Majibu ya Waziri Simbachawene hayaridhishi, kuna harufu ya ufisadi

Yaani kutakata kote huko ni 40 bilion za wizi!! Haki itendeke. Ndiyo maana nilikuwa nahimiza kauli ya hapa kazi tu iboreshwena kuwa HAPA KAZI NA HAKI TU.
 
Unaongea wakat huo akiwa waziri wa nishati wakat wa JK saiv ni tamisemi

Ndio, ufisadi hu emefanya miezi mitatu ya mwisho ya Uwaziri wake, septemba mpaka desemba 2015. Hata kama amehamia wapi kuwajibishwa ni lazima maadamu amefanya hilo kosa
 
Katika utetezi wake ndani ya gazeti la Mwananchi la leo, uamuzi wake wa kutofuata sheria ya Mamlaka ya udhibiti wa nishati na maji(EWURA) ya kushindanisha zabuni ya uingizaji mafuta nchini na hatimaye kufanya serikali kutumia bil 40 zaidi ya zile ambazo ingelitumia kama sheria ingefuatwa jambo lililosababisha bei ya mafuta isishuke nchini wakati ilikuwa chini soko la dunia, Waziri huyo wa Nishati na madini wa serikali iliyopita( ambaye kwa sasa ni waziri wa Nchi ofisi ya Rais,Tamisemi) anadai ni kwa sababu za wasiwasi juu ya hali ya usalama kipindi cha uchaguzi

Mimi sio mjuzi wa masuala ya uchumi na kiusalama lakini naamini tathmini ya hali ya kiusalama na madhara yake hufanywa na vyombo husika vya usalama, hasa shirika letu la ujasusi TISS ambao nadhani wanakitengo kinachohusiana na mambo ya uchumi. Sasa maswali yanakuja
1.Waziri alifanya tathmini akiwa kama nani? Alishirikisha mamlaka zipi?
2.Kwa nini hakufuata ushauri EWURA ambao walimshauri kuwa mafutwa yasiingizwe bila mzabuni ili bei isiwe juu


Waziri inasemekana ana uhusiano mkubwa sana na viongozi wa kampuni iliyopewa tenda hiyo, na pia ana ndugu yake anayefanya kazi kwenye hiyo kampuni. Pia baadhi ya watendaji wa kampuni hiyo alishauri au kuagiza wapatiwe ajira hapo( kinachoonekana maandalizi ya upigaji fedha huo)

Kuna shaka waziri atakuwa anahusika katika faida hiyo ya bil 40. Huu ni ufisadi, Hili jipu Rais Magufuli alitumbue

Waziri Simbachawene anatoa majibu ambayo hayaeleweki kabisa. Washauri, kama walivyo EWURA, wanaajiliwa ili watoe ushauri na ushauri yapaswa yazingatiwe kwani wao ni wataalamu na wanategemewa sana serikali. Iweje mtu kama waziri anayehimiza uadilifu atoe maamuzi yanahusisha Sh.40 billioni bila kufuata ushauri na taratibu na kanuni zilizowekwa?????
Kuna NAMNA, ni vema kufanyike uchunguzi zaidi, hili ni JIPU KUBWA. Huyu na yule aliyetuma sms kwa Mama CHUWA, hawanatofauti. Fuatilia
 
Waziri Simbachawene anatoa majibu ambayo hayaeleweki kabisa. Washauri, kama walivyo EWURA, wanaajiliwa ili watoe ushauri na ushauri yapaswa yazingatiwe kwani wao ni wataalamu na wanategemewa sana serikali. Iweje mtu kama waziri anayehimiza uadilifu atoe maamuzi yanahusisha Sh.40 billioni bila kufuata ushauri na taratibu na kanuni zilizowekwa?????
Kuna NAMNA, ni vema kufanyike uchunguzi zaidi, hili ni JIPU KUBWA. Huyu na yule aliyetuma sms kwa Mama CHUWA, hawanatofauti. Fuatilia

Kabisa mkuu
 
Inaonekana kazipiga yeye binafsi

majibu yake ni mepesi sana.

Huyu Simbachawene ilitakiwa hapa tunavyojadili hii habari awe tayari yuko Segerea. Kapiga dili la bilioni 42 kwa mgongo wa sisi walalahoi tunaotaabika sasa na kununua mafuta bei kubwa


kama taratibu na sheria za manunuzi zimekiukwa wahusika inabidi wachunguzwe na pamoja na kufunguliwa mashtaka.

inasikitisha kuona mamlaka kama PPRA na PCCB wakishindwa kuchunguza suala hili na kujua ni halali au batili.
 
Hii serikali imeshughulikia watendaji wa serikali ila haijawagusa wala kushughulikia wanasiasa wowote ambao kimsingi ndio walioifikisha hii nchi mahali ilipo iwe kwa mabaya yote.
 
kutumbua majipu ni kazi inayotakiwa kuombewa kama kweli kuna msikilizaji wake na mtattuzi. ni kazi sana kama ile methali isemayo "kikulacho ki nguoni mwako".
Yesu alisalitiwa na Yuda mmoja wa wafuasi wake. kuna wanaomsifu Magu tu ili waishi.
Kinachonitia hofu ni huu mtindo wa wasaidizi wa rais kuiga kwa mtindo wa mkuu wao. kila mmoja anasaka wakosaji kama majipu na kujifanya kutumbua huku nyuma kukiwa na kamera.
wanatatakiwa kuwa wabunifu na si kuiga. rais alibuni na kufanikiwa na wao wabuni mengine tuone wanaisukumaje nchi mbele. inaelekea ubunifu unakufa na wote tunaenda kwa mtindo uleule wa "ukuti ukuti!"
 
majibu yake ni mepesi sana.




kama taratibu na sheria za manunuzi zimekiukwa wahusika inabidi wachunguzwe na pamoja na kufunguliwa mashtaka.

inasikitisha kuona mamlaka kama PPRA na PCCB wakishindwa kuchunguza suala hili na kujua ni halali au batili.
Mkuu hata mimi nashangazwa na ukimya huo, ila naamini wanayafanyia kazi.
 
Hii serikali imeshughulikia watendaji wa serikali ila haijawagusa wala kushughulikia wanasiasa wowote ambao kimsingi ndio walioifikisha hii nchi mahali ilipo iwe kwa mabaya yote.
Tusubiri tuone
 
Akimwacha anamwogopa akimtumbua ni safisha ya mabaki ya mkwele akiwaamisha anawakumbatia. Tufuate lipi?
 
Katika vitu vinampa shida sana muda rais Magu ni mawaziri Wa jk waliochaguliwa tena awamu hii wengi WAo walizoeya rushwa tena grand corruption ukianzia huyo simbachawene kina makamba name wengneo SAS ili kuwatumbua HAWA jamaa na kumpunguziaa mzigo raisi hii ni opportunities kwa upinzani kutumia hizi gaps kumsaidia rais kutumbua majipu mana nao wapinzani wapo kimya hawafichui uvundo aina hii pak magazeti ndo wana mchango mkubwa kuweka wazii ufisadi mbalimbali.#TupazeniSautiUfisadiiTuumalizee
 
Anatakiwa awe mfano kwa mawaziri wengine


mngony;
Labda husomagi post za wengine ila tumeshasema saana tu kwa habari ya kuwajibika. CCM hainaga msamiati huo wa kuwajibika.
Hata mpige kelele Tz nzima, haifiki Magogoni au Mnazimmoja. CCM wanafarijiana kuwa; Huo ni upepo tuu unapita, utulivu unafuata punde.
Hatoki mtu hapo. Tena Simba cha wenyewe. Mmekoseaaaaaa
 
Katika vitu vinampa shida sana muda rais Magu ni mawaziri Wa jk waliochaguliwa tena awamu hii wengi WAo walizoeya rushwa tena grand corruption ukianzia huyo simbachawene kina makamba name wengneo SAS ili kuwatumbua HAWA jamaa na kumpunguziaa mzigo raisi hii ni opportunities kwa upinzani kutumia hizi gaps kumsaidia rais kutumbua majipu mana nao wapinzani wapo kimya hawafichui uvundo aina hii pak magazeti ndo wana mchango mkubwa kuweka wazii ufisadi mbalimbali.#TupazeniSautiUfisadiiTuumalizee
Magazeti ya The Citizen na Mwananchi ndiyo yaliandika, baada ya kama wiki hivi nikamsikia Mnyika akilizungumzia hili, sio mshabiki wa Chadema lakini nilifurahishwa na hilo, alisema wataliwasha bungeni hilo likifunguliwa. Hivi ndivyo jinsi ya kumuunga mkono Magufuli katika kuhakikisha taifa linasonga mbele na sio poroji, kejeli, maandamano n.k
 
mngony;
Labda husomagi post za wengine ila tumeshasema saana tu kwa habari ya kuwajibika. CCM hainaga msamiati huo wa kuwajibika.
Hata mpige kelele Tz nzima, haifiki Magogoni au Mnazimmoja. CCM wanafarijiana kuwa; Huo ni upepo tuu unapita, utulivu unafuata punde.
Hatoki mtu hapo. Tena Simba cha wenyewe. Mmekoseaaaaaa

Sawa limesemwa sana, lakini hakifanyi mtu mwingine asiliseme sana. Tuna haki ya kuendelea kusema kama raia katika yale tunayoona hayako sawa. Usichoke kusema
 
Mimi kilichoniuma na kunishangaza inakuwaje mafuta yanapita hapa kwetu yanaenda zambia bei yao ilikuwa chini na hata Kenya bei ilishuka hila Tanzania ilikuwa tofauti,wetu wenye dhamana fanyeni kazi kwa weledi mkijua mnaongoza tabaka maskini.
 
Kuna mtu mwenye takwimu zinazoeleza jumpa ya lita au tonnes za mafuta zilizoagizwa ktk kipindi hicho cha Simbachawene ili tukokotoe jumla ya cha juu kilicholiwa?
KWA kijiti cha yule mama ama??mt zilizimwa wapige kazi
 
Back
Top Bottom