- Thread starter
- #21
SEHEMU YA TATU
Haya sasa ile siku ndio leo! Mambo vipi wanajf. Binafsi niko poa kama wasemavyo vijana wa kitanzania. Siku zinakimbia sana mwaka ndio huoo! Ni kama unainama siku zitembee. Kifo nacho chaja. Haya bwana huo ni utangulizi tu wa hadithi yetu juu ya Meja jenerali Suheil Al Hassan.
Huyu kamanda Suheil El Hassan akaanza kushangaza wengi kwa mbinu na tabia zake vitani. Tofauti na makamanda wengi wa Kisyria huyu Colonel Suheil El Hassan ( akiwa canali kipindi hicho) akaagiza maiki na speaker kitu cha ajabu vitani. Speaker ? Ya nini sasa? Hizi speaker alizoagiza zilikuwa zenye uwezo wa sauti yake kupenya umbali mrefu sana.
Basi Suheil El Hassan na kikosi chake hiki wakaanza kutembea na speaker hizi katika mission zao . Baadae wakuu wake wakagundua Kwamba speaker zilikuwa maalum kwa ajili ya kuwaimbia maadui zake mashairi ya kutisha sana. Al Hassan huwakanya kwamba wasijaribu kupigana nae kwani wataangamia vibaya.
Pia huwaomba wakumbuke watoto wao na familia zao kwa mara ya mwisho kwani muda wao wao wa kufa umefika Kama hawatasalimu amri. Hii kwa kichaga huitwa Psychological Warfare.
Yaani kuwapiga maadui kwa maneno magumu ya kupukuchua nati za mioyo yao. Na Ni kweli kwa namna hii mara kadhaa waasi walisarenda kwa hofu ya nguvu ya gharika ya mabomu ya kanali Hassan. Mfano kule Allepo na Eastern Ghouta waasi wengi walisarenda kwa wingi kuepuka hasira ya Al Hassan.
Haya sasa katika mwaka 2013 jiji karibu lote la Allepo lilishaangukia mikononi mwa waasi wa Syria. Waasi walikuwa wameteka jiji hilo na hivyo kukata mawasiliano ya barabara ya kijeshi na kiraia kati ya Allepo na eneo la ukanda wa kati wa Syria. Kutokana na jambo hili basi Colonel Suheil El Hassan akapewa jukumu la kuhakikisha kwamba supply line kutoka Allepo na central Syria inarudi mikononi mwa Serikali . Operation dhidi ya waasi hawa ikaitwa Operation Canopus Star. Hii ni moja ya operation ngumu zaidi iliyowahi kutokea katika vita ya Syria.
Waasi waliposikia hili la offensive operation dhidi yao na kamanda ajae wa operation hiyo dhidi yao hofu ikawatawala sana. Wakizungumzia jambo hili dhidi ya kanali Hassan walisema kwamba El Hassan wanamjua na kwa jina la mola hatashinda.
Ilipofika ile siku ya operation,, ndege vita vita za Kisyria zilianza kupiga maeneo yote yaliyosemekana kuwa ngome za waasi. Kwa masaa 48 angani ilikuwa ni makombora yakivurumishwa kutoka ndege Vita za kirusi su 25 frog foot, su 24 fencer . Ndege zikawaminya waasi vilivyo. Wasiopatwa na makombora wakafukiwa na majengo yaliyodondoka. Waswahili wana msemo wao vita havina macho. Ni kweli hata wasio waasi yaani wananchi wakaangamia vibaya.
Unaambiwa kwa siku mbili yalianguka mabom 3000 ndani ya jiji la Allepo. Allepo ya maghorofa ikawa ni magofu ndege zilifanya uasi , si tu dhidi ya wananchi wasio hatia na waasi bali hata kwa maghorofa. Ohh ile Syria nzuri ilikua inaangamia waso huruma walifanya kiitwacho capet bombing yaani kusafisha na kushusha kila kilichosimama.
Siku ya tatu ilikuwa siku ya kanali Hassan. Alipofika tu uwanja wa Vita akawahamasisha vijana kupigana dhidi ya vibaraka wa Ulaya na Marekani. Akaomba kipaza sauti halafu akakiinua juu na akaanza kuimba mashairi mazito akisema..
" Ile siku mbaya ya kijana mpenda mashairi imefika. Mimi ndio yule mtu hatari mwenye moyo wa chuma. Isitoshe nina fikra pana ya kuwamaliza wote msiposarenda. Lakini pia mimi ni mpole kama bahari tulivu mkinielewa. Mimi kwa jina langu huitwa colonel Suheil Al Hassan. The Tiger"
Baada ya hapo kama hakuna kusarenda Kanali Hassan huingia rasmi kama ambavyo Rambo hufanya vitani. Kushambulia bila kukoma. Kupigana kufa na kupona.
Kwa nguvu yake ya ushawishi na morali kikosi chake kikapigana kufa na kupona mjini Allepo. Wakafanya operation ya nyumba kwa nyumba kuwasaka wabishi. Baada ya wiki moja na siku tatu jeshi la Syria likashinda kwa kishindo na hivyo Alepo ikakombolewa huku operation ikiacha makovu ya raia 248 kufa vitani.
Je ilikuwaje mpaka kanal Hassan akatambulika hadharani? Moja kati ya mambo yaliyopaisha jina la kanali Hassan ilikuwa ni kuwa kamanda kiongozi bora wa kivita ya ardhini kote Syria kuanzia mwaka 2011 hivi na kuendelea. Kutambulika huku kwa El Hassan ilikuwa kwa namna ya jina lake tu na sio picha yake.
Mnamo mwaka 2014 Al Hassan aliletwa Hadharani na watu wakaanza kumjua yeye ni nani historia umri
kwa namna ya picha na video. Ni nani waliofanya hivi na kwanini? Hao walikuwa ni serikali ya Syria waliotaka kuongeza morali ya kivita kwa wapiganaji watiifu wa Assad.
Kupitia SAMA TV, Al Hassan alionekana akiwa mstari wa mbele akiwafariji, na kuongeza morali Vita kwa wapiganaji watiifu wa Assad. Video hiyo ilichukuliwa wakati El Hassan akiwa mjini Ghouta kwenye operation iliyofaulu pia dhidi ya waasi. Kupitia Hassan ardhi nyingine ya Syria ikakombolewa kwani kila kitu kinawezekana. Al Hassan ameweza wao washindwe wana Nini?
Hapo Easten Al Ghouta Al Hassan alikichafua ile mbaya chafu hivyo basi kutokana na nidhamu na ushujaa vitani Rais Dr Assad akampandisha cheo kutoka kanali na kuwa brigedia jenerali mwaka 2015. Hassan alikubali cheo lakini akaamua kupigana mstari wa mbele Kama wapiganaji wengine.
Syria bado iko mikononi mwa waasi. Hivi Bgedia Jenerali El Hassan atafanya nini juu ya Hili?
Pencil
formula2
mbogo mzee
taamu
Spartacus boy
njumu za kosovo
Mamlukii
kawombe
Mr Bundi mtu wa peponi
ITAENDELEA....
Haya sasa ile siku ndio leo! Mambo vipi wanajf. Binafsi niko poa kama wasemavyo vijana wa kitanzania. Siku zinakimbia sana mwaka ndio huoo! Ni kama unainama siku zitembee. Kifo nacho chaja. Haya bwana huo ni utangulizi tu wa hadithi yetu juu ya Meja jenerali Suheil Al Hassan.
Huyu kamanda Suheil El Hassan akaanza kushangaza wengi kwa mbinu na tabia zake vitani. Tofauti na makamanda wengi wa Kisyria huyu Colonel Suheil El Hassan ( akiwa canali kipindi hicho) akaagiza maiki na speaker kitu cha ajabu vitani. Speaker ? Ya nini sasa? Hizi speaker alizoagiza zilikuwa zenye uwezo wa sauti yake kupenya umbali mrefu sana.
Basi Suheil El Hassan na kikosi chake hiki wakaanza kutembea na speaker hizi katika mission zao . Baadae wakuu wake wakagundua Kwamba speaker zilikuwa maalum kwa ajili ya kuwaimbia maadui zake mashairi ya kutisha sana. Al Hassan huwakanya kwamba wasijaribu kupigana nae kwani wataangamia vibaya.
Pia huwaomba wakumbuke watoto wao na familia zao kwa mara ya mwisho kwani muda wao wao wa kufa umefika Kama hawatasalimu amri. Hii kwa kichaga huitwa Psychological Warfare.
Yaani kuwapiga maadui kwa maneno magumu ya kupukuchua nati za mioyo yao. Na Ni kweli kwa namna hii mara kadhaa waasi walisarenda kwa hofu ya nguvu ya gharika ya mabomu ya kanali Hassan. Mfano kule Allepo na Eastern Ghouta waasi wengi walisarenda kwa wingi kuepuka hasira ya Al Hassan.
Haya sasa katika mwaka 2013 jiji karibu lote la Allepo lilishaangukia mikononi mwa waasi wa Syria. Waasi walikuwa wameteka jiji hilo na hivyo kukata mawasiliano ya barabara ya kijeshi na kiraia kati ya Allepo na eneo la ukanda wa kati wa Syria. Kutokana na jambo hili basi Colonel Suheil El Hassan akapewa jukumu la kuhakikisha kwamba supply line kutoka Allepo na central Syria inarudi mikononi mwa Serikali . Operation dhidi ya waasi hawa ikaitwa Operation Canopus Star. Hii ni moja ya operation ngumu zaidi iliyowahi kutokea katika vita ya Syria.
Waasi waliposikia hili la offensive operation dhidi yao na kamanda ajae wa operation hiyo dhidi yao hofu ikawatawala sana. Wakizungumzia jambo hili dhidi ya kanali Hassan walisema kwamba El Hassan wanamjua na kwa jina la mola hatashinda.
Ilipofika ile siku ya operation,, ndege vita vita za Kisyria zilianza kupiga maeneo yote yaliyosemekana kuwa ngome za waasi. Kwa masaa 48 angani ilikuwa ni makombora yakivurumishwa kutoka ndege Vita za kirusi su 25 frog foot, su 24 fencer . Ndege zikawaminya waasi vilivyo. Wasiopatwa na makombora wakafukiwa na majengo yaliyodondoka. Waswahili wana msemo wao vita havina macho. Ni kweli hata wasio waasi yaani wananchi wakaangamia vibaya.
Unaambiwa kwa siku mbili yalianguka mabom 3000 ndani ya jiji la Allepo. Allepo ya maghorofa ikawa ni magofu ndege zilifanya uasi , si tu dhidi ya wananchi wasio hatia na waasi bali hata kwa maghorofa. Ohh ile Syria nzuri ilikua inaangamia waso huruma walifanya kiitwacho capet bombing yaani kusafisha na kushusha kila kilichosimama.
Siku ya tatu ilikuwa siku ya kanali Hassan. Alipofika tu uwanja wa Vita akawahamasisha vijana kupigana dhidi ya vibaraka wa Ulaya na Marekani. Akaomba kipaza sauti halafu akakiinua juu na akaanza kuimba mashairi mazito akisema..
" Ile siku mbaya ya kijana mpenda mashairi imefika. Mimi ndio yule mtu hatari mwenye moyo wa chuma. Isitoshe nina fikra pana ya kuwamaliza wote msiposarenda. Lakini pia mimi ni mpole kama bahari tulivu mkinielewa. Mimi kwa jina langu huitwa colonel Suheil Al Hassan. The Tiger"
Baada ya hapo kama hakuna kusarenda Kanali Hassan huingia rasmi kama ambavyo Rambo hufanya vitani. Kushambulia bila kukoma. Kupigana kufa na kupona.
Kwa nguvu yake ya ushawishi na morali kikosi chake kikapigana kufa na kupona mjini Allepo. Wakafanya operation ya nyumba kwa nyumba kuwasaka wabishi. Baada ya wiki moja na siku tatu jeshi la Syria likashinda kwa kishindo na hivyo Alepo ikakombolewa huku operation ikiacha makovu ya raia 248 kufa vitani.
Je ilikuwaje mpaka kanal Hassan akatambulika hadharani? Moja kati ya mambo yaliyopaisha jina la kanali Hassan ilikuwa ni kuwa kamanda kiongozi bora wa kivita ya ardhini kote Syria kuanzia mwaka 2011 hivi na kuendelea. Kutambulika huku kwa El Hassan ilikuwa kwa namna ya jina lake tu na sio picha yake.
Mnamo mwaka 2014 Al Hassan aliletwa Hadharani na watu wakaanza kumjua yeye ni nani historia umri
kwa namna ya picha na video. Ni nani waliofanya hivi na kwanini? Hao walikuwa ni serikali ya Syria waliotaka kuongeza morali ya kivita kwa wapiganaji watiifu wa Assad.
Kupitia SAMA TV, Al Hassan alionekana akiwa mstari wa mbele akiwafariji, na kuongeza morali Vita kwa wapiganaji watiifu wa Assad. Video hiyo ilichukuliwa wakati El Hassan akiwa mjini Ghouta kwenye operation iliyofaulu pia dhidi ya waasi. Kupitia Hassan ardhi nyingine ya Syria ikakombolewa kwani kila kitu kinawezekana. Al Hassan ameweza wao washindwe wana Nini?
Hapo Easten Al Ghouta Al Hassan alikichafua ile mbaya chafu hivyo basi kutokana na nidhamu na ushujaa vitani Rais Dr Assad akampandisha cheo kutoka kanali na kuwa brigedia jenerali mwaka 2015. Hassan alikubali cheo lakini akaamua kupigana mstari wa mbele Kama wapiganaji wengine.
Syria bado iko mikononi mwa waasi. Hivi Bgedia Jenerali El Hassan atafanya nini juu ya Hili?
Pencil
formula2
mbogo mzee
taamu
Spartacus boy
njumu za kosovo
Mamlukii
kawombe
Mr Bundi mtu wa peponi
ITAENDELEA....