Majimbo ya kukombolewa 2020

Majimbo ya kukombolewa 2020

Malisa Godlisten hivi majuzi alikuwa anamsifia Bulaya kupeleka maji Bunda ...Je kazi ya Bulaya ni kupeleka maji jimboni?

Muwe mnawasiliana kabla ya kuja kupost
Kupeleka siyo hoja. Bottom line ni kwamba hiyo siyo responsibility ya mbunge
 
Huyu Boniphace yuko jimbo gani ambayo imeendelea kuliko East Singida?Ukisoma Katiba imeandikwa kuwa serikali ina wajibu wa kuleta maendeleo kwa wananchi wake.Kazi ya mbunge ni kutunga sheria,kukosoa serikali pale inapokosea,kuwakilisha wananchi kwa kuishauri serikali kuhusu changamoto zinazokabili wananchi wake,je kama ni kwel Singida mashariki kiuchumi iko chini kuliko majimbo mengine kwanini serikali ya ccm imetenga wananchi wa Singida mashariki au walikuwa wanawakomoa kwa sababu ya kumchagua TL?
Yupo jimbo la lumumba
 
Nilifikiri utazungumzia majimbo yote ya singida! Sera aliyotumia Lissu ya kuzuia ushuru wa kuku,debe na magunia machache,ndiyo JPM anaitumia sasa hivi. Sasa makosa yake nini. Juzi tu hapa watu walichangia kwa njia ya harambee ujenzi wa maabara,je hayo si maendeleo? Mkoa huu tangu uhuru ulitengwa na serikali lakini hivi sasa watu wamepiga hatua. Mtoa hoja tumekuwa tukihoji mgawanyo wa fedha za maendeleo ili Nchi nzima ipige hatua. Singida imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi. Tunachoimba serikali,pindi mafuta yatakapoanza kuchimbwa serikali iutendee haki huu mkoa.
 
Bujeti inapopitishwa bungeni huwa niya Tanzania nzima na pesa itaenda majimbo yote regardless la CCM au la UPINZANI
Ukitupa tofauti na Majimbo mwenza ya Singida tunaweza kukusikiliza japo kidogo.

Na kwa sasa naona mko busy kupeleka Maji na kuhudumia hospital itakuwa rahisi mno kulirudisha maana mnasolve vipaumbele vya jimbo bika kujitambua.

Na mnaweza mkajikuta mnapoteza mengine kwa maana wananchi Wa Singida watajiukiza kumbe ukichagua upinzani hopitali na Maji yanakuja bila kutumia nguvu kubwa.

Hongera sana Lissu.Kwako we we mleta mada pambana na hali yako Lissu humuwezi
 
mada zako hazna logic mpk zina boaa kuwa makini unapo andika
 
Wadau habarini,

Miongoni mwa waliofanya makosa ya Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 ni wapiga kura wa Jimbo ya Singida Mashariki.

Ukweli Jimbo hili hadi leo bado lipo chini sana Kiuchumi ukilinganisha na Majimbo mengine.

Jimbo hilo linakabiliwa na changamoto kadha zikiwemo ukosefu wa huduma muhimu za Jamii.

Changamoto hizi kiukweli zimeendelea kuwepo pamoja na ahadi nyingi walizopewa wakazi hao kwa nyakati mbalimbali.

Wakati umefika sasa kwa wakazi hao kuamka mapema kwa kujiandaa ili muda muafaka utakapofika mfanye maamuzi sahihi ya kidemokrasia na kufuta makosa mliyofanya hapo awali.

Mnaweza tu kuondokana na hali halisi mliyonayo kwa kufanya maamuzi sahihi kwa kuzingatia ubora wa chaguo lenu badala ya kuchagua kiushabiki.

Msikate tamaa ila msifanye makosa tena.

Aksanteni.
Ungeanzia Dodoma maeneo ya Bahi watu wanaishi kwa kula viwavi jeshi, jiulize kuanzia uhuru CCM ipo madarakani mpaka leo ila hata kusambaza maji ya kunywa bado ni shida.
 
kwa hiyo toka 1961 Tundu Lissu alikuwa anarudisha nyuma maendeleo ya Singida Mashariki?
 
Kuna watu wanakiwango kidogo sana cha kufikiria,, mtoa maada ni mmojawapo
 
Kwa hiyo majimbo mengine yanayoendelea yako chini ya nani?
Hivi unajua kuwa mbunge anapeleka changamoto za jimbo lake lakn fedha za maendeleo znatolewa na serikali_? Serikali ikoje kimawasiliano na vyama pinzan hadi iviunge mkono 100% majimbon mwao????
 
Uzezeta gani wakati unasema jamaa wameamua wamuue ili wachukue jimbo? Mimi nilipatwa na mfadhaiko niliposoma maandishi yako. Sasa kosa langu liko wapi?


Roho ya uuwaji itakufanya uweweseke hadi mwisho wa uhai wako,comment yangu ni hii:


Kwa hiyo kwa sababu huwezi kushindana na Mh.Lissu jukwaani ndiyo ukaamua umuuwe ili uchukue jimbo kiulaini?Jipange upya Lissu yu hai na anarudi na nguvu ya ajabu.

Acha kuwewekeka.
 
Wadau habarini,

Miongoni mwa waliofanya makosa ya Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 ni wapiga kura wa Jimbo ya Singida Mashariki.

Ukweli Jimbo hili hadi leo bado lipo chini sana Kiuchumi ukilinganisha na Majimbo mengine.

Jimbo hilo linakabiliwa na changamoto kadha zikiwemo ukosefu wa huduma muhimu za Jamii.

Changamoto hizi kiukweli zimeendelea kuwepo pamoja na ahadi nyingi walizopewa wakazi hao kwa nyakati mbalimbali.

Wakati umefika sasa kwa wakazi hao kuamka mapema kwa kujiandaa ili muda muafaka utakapofika mfanye maamuzi sahihi ya kidemokrasia na kufuta makosa mliyofanya hapo awali.

Mnaweza tu kuondokana na hali halisi mliyonayo kwa kufanya maamuzi sahihi kwa kuzingatia ubora wa chaguo lenu badala ya kuchagua kiushabiki.

Msikate tamaa ila msifanye makosa tena.

Aksanteni.
Mngejua hata kura mlizopata 2015 singida mashariki 2020 mtazisikiaga tu mnashindwa kutushawishi kwa hoja mnakimbilia kumuuwa mbunge wetu...kwani shida zetu zitatatuliwa na mbunge kwani ndio mnaompaga kodi zetu mnazokusanyaga mbunge ni mwakilishi wetu tu anachowaambia hamumsikilizi sasa yeye afanyaje....2020 tunamrudisha kwa kishindo bungeni hata kama atakuwa anatambaa wauwaji wakubwa nyinyi
 
Wadau habarini,

Miongoni mwa waliofanya makosa ya Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 ni wapiga kura wa Jimbo ya Singida Mashariki.

Ukweli Jimbo hili hadi leo bado lipo chini sana Kiuchumi ukilinganisha na Majimbo mengine.

Jimbo hilo linakabiliwa na changamoto kadha zikiwemo ukosefu wa huduma muhimu za Jamii.

Changamoto hizi kiukweli zimeendelea kuwepo pamoja na ahadi nyingi walizopewa wakazi hao kwa nyakati mbalimbali.

Wakati umefika sasa kwa wakazi hao kuamka mapema kwa kujiandaa ili muda muafaka utakapofika mfanye maamuzi sahihi ya kidemokrasia na kufuta makosa mliyofanya hapo awali.

Mnaweza tu kuondokana na hali halisi mliyonayo kwa kufanya maamuzi sahihi kwa kuzingatia ubora wa chaguo lenu badala ya kuchagua kiushabiki.

Msikate tamaa ila msifanye makosa tena.

Aksanteni.
Wakati unazungumza haya ujue Ruangwa kwa Waziri mkuu Majaliwa hakuna maji na umeme wa uhakika. Pia Iramba kwa Mwigulu Nchemba, maji ni ya tabu sana. Je nako kukombolewe?
 
Kiufupi umenikera sana, ukitaka kujua hasira niliyonayo njoo na hoja hopeless kama hizi
 
Back
Top Bottom