Majina ya utani enzi za utoto!

Majina ya utani enzi za utoto!

hahahahahaha mimi na raki yangu hadi leo tukikutana tuna itana majina ya utani mimi alikuwa ana niita kibodi na yeye nilikuwa na muita kitambi na haya majina yalioshika hadi leo hii.

Kwa nini mlikuwa mnaitana hivo???
 
Habari za usiku wanaCC....

Miss u mingi wapendwa, hope mko mwake mwake babaake!!

Dah, leo nimekumbuka majina ya utani enzi za utoto, hapa nitataja baadhi ya majina ya utani ya marafiki zangu wa utotoni na langu nitalitaja humohumo ila sitaliweka wazi maana kuna watu humu wanaweza kunistukia....

Nawe pia unaweza kuongeza jina lako au la marafiki zako wa utotoni!!!!!

Kuna dogo mmoja alikuwa akiitwa Pendo, yeye tulimtungia Pendo mshua alikuwa.mshua kweli, Dogo mmoja tulikuwa tunamuita Maudaga ( mihogo iliyokaushwa kwa ajili ya kusagwa kuwa unga) yeye huyu kichwa chake kila siku kilikuwa na vidonda donda visivyopona.

Mwingine tulimuita pengo tochi, baada ya kung'ooka meno mapengo yake yalikuwa makubwa kweli. Hata baada ya meno kuota jina lake la utani likawa pengo tochi...

Mwingine tulimuita Miss Coke.. huyu alikuwa msichana mweusi ti, yaan ule weusi wa mng'ao sana!

Mwingine tulimuita Mchomoko, yaan huyu msichana alikuwa anaongea saaana, afu alikuwa hajatulia, mara yuko. hapa mara kule ya ana kiherehereeeeeee........

Hebu ongezea!!!!!

Kumbe nawe unatoka Kanda ya ziwa
 
charminglady hivi watoto wa siku
hizi na wenyewe wanajiitaga haya majina kama sie zamani

ndio, hapa mtaani kuna watoto wanaitana majina mpaka yamezoeleka na kwao yanaanza kuzoeleka. Mfano kuna mtoto anaitwa Aziza(kibuga), lukumani(bonye), halfan mpemba(kibela), khailat(kilikuu, kisa hakaoti nywele kapo kama kadoli), Chausiku(chiku midenda, yupo std 6 ila anatoa maudenda). Hao wengne cjui sababu.
 
Last edited by a moderator:
Msema kweli mpenzi wa mungu, mimi sekondari niliitwa jina la JASHO, coz ukiniitia binti natoka jasho mpaka natia huruma japo now ni jasiri na ninawatafuta kishenzi.
 
Msema kweli mpenzi wa mungu, mimi sekondari niliitwa jina la JASHO, coz ukiniitia binti natoka jasho mpaka natia huruma japo now ni jasiri na ninawatafuta kishenzi.

hahaaa...saiv hutoki jasho mkuu???
 
Back
Top Bottom