Barbarosa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2015
- 22,584
- 27,838
- Thread starter
- #21
Hizo hela hazilingani hata kidogo na hela alizokwapuwa yule "Nyoka mwenye Makengeza" Kama bakshishi ya udalali wa ununuzi wa Rada. Zaidi ya bilioni mia tatu watu waligawana kama njugu na hakuna walichofanywa. Kivuko cha Dar es salaam ni mfano mwingine kuhusu ufujaji wa fedha zetu, lakini mko kimya.
Kuna watu wanakuona Barbarosa kama vile akili imekurudia lakini ukweli wa mambo ni kwamba huwa mnawatoa kafara watu wasio na madhara kwenu kuhalalisha "Uzalendo" wenu kwa Tanzania. Hizo hela za Kahama unazilinganishe na zile zinazotumika kule chato kufanya uwekezaji ambao hauna tija kwa taifa kwa mwaka huu wala kwa miaka kumi ijayo?
Sijaleta hii Mada kutafuta mchawi, kumshutumu yoyote kwa lolote wala kulinganisha nani kafanya nini na wapi bali nimeleta ili kutataka kufahamu jinsi Wilaya ya Kahama inavyotumia hizo fedha kama kuna mwenye uelewa, ni hivyo tu!