Majibu ya Waziri Mwigulu Nchemba kuhusu tuhuma za kughushi vyeti vya taaluma, kuiba jina

Ila wewe ni kichwa period.

Tuwe wakweli, hakuna kusema wewe ni kichwa ,period. Maelezo ya Mwigulu bado yanazua maswali.Jina alilopewa na daktari alianza kulitumia lini? Ndilo aliloandikishwa nalo shule toka mara ya kwanza au alilitumia baada ya kurudi tena shule? Japo swali hili moja tu lijibiwe, halafu yaje maswali mengine. Ukweli utatuweka huru
 
Salama comrades?

Nimeiona thread hii: Mwigulu, Kigwangalla, Makonda jibuni tuhuma hizi nzito, aliyeandika naona hajui historia yangu.

Ni vema kuweka rekodi sawa:
Kwanza anasema nilikuwa nanaitwa Lameck Madelu Mkumbo, sasa moja Lameck sio jina la kinyiramba, na Madelu sio jina halisi la baba bali ni utani kuwa ana ndevu nyingi, yaani ni mandevu, ndio maana hata kwenye ubunge nililiongeza tu kama a.k.a ili watu hasa wazee wanifahamu hili haliko kwenye vyeti.

Hili la Lameck siyo jina la kinyiramba ni jina la daktari aliyenipokea zahanati ya Iliyopo kijiji cha Mukulu, daktari tunaita hivyo lakini ni Nesi ndiye aliyekuwa anaitwa Mwigulu na jina la kizungu Lameck. Mimi nilipelekwa hosipital nikiitwa Mugulo na jina la ukoo kwa watoto wote wakiume ni Shumbi ambalo hata hivyo wanatumia wazee tu wanaojua kinyiramba hilo ndio jina la kinyiramba. Mama akaulizwa jina akanitaja Nesi yule akamwambia mama unamwitaje jina hilo hakuna lingine mama akamwambia hakuna labda mtaje wewe, basi jamaa akajitaja. Hili lilikuwa jambo la kawaida sana kijijini kwani familia inakuwa na watoto wengi mpaka majina inakuwa sio jambo la kujali sana. Hata pale kijijini kuna wengine waliotajwa majina ya waganga wa kienyeji wazee walikopewa dawa, majina ya manesi/matabibu kama mimi, majina ya walimu nk.

Kuhusu Elimu:
Mimi niliacha shule kwa mara ya kwanza 1984 baada ya kuanza na kaka yangu aitwaye Jugulu, mzee akasema tupeane zamu, nikaacha. Nikaanza 1985, nikaachia darasa la tano nikaenda kuchunga miaka kama miwili. Nikarudi tena baada ya mifugo kuanza kufa sana, mzee akashauri awekeze kwenye elimu. Walimu walikuwa wanashinda nyumbani kumsihi anirudishe shule, ndio nikarudi na nikachukua majina ya daktari. Mtu asichanganye kuona ni udanganyifu, mimi sijachukua vyeti vya mtu. Nimefanya mitihani tena kwa kupiga na picha za passport ili mtu asitumie haki ya mtu mwingine aliyefaulu, na mpaka sasa naona ni struggle za mfano kuwa nilisoma kwa mazingira ya kutoka kuchunga na kurudishwa shule na kufaulu mwenyewe.

Kwa anayetaka kuthibitisha haya anaweza kuwauliza niliosoma nao shule ya msingi.

Comrades, kwa mawazo yangu kosa ni mtu kuchukua nafasi ya mtu aliyefaulu na kwenda yeye, hapo ni kuiba haki ya mtu. Najua hii ilikuwa ikitokea baadhi ya maeneo, mtu anafaulu ila anakuwa hataki kwenda shule au amefariki then anakwenda mwingine. Mimi sijawahi chukua nafasi ya mtu. Halafu watu wanasema jina la mtu, labda kama wanamaanisha tofauti na wizi wa jina kwani kila mmoja hapo alipo ana jina la mtu, yaani atakuwa John wa biblia, Mohamed wa quran, litakuwa la babu, la bibi, la mganga, la daktari, la rafiki, la kiongozi, la tukio nk.

Nijuavyo, jina unakula kiapo tu kama sio la kwako kisheria na unatumia, na hata sasa nikitamani jina jipya nakula kiapo na kutangaza gazeti la serikali na lisipopingwa ndio linakuwa jina langu jipya.

Hoja ni kama mtu kapora cheti cha mtu, kapora nafasi ya mtu mwingine aliyefaulu akaenda kuisomea yeye. But, things do change pia kutokana na nyakati na mazingira

Mwigulu,
Habari yeye ungempelekea aliyekuteua Uwaziri,basi.Ungekuwa umemaliza mchezo lakini kwa kuuleta hapa jamvini na niliyoyaona ndani yake,you are inviting more questions!!
 
Miye sikulaumu mweshimiwa bali na laumu mfumo wa elimu ambapo hauruhusu mwanafunzi kurudia darasa endapo akifeli darasa la saba wakati hakuna private school za sekondari za kwenda kuendelea kusoma kwa wale waliofeli drs la saba.

Nadhani utakuwa mhanga wa hilo kama walivyo watanzania wengi
 
Ndio tatizo la kuchimba makaburi!Kipindi cha nyuma ilikuwa kawaida kuomba kurudia shule ya msingi na kutumia jina la mtu mwingine sie Musoma tukiwaita ripiti tukimaanisha repeater.Kwa waliosoma zamani wanajua figisu figisu za kujiunga na sekondari zilivyokuwa na shule za private zilikuwa chache mno kiasi kwamba watu wengi walilazimika kurudia shule ya msingi ili kujaribu bahati ya kufaulu.Hakuna asiyejua katika hao wakubwa walioko huko sasa.Ni namna ya kuvuruga amani na utulivu tu lakini hii issue ilikuwa imeshamalizwa na mfumo uliopo sasa ambao ni imara na bora zaidi kuliko hapo zama zisizokuwa za digitali
 
Kwema mkuu Shumbi?

Kwanza nikupongoze kwa ujasiri wa kujitokeza hadharani na kujibu tuhuma hizi. Hakika huo ni ukomavu na uungwana uliotukuka.

Nimefurahi pia kujua maana ya neno Mwigulu na Madelu leo. Asante sana. Ila mzee, hapa tutakutwanga tu maswali kwa heshima na taadhima. Usitukimbie tafadhali..

Sasa mie swali langu ni moja tu hapo kwenye kuamua kuchukua majina ya huyo nesi/daktari.


Ninachouliza, yeye hakuwahi kusoma? Na kama alisoma alitumia majina gani? Huoni kwamba utakuwa umechanganya kuchukua jina lililowahi tumika kutahiniwa? Nadhani hapo ndio msingi wa maswali haya kuibuka...

Iliwezekanaje kutumia majina ya daktari kwenye taaluma ilihali na yeye aliyatumia pia?

Yaani daktari hakuwa shule, hakuwa umri wangu, alijitaja nilipopelekwa nikiwa na siku saba, kama hivi mtoto akizaliwa siku ya mwenge kule simiyu wapo wataitwa Mwenge, hivyo alinitaja, na kuna mtoto wa rafiki yake baba tulizaliwa wiki hiyo naye aliitwa jina la huyo nesi, sikuchukua jina kwa kuomba wala hatukuwa tunaongea mimi nilikuwa mchanga bhana
 
Nilidhani ulianza shule upya ndiyo maana ukabadili jina,kama uliendelea ulipoishia,kwanini ulibadili jina?na kama ukibadili kama taratibu zinavyoruhusu,je ulitangaza kwenye gazeti la serikali na wewe?
Huenda nimekuelewa vibaya katika maelezo yako,hasa pale uliposema kuwa uliporudi tena shule ndiyo ukaanza kutunia jina jipya.
 
Kiongozi wangu, ufafanuzi ulioutoa umejibu maswali yote ya msingi wewe ndiye mmiliki halali wa hilo jina kama kuna mwingine anahisi jina lake limeibwa basi atajitokeza na kupinga uhalali wako wa kulitumia au kulidai jina hilo mahakamani. Kimsingi jina siyo kitu cha kudumu, unaweza ukabadilisha kwa kutumia deed poll, wenzetu wanaruhusu kubadili majina yote uliyopewa (Given Names) kama unapofikia umri wa utu uzima na ukahisi hauyataki tena majina hayo au majina hayo ni kinyume na legacy yako ya kimaisha au itikadi yako mpya ya kidini basi unaruhusiwa kubadili. Kwa mfano, Bw. Ron Artest mchezaji wa mpira wa kikapu wa ligi ya USA (NBA) alibadili jina lake na kuitwa kwa sasa Metta World Peace. Kwa maneno haya mafupi, mjadala kuhusu majina ya muheshimiwa huyu amabaye anaonesha uwezo mzuri kwenye uongozi usivuke mipaka ya haki zake zinazotambuliwa kisheria.
 
Asante kwa majibu mheshimiwa, lakini inakuwaje muwe na majina tofauti hasa hili la tatu, kwani nimesoma na ndg mmoja anaitwa Shabani Mkumbo pale minaki anadai ni mdogo wako?
Salama comrades?

Nimeiona thread hii: Mwigulu, Kigwangalla, Makonda jibuni tuhuma hizi nzito, aliyeandika naona hajui historia yangu.

Ni vema kuweka rekodi sawa:
Kwanza anasema nilikuwa nanaitwa Lameck Madelu Mkumbo, sasa moja Lameck sio jina la kinyiramba, na Madelu sio jina halisi la baba bali ni utani kuwa ana ndevu nyingi, yaani ni mandevu, ndio maana hata kwenye ubunge nililiongeza tu kama a.k.a ili watu hasa wazee wanifahamu hili haliko kwenye vyeti.

Hili la Lameck siyo jina la kinyiramba ni jina la daktari aliyenipokea zahanati ya Iliyopo kijiji cha Mukulu, daktari tunaita hivyo lakini ni Nesi ndiye aliyekuwa anaitwa Mwigulu na jina la kizungu Lameck. Mimi nilipelekwa hosipital nikiitwa Mugulo na jina la ukoo kwa watoto wote wakiume ni Shumbi ambalo hata hivyo wanatumia wazee tu wanaojua kinyiramba hilo ndio jina la kinyiramba. Mama akaulizwa jina akanitaja Nesi yule akamwambia mama unamwitaje jina hilo hakuna lingine mama akamwambia hakuna labda mtaje wewe, basi jamaa akajitaja. Hili lilikuwa jambo la kawaida sana kijijini kwani familia inakuwa na watoto wengi mpaka majina inakuwa sio jambo la kujali sana. Hata pale kijijini kuna wengine waliotajwa majina ya waganga wa kienyeji wazee walikopewa dawa, majina ya manesi/matabibu kama mimi, majina ya walimu nk.

Kuhusu Elimu:
Mimi niliacha shule kwa mara ya kwanza 1984 baada ya kuanza na kaka yangu aitwaye Jugulu, mzee akasema tupeane zamu, nikaacha. Nikaanza 1985, nikaachia darasa la tano nikaenda kuchunga miaka kama miwili. Nikarudi tena baada ya mifugo kuanza kufa sana, mzee akashauri awekeze kwenye elimu. Walimu walikuwa wanashinda nyumbani kumsihi anirudishe shule, ndio nikarudi na nikachukua majina ya daktari. Mtu asichanganye kuona ni udanganyifu, mimi sijachukua vyeti vya mtu. Nimefanya mitihani tena kwa kupiga na picha za passport ili mtu asitumie haki ya mtu mwingine aliyefaulu, na mpaka sasa naona ni struggle za mfano kuwa nilisoma kwa mazingira ya kutoka kuchunga na kurudishwa shule na kufaulu mwenyewe.

Kwa anayetaka kuthibitisha haya anaweza kuwauliza niliosoma nao shule ya msingi.

Comrades, kwa mawazo yangu kosa ni mtu kuchukua nafasi ya mtu aliyefaulu na kwenda yeye, hapo ni kuiba haki ya mtu. Najua hii ilikuwa ikitokea baadhi ya maeneo, mtu anafaulu ila anakuwa hataki kwenda shule au amefariki then anakwenda mwingine. Mimi sijawahi chukua nafasi ya mtu. Halafu watu wanasema jina la mtu, labda kama wanamaanisha tofauti na wizi wa jina kwani kila mmoja hapo alipo ana jina la mtu, yaani atakuwa John wa biblia, Mohamed wa quran, litakuwa la babu, la bibi, la mganga, la daktari, la rafiki, la kiongozi, la tukio nk.

Nijuavyo, jina unakula kiapo tu kama sio la kwako kisheria na unatumia, na hata sasa nikitamani jina jipya nakula kiapo na kutangaza gazeti la serikali na lisipopingwa ndio linakuwa jina langu jipya.

Hoja ni kama mtu kapora cheti cha mtu, kapora nafasi ya mtu mwingine aliyefaulu akaenda kuisomea yeye. But, things do change pia kutokana na nyakati na mazingira

Mwigulu,
 
Bado kuna ukakasi kwenye maelezo yako, ukisema jina la MADELU lilikuwa la utani kwa kumaanisha mandevu inaleta shaka. Huku kwetu Mbeya kuna akina Mwafilombe(Mahindi), Mwambatata (Viazi vitamu) Mwakajumba (mwenye nyumba) Afyusisye (amejamba) na memngineyo mengi yanayo fanana na hayo lakini si yautani ni majina halisi yanatumika pahala pote tuendapo. So please, kwenye Madelu hapo hapako sawa.
Namuomba Mh. H. Kigwangala asimame kisha atafuatiwa na Mh. P. Makonda.
 
Taratiiibu Ukweli unaanza kudhihiri,Kama akaunti yake haikuingiliwa na mtu yeyote,Mh.amekiri kwa kinywa chake kuwa majina anayoyatumia si majina yake ya kuzaliwa,hayo ni majina ya muuguzi wa hospitali ya kijiji alikozaliwa na alianza kuyatumia mara tu aliporejea shule mara ya pili baada ya awali kuacha shule ili achunge mifugo.

Hii movie inavutia sana,kuiangalia nikiwa nimeketi inaweza ikaniumiza mgongo,ngoja nijilaze chini kabisa ili niifuatilie hatua kwa hatua............
 
Yaani daktari hakuwa shule, hakuwa umri wangu, alijitaja nilipopelekwa nikiwa na siku saba, kama hivi mtoto akizaliwa siku ya mwenge kule simiyu wapo wataitwa Mwenge, hivyo alinitaja, na kuna mtoto wa rafiki yake baba tulizaliwa wiki hiyo naye aliitwa jina la huyo nesi, sikuchukua jina kwa kuomba wala hatukuwa tunaongea mimi nilikuwa mchanga bhana
kama ulikuwa na siku saba kwanini uje tena kuchukua jina ulipoacha darasa la tano?
 
Natamani na MBOWE ajitokeze kujibu tuhuma zake.
Na siku Mbowe akijitokeza basi nijitoa kabisa kushabikia siasa.
Na mwenye kusoma PhD kwa miaka 3 badala ya 5 aje nae hapa ajibu tuhuma zake tena yeye akiwa ndio kiongozi mkubwa.

Atueleze alisomaje kwa miaka 3 kama mwanafunzi wa "full time" huku akiwa kiongozi mwandamizi serikalini tena mwenye majukumu mengi.
 
Hongera mkuu kwa ujasiri wako wakuja na kutolea ufafanuzi jambo hill. We we ni kiongozi wa kuigwa kwani unatambua umuhimu na nguvu ya JF katika kupashana habari. Viongozi wengine waige hili nakama wanajambo la kulisemea hapa JF ni vyema wakalisemea. hili litatuongezea imani kwa viongozi wetu.
 
Back
Top Bottom