Mwifwa
JF-Expert Member
- Apr 3, 2017
- 48,721
- 126,568
Wazee wa ndioo Bunge ni akina nani?Sawa, Bunge liko wapi katika hili? naamini unasukumwa kusema hivi kwa sababu majimbo mengi yaliyorudiwa uchaguzi chama chako kimepoteza nafasi.
Wabunge wengi ni wa Chama gani?
Kwa nini hao hao wabunge ambao wana nguvu kupitisha mambo wanashindwa kukemea haya mambo ya kipuuzi?
Hata kama chama chochote cha upinzani kingeshinda hasara ni ileile, Serikali badala ya kujikita kufanya miradi mbali mbali kama hili suala la maji vijijini yenyewe inajikita kwenye marudio ya uchaguzi.
Hivi kweli tuna nia na nchi ya Viwanda na uchumi wa kati ilihali kuchimba visima vya maji imetushinda? Tuko serious kweli!!
Serikali inatakiwa ikubali juu ya matatizo muhimu kama haya na kuyapatia ufumbuzi kuliko na kuhangaika na mambo ya kipuuzi yasiyokuwa na tija kwa Taifa.