Maji Uhai yana ladha mbaya

Maji Uhai yana ladha mbaya

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,255
Reaction score
16,185
Maji ya kunywa ya uhai yana ladha mbaya chumvi isiyofaa kwa matumizi ya kunywa. Hivi wanachota baharini? TFDA na tbs toeni majibu kuhusu maji haya. Kunywa Chumvi nyingi kuna madhara kiafya.


A True story: siku moja nilitembelea afisi moja ya mmojawapo wa wamiliki wa kampuni zinazotengeneza maji ya kunywa ya chupa (sio uhai), mmmh nilishangaa kuona mezani kwake yako maji ya kunywa ya chupa ya kampuni nyingine, nikashikwa na butwaa kwanini yeye mwenyewe hanywi maji ya kampuni yake. Nilipomuuliza yule ambae alinisindikiza kwenye afisi ile ambaye ni fundi umeme wa kampuni ile ya kutengeneza maji akasema bosi wao (owner) hajawahi hata kuyaonja maji yake. Wewe unaonaje tukio kama hili?
 
Halafu mi nikinywa yananifanya nikakojoe mara kwa mara
 
Utadhàni kuwa yamechotwa baharini, maji ya kunywa ya Uhai yana ladha ya chumvi nyingi isiyofaa kwa kunywa na kutuliza kiu
TFDA na tbs mko wapi?
 
Uhai ipi hiyo uliyokunywa yenye chumvi nyingi?
 
Utadhàni kuwa yamechotwa baharini, maji ya kunywa ya Uhai yana radha ya chumvi nyingi isiyofaa kwa kunywa na kutuliza kiu
Tfda na tbs mko wapi?

ushaingizwa mjini aisee.
hapo sio uhai wala nini, umeuziwa feki; waswahili wanasema umepigwa KANYABOYA.
 
Kwani haya maji yaandaliwa wapi? Source ya hayo maji ni baharini? Visimani? Mtoni?
 
Hayo maji hayana ladha kabisa, hata ukiangalia hafla mbalimbali za kiserikali huwezi kuyaona huko
 
Bidhaa nyingi za Azam ubora wake upo chini sana, ni kwa vile hakuna ushindani wa kutosha ndio maana tunaridhika nazo....

Nashauri hata hiyo TBS ipimwe ubora wake maana bidhaa inazopitisha ni duni sana
 
Hivi hata Maziwa ya Azam anatoa wapi...!!? Ng'ombe wake wako wapi...!!? Lini kaanza kufungua mashamba ya ng'ombe wa maziwa...!!? Sbb Tanga Fresh wana shamba kubwa la ng'ombe Tanga.....as well Asas Milk ana mashamba ya ng'ombe wa maziwa makubwa 3 Iringa na Mikumi...!!!!

Ubora wa bidhaa za Azam ni mashaka sana....mm sijawahi kunywa au kununua maziwa yake...sbb sijui anatoa wapi maziwa nchi zima...wakati sijana shamba anakofugia ng'ombe...hii ni hatari sana...!!
 
Back
Top Bottom