Maji ni Mtego wa Umasikini (poverty trap)

Maji ni Mtego wa Umasikini (poverty trap)

Aisee ndugu Zitto analysis yake kuhusu maji ni sahihi kabisa.

Karibu saana mheshimiwa. Tunahitaji fikra zako pevu.
 
Utawala wa CCM umelaaniwa.

Wewe angalia maeneo ya Temeke, Mbagala, Mkuranga kuna shida kubwa ya maji lakini toka Mbagala hadi mto Rufiji ni kama kilometers 100 tu, lakini serkali za CCM zimeshindwa kuvuta maji toka mto rufiji kuja mkuranga, Mbagala na Temeke.

Watu maeneo hayo wanakunywa maji ya visima vya mavi, lakini mamilioni ya lita za maji ya mto Rufiji yanamiminikia baharini kila siku.

Bomba la gesi limeweza kutoka Mtwara hadi Dar wanashindwaje kuchukua maji Rufiji kuleta Dar?
 
Hatuwezi kufanya hayo mnayoyasema,

Msitupangie vya kufanya,

Kama vipaumbele vyenu ni maji na Afya sisi vipaumbele vyetu ni fly-over,treni na kubomoa nyumba za watu ili tupanue bara bara,

Nawahakikishia kwamba hatupangiwa
 
Ni aibu sana kwa taifa lililo na mazingira kama yetu kuwa na tatizo la maji. Aibu kwa watawala kuishi katika kila aina ya privilege wakati hawataki kutoa nafasi angalau ya watu wengine kutoa mawazo yao kuhusu mustakabali wa nchi yetu.
 
Painfull facts.. CCM wao wako busy na biashara ya madiwani na wabunge?
Tutafika tu
 
brilliant analysis....

karibu tena jukwaani comrade zitto, umeadimika si kidogo kipindi hiki unahitajika sana.
 
Najua ipo tutafika kwenye nchi ya maziwa na hasali cha msingi ni kuvumilia na kufanya kazi
 
Utawala wa CCM umelaaniwa.

Wewe angalia maeneo ya Temeke, Mbagala, Mkuranga kuna shida kubwa ya maji lakini toka Mbagala hadi mto Rufiji ni kama kilometers 100 tu, lakini serkali za CCM zimeshindwa kuvuta maji toka mto rufiji kuja mkuranga, Mbagala na Temeke.

Watu maeneo hayo wanakunywa maji ya visima vya mavi, lakini mamilioni ya lita za maji ya mto Rufiji yanamiminikia baharini kila siku.

Bomba la gesi limeweza kutoka Mtwara hadi Dar wanashindwaje kuchukua maji Rufiji kuleta Dar?


Punguza jazba unavyokuwa unachangia hoja za msingi zenye maslahi ya taifa letu. Sidhani kama unafahamu maana ya laana?
Tuishauri serikali kupitia wawakilishi wetu, serikali ya ccm ni sikivu haitaacha mawazo mazuri yapotee. Hili taifa ni letu sote tuache mahaba tuisaidie hii serikali kutatua matatizo yetu na siyo kubeza.
 
Karibu sana Mh umepotea sana jukwaani.

Ni kweli kabisa tatizo la maji vijijini ndio kikwazo kikubwa cha maendeleo na ndio chanzo cha umasikini pia.
Kuna mambo ambayo serikali inayafanya na hayana tija kabisa kwa wananchi kama hili la ukosefu wa maji kwa wananchi vijijini.

Ikumbukwe pia wananchi wa vijijini ni wazalishaji kupitia kilimo, kama kiasi kikubwa cha fedha wanakitumia kugharamia maji, mipango na bajeti yabuzalishaji mali kupitia kilimo japo sio cha kisasa lazima ipungue hatimaye wanaendelea kudumbukia kwenye umasikini.

Salama,
Ni mambo yapi ambayo serikali inafanya hayana tija kwa wananchi? Bunge letu liko wapi? katika hayo mambo ambayo unaamini serikali inafanya hayana tija kwa wananchi wake?

shukrani!
 
Salama,
Ni mambo yapi ambayo serikali inafanya hayana tija kwa wananchi? Bunge letu liko wapi? katika hayo mambo ambayo unaamini serikali inafanya hayana tija kwa wananchi wake?

shukrani!
Kupoteza mabilioni ya pesa kwenye chaguzi za marudio kuna tija yoyote kwa Taifa zaidi ya kupata hasara?
 
Kupoteza mabilioni ya pesa kwenye chaguzi za marudio kuna tija yoyote kwa Taifa zaidi ya kupata hasara?

Sawa, Bunge liko wapi katika hili? naamini unasukumwa kusema hivi kwa sababu majimbo mengi yaliyorudiwa uchaguzi chama chako kimepoteza nafasi.
 
Tatizo ambalo naliona kwa wanainchi ni kwamba wanapenda mteremko sana. Niliishigi Kwimba nakumbuka tulifanyaga mpango wa kupata maji ya bomba tukajichanga changa sisi watumishi wa tatu tukavuta maji yakaja. Cha ajabu nashangaa mama mwenye nyumba akaja na biashara yake ya mama ntilie.

Mi nasema wacha wengine wakose maji tu na waumwe matumbo kwa sababu hawataki kuwajibika maana wanataka maji alafu kuyalipia hawataki.

Mimi nilifundishwa na baba yangu kwamba unafanyia kazi kila kitu. Wanainchi waonyeshe njia sio kukaa na kuletewa mradi

Mkuu unajua vijijini kuna watu wananunua Maji ya dumu la Lita 20 kwa shilingi mia tano, una jua kuna sehemu watu wamevuta mabomba lakini unapita mwezi Maji hayajatoka?

Vijijini hali ya upatikani ni mbaya sana na wananchi wake ni masikini.
 
Everything is a trap in this country.

Lack of water is a trap....lack of electricity is a trap....poor roads is a trap....poor healthcare is a trap.....don't even mention the education system!

All one vicious cycle designed to keep us perpetually deprived
 
Tatizo ambalo naliona kwa wanainchi ni kwamba wanapenda mteremko sana. Niliishigi Kwimba nakumbuka tulifanyaga mpango wa kupata maji ya bomba tukajichanga changa sisi watumishi wa tatu tukavuta maji yakaja. Cha ajabu nashangaa mama mwenye nyumba akaja na biashara yake ya mama ntilie.

Mi nasema wacha wengine wakose maji tu na waumwe matumbo kwa sababu hawataki kuwajibika maana wanataka maji alafu kuyalipia hawataki.

Mimi nilifundishwa na baba yangu kwamba unafanyia kazi kila kitu. Wanainchi waonyeshe njia sio kukaa na kuletewa mradi
Hayo maji mliyovuta watumishi watatu mlivuta toka sehemu gani? Na mlichanga kiasi gani?
 
Huwa nashangaa sana Tanga jiji kupata maji toka Muheza mto Zigi,cha ajabu pale Muheza maji yanakotoka kuna shida ya maji ni balaa,nadhani tumekosa vipaumbele kama nchi.
 
MaCcm wapo bize kununua wabunge na madiwani huku wakina mama wana uwawa na mamba
 
MH ZITTO HAMNA NAMNA NYINGINE UNAWEZA HAMASISHA WANANCHI WAJIUNGE KWA FEDHA NA KUJITOA BINAFSI KUJENGA BOREHOLES?MANA SIDHANI KAMA KUNA MSAADA UTAKAA UPATIKANE KUTOKA HUKO TUNAKOTEGEMEA.

UKIANZISHA MOVE KAMA HIYO NI RAHISI KUSAMBAANCHI NZIMA,WATU KUJUA HAMNA CHA KODI WALA NINI KITAKACHOTUOKOA,TUJIORGANIZE THEN TUTATUE CHANGAMOTO ZETU.

UBINAFSI UMETUFIKISHA HAPA KWA HIYO KUUPUNGUZA ITASAIDIAITASAIDIA KULETA ORDER,THEN TUTAPATA UBUNIFU WA KUJINASUA.
 
Back
Top Bottom