Majibu ya Waziri Mwigulu Nchemba kuhusu tuhuma za kughushi vyeti vya taaluma, kuiba jina

mwacheni kiongozi,watu wanatapatapa hawana pa kushika,tuache kuzushiana wadau haina msaada wowote ile.majibu mazuri nimefurahi kwa kweli

Once muongo always muongo.
Atujibu na kwa nini kuna tofauti ya tarehe za kuzaliwa katika vyeti vyake vya shule?

 
kwanza aliporudi baada ya miaka miwili tayari wenzake hawakuwepo walikuwa washamaliza shule, hivyo alikaririshwa darasa, akubali kuwa alifeli akalamba jina la msukuma, labda nesi ndiye aliyemtafutia msukuma huko kwao akaliamishaia shule anayodaiwa kusoma ili aonekane mpya.
 
Nazidi kujifunza lakini bado sijakuelewa mkuu... Why kasoro mingi mingi namna hii.

By definition you are a liar
 
Mkuu umefanya vizuri kutuelekeza. Binafsi nimeelewa na nimependa maelezo yako

Naomba kakitengo kokote basi

Ukikakuta ka kunipatia PM me Sir.

 
mkuu bwana Mwigulu hivi ulipo katiza masomo ulikuwa na jina jingine na ulipo rudi ukatumia jina jingine swali linakuja je uliendelea na darasa uliloachia kwa jina jipya au ulianza.darasa la kwanza kwa hilo jina la nesi dokta?
 
m
mkuu kuna post ya ID frank haijajibiwa
 
Hata mimi ki utu uzima nimemuelewa,mambo mengine itakuwa ufukunyuku tu,tuendelee kupiga kazi!
Mkimuelewa waziri wetu kwenye hili, basi muwaelewe wote wenye vyeti siyo vyao na majina siyo yao...

Unajuwa kwenye process ya kusoma shule, kama katika steji moja ulipita visivyo halali, basi madarasa yote uliyofika kwa kuwezeshwa na steji isiyo halali, NAYO YANAKUWA SI HALALI... MI NAIONA NI KAMA KUTAKATISHA FEDHA....
 
Majina hufanana kisha kutofautishwa na namba za mtahiniwa (Index Number).

Maswali mengine jiongeze tu
 
Kama huu mjadala wa Mwigulu ndo kwanza umeuona hapa hutajua cha kuchangia ila kama umefuatilia thread mbili kabla utaelewa amejitetea nini kukusaidia nitakuwekea link zake pale juu sasa hivi vinginevyo huna sababu ya kuuliza kwa jazba.

Niwekee hizo link, halafu ufanye haraka dogo.....tehtehtehteh
 
Mheshimiwa mbona umepata kigugumizi? wajibu basi wana jamvi maswali yao ili waondoe dukuduku, maana inaonekana kuwa maelezo yako hayakukamilika. Hivi ulidhani kuwa wana jamvi hapa ni watu wasiokuwa na upeo? na ndiyo maana ukaleta hayo maelezo yako yanayochanganya changanya hapa? Kama ingekuwa umeyatoa pale kariakoo sokoni basi hakuna shaka usingepata challenge zozote, lakini hapa siko. Tafadhali wajibu basi hao vijana hayo maswali yao ili tuujue ukweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…