Bwana
Zitto, Kosa kubwa lililofanyika na nyie wabunge mlihusika ni pale ambapo miradi wa maji vijijini kupitia mkopo wa benki ya dunia ulifanyika pasipo weledi.
Nitafafanua:
1. Mradi ulihusisha manunuzi ya kimataifa kuanzia utafutaji wa vyanzo vya maji hadi utekelezaji. Hivyo gjarama ikawa kubwa sana.
2. Mradi ulilenga maji ya visima. Kwa kudhani kila eneo la nchi hii lina maji chini ya ardhi. Hata pale kijiji kilikuwa pembeni mwa ziwa waliambiwa kuchimbiwa kisima. Hapakuwa na utafiti madhubuti kuhakikisha kwamba maji chini ya ardhi yapo eneo hisika. Siasa iliingilia hasa diwani au mwenyekiti wa kijiji alipolazimisha kisima kichimbwe nyumbani kwake. Matokeo yake visima vingi vilikosa maji.
3. Dhana ya kila kijiji kuwa na chanzo chake huongeza gjarama za miradi. Huongeza gharama za uendeshji na haiwezekani. Tulitakiwa kuwa na miradi mikubwa ya kuhudumia eneo kubwa. Kuchagua vyanzo vichache visambaze maji nchi nzima. Mijini na vijijini.
Mfano ni kama hii miradi ya kitaifa inavyofanya kazi. Au mradi wa KASHWASA. Maji hutolewa kwenye chanzo kimoja na kusambazwa maeneo mengi ya nchi. Mijini na vijijini.
Nchi hii tunahitaji vyanzo vya maji visivyozidi vitano. Kwanza ni ziwa Victoria. Maji yake yasambazwe mikoa ya Mara, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Dodoma, Kagera, Singida, Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Pwani, Morogoro, Dar na maeneo ya jirani.
Pili ni bwawa la Stieglers Gorge. Maji yake yasambae maeneo ya Dar, Pwani, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Morogoro na Iringa.
Chanzo kingine ni Ziwa Nyasa. Maji yake yasambazwe maeneo ya mikoa ya Ruvuma, Mtwara, Mbeya, Njombe na Iringa.
Mwisho ni Ziwa Tanganyika ambalo litagawa maji maeneo ya mikoa ya Katavi, Kigoma, Rukwa na maeneo ya jirani.
Mabwawa makubwa kama Mtera na Ziwa Rukwa vitakuwa ni vyanzo vya ziada kwa maeneo ya jirani.
Kusambaza maji kwa kuchimba visima kila kijiji ni aghari sana na si endelevu kuliko BULK SUPPLY.