Majukumu ya familia yamekuwa makubwa kuliko kipato chake, mpe ushauri

Huyu jamaa yangu amejikuta kwenye dimbwi zito la Mawazo anaomba ushauri

Ana miaka 37 ameoa ana mke na watoto watatu ,ana watoto wa mdogo wake wa kike watatu

Mdogo wake wa kike alizalia nyumbani na alikimbia nyumbani na kuwaacha watoto wake ,ili kupunguza shida kwa wazazi akaamua kuwachukua

Anamlaumu baba yake kwa maisha wanayoishi kwa sababu zifuatazo

Aliajiriwa kama dreva kwenye makampuni ya usafirishaji,lakini hakuwekeza sehemu yoyote ,hakununua ardhi yoyote,hakujenga nyumba yake ya kudumu,hakuwekeza hata kwenye biashara ,alichoambulia ni pombe na wanawake akaambulia ugonjwa wa kisasa

Mama yake yeye ndiye alkuwa anajitahidi kuwahudumia wakati baba yao akishindia baa

Familia sasa ni maskini kweli kweli,kwa juhudi za mama huyo jamaa yangu akajitahidi akasoma akapata kazi serikali za mitaa ingawa mshahara ni mdogo ila anajitahidi kuwahudumia wazazi wote .

Sasa hivi amejikuta katika msongo wa mawazo mazito ambayo yanahitaji tiba haraka sana

Anasema ndo ameanza kujenga pamoja na mshahara huo mdogo maana familia inakua lakini anajikuta anazidiwa ..Pamoja na kuanza kujenga nyumba yake wazazi wanapinga kujenga kwa sababu wazazi wanadai awajengee kwanza kabla hajaanza kujenga nyumba yake

Anasema kila mwezi alkuwa anawanunulia wazazi wake mahitaji na familia yake,alipoanza kujenga kuna vitu vimepungua hasa kwa wazazi wake (huduma)

Mbaya zaidi mama yake anaumwa ugonjwa wa kuvimba viungo vya mwili,ikabidi akope amtibu mama yake

Hata mwezi haujaisha baba naye anaumwa hali yake imedhoofika kwa sababu ana ugonjwa mwingine wa kisasa,na mbaya zaidi baba yake ameenda kukaa kwake akimwambia huyo kijana wake ampeleke hospital anajiskia vibaya mnooo

Na wakati huo huo zimebaki wiki chache mke wake ajifungue

Mpe jamaa ushauri ,afanyeje na hela hana ...ana familia ya watu watu 7 ina maana watoto watatu na mke wake,watoto wa dada yake wapo watatu na wazazi hao wanamtegemea asilimia mia na wanaumwa tena magonjwa makubwa anafanyaje?
Mwambie akimbie mji aende kuishi peke yake huko na tembo.

Nawatahadhalisha vijana mnaokwenda kuoa sasa hivi, mjihadhari na kupata watoto...utakuwa na shida hadi kaburini..
Ingekuwa kuna switch ya kuzima via vya uzazi ningevizima ili nisiweze kupata watoto, nyege ndo adui yetu mtamu!!!
 
Huyo rafiki yako kazaliwa yeye na dada yake pekee kwa hao wazazi.? Au kuna ndugu zao wengine pia wa tumbo moja.?
 
Alipotoka ni mbali aendako ni mbali hakuna kukata tamaa maisha ni mapambano mpaka kifo
Hili ndilo la msingi zaidi never give up hata kama giving up is the only solution.... Mungu hakupi mtihani ili ushindwe there is always a way.. mjamaa asikate tamaa aendelee kupambana to the last drop of his blood..
 
Mwambie akimbie mji aende kuishi peke yake huko na tembo.

Nawatahadhalisha vijana mnaokwenda kuoa sasa hivi, mjihadhari na kupata watoto...utakuwa na shida hadi kaburini..
Ingekuwa kuna switch ya kuzima via vya uzazi ningevizima ili nisiweze kupata watoto, nyege ndo adui yetu mtamu!!!
Nyege zinakutengenezea uadui wa nini.?
 
Mwambie aache upumbavu,kuna watu Wana shida mara ya hizo na still wapo happy.Kuzaliwa masikini hamkufanyi mtu kuwa masikini.
 
Kuna vitu hujavieleza sawasawa,ni kusema hana ndugu alizaliwa peke yake ktk uzao wao?

Then kama wapo awashirikishe,na sometimes vijana tujiongeze kujifunza kitu...kumlaumu mzazi kwamba hakujenga nyumba ili uje kuwa mrithi siyo solution (wakati mwengine kujenga ni bahati ya mtu au ni kipaji Mungu anatoa kwa watu) so mzee wako hakuwa na hiko kipaji solution ni wewe mwenye uzao wako kupambana ili nao wasije wakaishi kama wewe,atulize akili hii ya wazazi kulalamika awatulize awaambie wamuache kwanza ajenge nyumba yake kwa ajili ya familia yake ila hatawaacha akihamia atawachukua kuishi nao huku akijenga kule kwenye kitovu cha familia.

Kujiua hakujawahi kuwa suluhisho la matatizo.
 
Aombe Mungu akumbuke zaburi ya 51, kisa za Zakayo, Kisa cha Paulo na Silla, na Kisa Meshack, Abedinego na etc. Walafme wa 2 /Kitabu cha Daniel amwambia Mungu shida zake chozi likimtoka ndani ya wiki Mungu atatenda. Abarikiwe Mungu yupo si utani.
 
Na wakati huo huo zimebaki wiki chache mke wake ajifungue
Sasa huyu rafikiyo inaonekana aidha ni hamnazo kabisa ndio maana hata anawaza kujiua, au ni shida zimezaa shida kwenye akili!

Yaani kwa shida zote hizo bado anapachika mimba...kweli!?
Na huyo mke wake naye ana tatizo, maana kwa mazingira hayo ana wajibu wa kuzuia mimba ili kumpunguzia mzigo waubani wake.

Mwambie asijiue, apambane na hali yake.
Sio amjazie binti wa watu mimba halafu akimbie...no way!
 
Mkuu watoto hao wa mdogo wake ndo wa kwanza yupo darasa la pili,na wengine chekechea,hivyo hawawezi kufanya chochote,pia ujue nao wanatakiwa wasome,wale,wavae na watibiwe,si kutoka kwa mtu mwingine wanamungalia uncle yao
Aajiri MTU.
 
Yeye ndo amekuja na wazo hilo kwamba Mr cosovo kama hali ndo hii kwa nini asijinyonge,?
Kuwaz kujiua tayar tatizo lingine nje ya maisha! Hiyo Ni emotional case... Ni ishar pia ya matatizo ya sonona mkuu vipi unahisi Kuna kit lingine anacho kwa sasa awali hakuwa nacho!? Mfano( kuwa smart au kusosholaiz n wat Kama zamani kumepungua)
 
Mwambie afungue biashara ndogo ndogo kama vile kuuza vitumbua maandazi Na Chai Na chakula itasaidia kupata Hela ndogo ndogo Kwa ajili ya kupunguza ukali WA gharama ZA maisha... Biashara HII isimamiwe Na Hao watoto wa kike anao walea hapo kwake
Conglomerate income source!!!!!
 
ubinafsi unamsumbua anajiangalia yeye tu,wanasema hivi wasemaji.
unazo sababu billioni za kutabasabu,kwa sababu tabasamu lako linaamsha matumaini kwa wengine,huyu jamaa hawazi siku yuko ndani ya jeneza,huo msururu utafarakana kwa style gani!!!
Kasahau Kam yeye yupo tu mambo hayaelekei akifa hawa wanaomuangalia anawaachaje
 
Kuna vitu hujavieleza sawasawa,ni kusema hana ndugu alizaliwa peke yake ktk uzao wao?

Then kama wapo awashirikishe,na sometimes vijana tujiongeze kujifunza kitu...kumlaumu mzazi kwamba hakujenga nyumba ili uje kuwa mrithi siyo solution (wakati mwengine kujenga ni bahati ya mtu au ni kipaji Mungu anatoa kwa watu) so mzee wako hakuwa na hiko kipaji solution ni wewe mwenye uzao wako kupambana ili nao wasije wakaishi kama wewe,atulize akili hii ya wazazi kulalamika awatulize awaambie wamuache kwanza ajenge nyumba yake kwa ajili ya familia yake ila hatawaacha akihamia atawachukua kuishi nao huku akijenga kule kwenye kitovu cha familia.

Kujiua hakujawahi kuwa suluhisho la matatizo.
Ana ndugu wawili wa kiume na mmoja wa kike ,hawa wakiume wamezamia mjini na hawajulikani walipo

Anacholaumu ni kwa nini wazazi hawakujenga nyumba yao bora na wakati baba alkuwa anafanya kazi nzuri,yeye kuanza kujenga wazazi wacomplain?
 
Mkuu ni hali halisi huyu jamaa anayokumbana nayo,kama hapa anawaza baba yake ni kweli ni mgonjwa na hana hela na mbaya Mzee kaja kukaa kwake akimshinikiza ampeleke hospital, ungekuwa wew unafanyaje kwa mfano na huku ukumbuke siku si nyingi ametoka kumuuguza mama yake na mama yake bado hajapona kuna madawa inapaswa awe ananunuliwa dah!!!

kama mzee ni mgonjwa, la msingi la kwanza ni uzima, aanze kumtibu mzee aka baba yake....na kama ni muathirika amuanzishie dozi fasta fasta.

Mzee akishaanza dozi na kurecover akae naye chini kiume wakiwa mtu mbili amsisitizie umuhimu wa matumizi ya dawa ili kumuepusha na shida za hapa na pale ambazo zinacost na kuzidisha umasikini...
Ampe somo mzee namna anavyouchukia umasikini na kupambana kujinasua nao na kuokoa kizazi chao..kulingana na hali ajaribu kumueleza mzee uelekeo ni upi ikiwa ni pamoja ya yeye mzee na mama kuishi kwa budget maana mzigo unakwenda kwake huku kipato chake ni kidogo...

Mwisho, ukizaliwa kwenye hizi familia za kimasikini na wewe ukauchukia umasikini basi huna budi kupambana kuokoa jahazi hasa kwa wale wadogo the upcoming ili wasije nao wakawa wazembe na kuendeleza wimbi labda iwe ni mipango tu ya Mungu...
 
Yeye ndo amekuja na wazo hilo kwamba Mr cosovo kama hali ndo hii kwa nini asijinyonge,?
Sasa akijinyonga serikali ina ajiri mtu mwingine
Halafu Wazazi wake wataishi vp pia atakuwa ameongeza tena tatizo jingine watoto wake wataenda wapi familia yote itajikuta ipo kwenye shimo lile lile la umasikini wa kutupwa bora hata yeye anapokea kitu kidogo kutoka kwenye ajira yake.!
 
Kwenye maisha kila mtu anamipango yako kulingana na nyakati zake..

Mzee wako au Mama yako ana nafasi ya kutoa ushauri lakini sio lazima ukafuata ushauri wake maana hata wewe sasa umeshakua na ni nafasi yako ya kufikiri namna sahihi ya wewe kwenda mbele..
 
Huyu jamaa yangu amejikuta kwenye dimbwi zito la Mawazo anaomba ushauri.

Ana miaka 37 ameoa ana mke na watoto watatu ,ana watoto wa mdogo wake wa kike watatu.

Mdogo wake wa kike alizalia nyumbani na alikimbia nyumbani na kuwaacha watoto wake ,ili kupunguza shida kwa wazazi akaamua kuwachukua.

Anamlaumu baba yake kwa maisha wanayoishi kwa sababu zifuatazo.

Aliajiriwa kama dreva kwenye makampuni ya usafirishaji,lakini hakuwekeza sehemu yoyote ,hakununua ardhi yoyote,hakujenga nyumba yake ya kudumu,hakuwekeza hata kwenye biashara ,alichoambulia ni pombe na wanawake akaambulia ugonjwa wa kisasa.

Mama yake yeye ndiye alkuwa anajitahidi kuwahudumia wakati baba yao akishindia baa.

Familia sasa ni maskini kweli kweli,kwa juhudi za mama huyo jamaa yangu akajitahidi akasoma akapata kazi serikali za mitaa ingawa mshahara ni mdogo ila anajitahidi kuwahudumia wazazi wote.

Sasa hivi amejikuta katika msongo wa mawazo mazito ambayo yanahitaji tiba haraka sana.

Anasema ndo ameanza kujenga pamoja na mshahara huo mdogo maana familia inakua lakini anajikuta anazidiwa. Pamoja na kuanza kujenga nyumba yake wazazi wanapinga kujenga kwa sababu wazazi wanadai awajengee kwanza kabla hajaanza kujenga nyumba yake.

Anasema kila mwezi alkuwa anawanunulia wazazi wake mahitaji na familia yake,alipoanza kujenga kuna vitu vimepungua hasa kwa wazazi wake (huduma).

Mbaya zaidi mama yake anaumwa ugonjwa wa kuvimba viungo vya mwili,ikabidi akope amtibu mama yake.

Hata mwezi haujaisha baba naye anaumwa hali yake imedhoofika kwa sababu ana ugonjwa mwingine wa kisasa,na mbaya zaidi baba yake ameenda kukaa kwake akimwambia huyo kijana wake ampeleke hospital anajiskia vibaya mnooo.

Na wakati huo huo zimebaki wiki chache mke wake ajifungue.

Mpe jamaa ushauri ,afanyeje na hela hana ...ana familia ya watu watu 7 ina maana watoto watatu na mke wake,watoto wa dada yake wapo watatu na wazazi hao wanamtegemea asilimia mia na wanaumwa tena magonjwa makubwa anafanyaje?
Mkuu ni wewe
 
Back
Top Bottom