Makame Mbarawa aiwakia ATCL

Makame Mbarawa aiwakia ATCL

False start at ATCL; Ni bora hizo nyingine zilizoagizwa wangesubiri kidogo ili ATCL ijipange vizuri zaidi kiutendaji kwani ATCL ilishakufa zamani sana kwa hiyo hata watendaji wake wengi ni Obsolete kabisa, hawajui kinachoendelea kwenye Airline industry; wameshaota kutu wanasubiri kukatika kama chuma chakavu!
Well said
 
Kwa hiyo mkuu unamaanisha body mpya ila chasis na engine ni zile zile mbovu[emoji3] [emoji3] [emoji3]


Haswaaa, wafanyakazi (Chasis) wote ni chuma chakavu; Ndege na bodi ya wakurugenzi ni mpya (Bodi); kweli unategemea ufanisi gani hapo?! Si chasis itavunjikilia mabali na kuiacha Bodi inagalagala porini?!
 
Haswaaa, wafanyakazi (Chasis) wote ni chuma chakavu; Ndege na bodi ya wakurugenzi ni mpya (Bodi); kweli unategemea ufanisi gani hapo?! Si chasis itavunjikilia mabali na kuiacha Bodi inagalagala porini?!
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Mmmh... Conspiracy?


Ile kampuni ya Kirombo (PW) ndio ililihujumu ATC ya awali, sasa si lazima wamejipanga kusurvive ushindani mpya wa shirika la umma kwa mbinu zilezile walizotumia kuimaliza ATC wakati huo!
 
Ile kampuni ya Kirombo (PW) ndio ililihujumu ATC ya awali, sasa si lazima wamejipanga kusurvive ushindani mpya wa shirika la umma kwa mbinu zilezile walizotumia kuimaliza ATC wakati huo!
Hii conspiracy theory yako bado cjaielewa
 
False start at ATCL; Ni bora hizo nyingine zilizoagizwa wangesubiri kidogo ili ATCL ijipange vizuri zaidi kiutendaji kwani ATCL ilishakufa zamani sana kwa hiyo hata watendaji wake wengi ni Obsolete kabisa, hawajui kinachoendelea kwenye Airline industry; wameshaota kutu wanasubiri kukatika kama chuma chakavu!
Ni bora ungeporomoa matusi ya zamani kuliko haya mapya.
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Leo ameiwakia, kesho ataizimikia hamna chochote kitakachobadilika kama wasipofanya mabadiliko kwenye mfumo mzima wa utendaji kazi, ni bora waziri akae na wakurugenzi kuunda mfumo utakaodhibiti upigaji hela kuliko kutoa tu tamko la kuwaasa waache kupiga hela au kubadilisha safu.

Hii ni karne ya 21 unaweza kufanya automation ya full business process ya industry yoyote na kuwa na full transparency ya transaction zinazofanywa na kuweza kumfanya mtu kuwa accountable kwa jambo lolote atakalofanya wakati huo huo (realtime).

Angalia kampuni kubwa za nje wanavyofanya management zao si rahisi kupiga hela ukapona hivi hivi lazima utajulikana lazima utashughulikiwa ipasavyo.
 
Solution hapo ni kuvuruga vuruga wote...wahamishwe hamishwe waje wapya..hao wanafanya kazi kwa mazoea..
 
Kwa wenye kampuni za utalii huwezi kupanga ratiba za wageni kwa kuitegemea atl maana hakuna siku utakuwa na uhakika wa safari. Kila dakika kuahirisha safari. Wageni wanakosa flight za kurudi kwao. Inakuwa hasara ya kampuni yenye wageni.
 
Tatizo la ATCL ni kubwa sana kuliko vile watu wanavyodhania.
Ni shirika lililoanzishwa kisiasa, Linafanya kazi kisiasa, Lilikufa kisiasa na sasa linafufuliwa kisiasa. Siasa na Biashara ni kama Maji na Mafuta, huwa haviendani kabisa.

Yaani, Waziri Mzima anasema, uwekwe utaratibu ili wafanyakazi wa serikali wanaposafiri kwa Ndege basi Walazimishwe kupanda ndege za ATCL pekee!!
Sijui kama waziri anajua athari za kauli yake kwa makampuni mengine ya ndege, Ubora wa Huduma za ATCL, Wajibu wa mfanyakazi wa serikali nk.

Sijawahi kuona siasa ikifanikisha biashara.
Ni suala la muda tu, ATCL itakufa tena, na tutaendelea kumsaka mchawi milele.

Anayeiloga ATCL ni serikali yenyewe.
 
Wambadilishe yule twiga wa canada waweke wa ki-tanzania
 
Ndio maana waziri amewaka Kweli Leo.. Nadhani ujumbe umefika

Mimi nafikiri Waziri kama kiongozi wa kisiasa ametimiza wajibu wake japo sifikiri kuwaambia wasio weza kasi wakae pembeni....kwani tunazikimbiza hizo ndege kwa miguu ili ziruke??

Hivi mtu hapo anajiwekaje pembeni??

Waambie waje na mikakati watafanya nini pamoja na targets zake na kwa muda gani wakutathmini mafanikio.

Wakishindwa kufikia targets hizo taratibu za ajira ziko wazi kwamba wanastahili kupata nini...kisha weka wengine tunasonga mbele kiroho safi bila makelele wala lawama zisizokua na masikio.

Vinginevyo tutaendelea kupigishana makelele na kutiana joto bila sababu za msingi wakati wahusika hawajui muelekeo ni upi watakao pimwa nao.

Tukiendelea hivi Yesu atarudi na jehanam itawadia na kuzikuta ndege zetu ziko hapohapo eapoti zinasubiri matamko.
 
Mbowe alikua wa kwanza kukimbilia kupanda na akawahi siti ya dirishani,Leo tanapa mnakandia ndege zetu?
 
Kuna mtu alileta uzi alisema hatapanda tena hizo ndege, Akisema waliambiwa ndege haiwez kutua arusha so wajigharamie gharama zao kwenda KIA alaf kufika kia wakawekwa 3hours kusibir crappy board members...
Kifupi hizi ndege hazina mwisho mzuri.....
Kuna jamaa yangu aliipanda from Mwanza to Dar.
Mpaka sasa (Almost two weeks elapsed) Masikio yake hayako sawa kwa Kelele za DearBomba angani
 
Back
Top Bottom