Maji ni rasilimali inayoweza kukutajirisha kwa muda mfupi bila jasho

sepema

JF-Expert Member
Jun 13, 2019
591
1,000
Wakuu salaam...

Nimekaa kupiga stori na mzee mmoja aliebahatika kutumia kiinua mgongo chake kufany biashara ya maji.
Mzee amegeuza changamoto ya maji katika eneo lake kuwa fursa ya kiuchumi.

Amechimba maji ardhini kwa gharama ya shilingi 15m.Hizo ni gharama zote hadi maji yametoka.
Kwasiku anadai anauza kiwango Cha chini 300k.

Kimahesabu nikwamba kwa wiki anakusanya 2.1m,ambapo kwa mwezi ni zaidi ya milioni8!. Hapo hapo anatumia maji hayo kumwagilia bustani yake yenye mboga zamajani,mipapai, migomba na matunda mengine.
Ni fursa yenye pesa japo inahitaji mtaji wakutosha.

Sijaona changamoto zake zaidi ya maintenance ndogondogo.

Wasalaam!
 
Back
Top Bottom