji au hata ustawi wa jamii wa wananchi wa Wilaya ya Kahama?

1.png
Mkuu unajadiriwa wewe sana kuliko hata ulichokileta, na hawa ndo wanadai demokrasia na haki sawa za mawazo katika ubinadamu wetu
 
Siyo kahama tu , umewahi kujiuliza serikali hii inalipwa bei gani kutokana na madini yake ? Na je hao waliolipa tsh 700 mil wao walipata bei gani ?

Wewe ni kati ya vi...ru..ka njia wa ccm hapa jf nadhani sasa umeanza kupata akili .
Unapatia mtu ng'ombe wako anamkamua anapata lita 20 za maziwa, anaenda kuyauza yote anakuletea hela ya mauzo ya lita 2 unachekelea na kushangilia kama zuzu!
 
Mkuu unajadiriwa wewe sana kuliko hata ulichokileta, na hawa ndo wanadai demokrasia na haki sawa za mawazo katika ubinadamu wetu


Kazi ipo, watu wananishambulia badala ya kujadili nilichokiweka, uko sawa kabisa nchi yetu sisi safari bado ndefu sana!
 
Barbarosa asante kwa thread ya jana na hii ya leo kwa ujumla, nimefurahi kwamba umeanza kuuona ukweli kwa baadhi ya mambo, hongera kwa kutokufungwa na fikra potofu, umewapoteza na kuwaumiza wengi ila tutayasahau na kuendelea mbele na wewe kama ndugu yetu assadsyria3 na wengineo. Hii nchi haijengwi kwa matamko ya vitisho, ni nchi yetu sote, tusipokemea tutapotea wote. Hakika hongera sana japo umetuumiza kwa mambo ya uongo. I wish Team Lumumba wangekua wanaleta mojadala ya namna hii kila siku mngepata watu wa maana zaidi. Once again, hongera kwa kusema ukweli. Hayo ndio Upinzani wanayoyapigia makelele kwa nguvu zao zote.
.....
.....salute Mkuu
 
Kahama ni miongoni mwa wilaya chafu, bora wangewekeza kwenye kuboresha miundombinu ya mji mitaro na dustbins.
Ukiacha hiyo service levy wanapokea nyingine nyingi kutoka kwa mgodi wa kakola na migodini mingine midogo.
Niliwahi kufika korogwe tanga na kushangaa kwa nini kule pamepangika na rami hadi mitaani na hakuna chochote ila kahama ilikuwa choka mbaya. Ingekuwa Uwezo wangu migodi ingepewa Uwezo wa kusimamia miradi ya hizo pesa maana hao jamaa wa almashauri sioni kama wanaaminika. Migodi ilipowajengea kahama rami Klm tano hapo mjini kazi ilionekana na kwa wakati.
Iwekwe system ya kufuatilia hizi pesa huwa zinaenda wapi. Uko sahihi kada Barbarosa
Yaani hizo halmashauri ziliopo kwenye maeneo yenye migodi ni hatari sana kuna project ya maji ilifadhiliwa na GGM pale geita aisee ni aibu tupu,ku
 
Hilo swali nin gumu kuliko jiwe...
Lilipaswa kuulizwa na wana Kahama...lakini ukute hawajui hili wala lile...

Kuna almashauri fulani wao walijengea ela yote ukuta wa almashauri....ha ha ha..we acha tu wakati jengo la almashauri lilijengwa wakati wa mjerumani...limechoooka...ukuta wa bei mbaya...

Hahahahaha
Geita hiyo
 
Umeanza kukisaliti chama sio, hivi ni kweli hujui ccm ni wapiga dili??
 
Unashangaa Pesa Zinaenda Wapi Wakati Wewe Mwenyewe Upo Kwenye System Hacha Kutuzingua.
 
Sawa natambua kwamba ni siyo nyingi lkn ni lazima ionekane mahali, yaani ni lazima itumike na ndicho ninachopenda kufahamu, hizo fedha zinatumikaje?
Siyo hiyo shilingi milioni 700 tu wanayoipata Kahama. Mgodi wa Buzwagi pia umejenga barabara za lami za mjini Kahama. Watanzania ni watu wa kulalamika tu hata pale hawajui undani wa wanachokilalamikia. Ukweli ni kuwa hakuna mgodi wowote usiolipa kodi mbalimbali, tena ukilinganisha na baadhi ya nchi nyingine, sisi tunatoza zaidi.

Bahati mbaya sana Watanzania wengi wanaamini uchimbaji wa madini ni sawa na kuchimba mchanga bila kufahamu kuwa kuna gharama kubwa sana zinazitumika katika uchimbaji madini. Kampuni inaweza kuchimba dhahabu ya dola milioni 100 lakini gharama za uchimbaji zikafikia dola milioni 70. Serikali ikipata corporate tax ya dola milioni 9, Watanzania wataishia kusema kuwa tumeibiwa. Tumelipwa kodi ya milioni 9 na mwekezaji amechukua dola milioni 91, kama vile hayo madini kutoka huko chini yanaletwa na upepo. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba hayo yanasemwa na hata wale unaofikiria wameelimika.
 
Back
Top Bottom