Majesuit walivyojipenyeza kwenye makanisa

Majesuit walivyojipenyeza kwenye makanisa

Wengine tumeshachoka kubishana na uongo mweupe kama huu. Hizi hadithi ni tamu kwa wasiojua historia ya Kanisa.

Huwezi amini porojo hizi wanafundishwa hadi wachungaji kwenye shule zao! Ukitoa makanisa makubwa kama Lutheran, Anglican n.k haya ya kiroho wanawekwa darasani na kujazwa maungo kama haya juu ya Kanisa Katoliki.

Mtu anajazwa huu uongo alafu hajiangaishi kuchimba kweli. Kweli ipo na siku hizi hata Google inaweza kukusaidia.
 
Wasabato bana....[emoji23][emoji23][emoji23]hivi nyie Wasabato inaonekana adui yenu sio shetani bali Wakatoliki [emoji23][emoji23][emoji23] kilasiku mnakuja na mapokeo yenu ya kuwaponda Wakatoliki lakini cha kushangaza wanazidi kupata wafuasi wengi duniani kuliko dhehebu lolote la kikristo [emoji38][emoji38]
Sio wasabato tu, wao ndio watunzi wakuu wa hizi hadithi lakini makanisa ya kiroho yamekopa hizi porojo na ni sehemu ya syllabus zao shule za wachungaji. Kwasasa hizi hadithi zinaenezwa zaidi na watu kutoka hayo makanisa ya kiroho.

Hizi porojo ukimpa hata mchungaji wa Lutheran au Anglican watazikataa wakati wao ndio founder wa reformation.
 
Wamekuwa wakitumia mgongo wa kusaidia jamii kupitisha ajenda zao

Mfano elimu na afya


Hapa Moshi Kuna Center inaitwa RAINBOW CENTER , Ni wao
Hapo kama unaenda stendi ya KCMC maeneo ya njia panda ya kwenda Uru wana makazi yao acha watumikie Kanisa kwa sie tuliopitia Seminari na kutumikia misa hapo Kristu Mfalme miaka ya kuanzia 1991 hadi 1997 tunajua umuhimu wao kwa muda mchache huo kipindi cha Paroko Padre Amani
 
Wamekuwa wakitumia mgongo wa kusaidia jamii kupitisha ajenda zao

Mfano elimu na afya


Hapa Moshi Kuna Center inaitwa RAINBOW CENTER , Ni wao
Kanisa gani halifungamani na RC....utasikia Adventist
 
1. SOMALIA
2. IRANI
3. AFGHANISTANI.
4. NORTH KOREA

Na nyingine zitafute utazipata na zipo nyingi tu.
somalia wakristo niwengi tu mbona, pia swala la dini na tamaduni ni kama pipa na mfuniko,kuna nchi toka zama zakale zimekuwa zimekuwa zikiishi kwamisingi yakidini na tamaduni flani anapoJitokeza mmoja wapo anaetakakupenyeza mambo yake yakidini au kitamaduni kwenye eneo au nchi ambayo haifati misingi hiyo yakidini huo unakua ni UKOROFI, yani mtu aende kufungua kanisa saudi arabia huo siniukorofi? Nchi kama north korea wanafata dini zao zajadi hakuna waislam wala wakristo kule utakapojaribu kuwaingizia tamaduni mpya lazima watareact tu, pia nchi ya myanmar kunakipindi walikuwa wakiwaua waislam wajamii flani kule kwao wakidai wanaharibu tamaduni na dini zao zakibudha, hata huko china kunawaislam wanauliwa kimyakimya kulinda tamaduni zakichina zisipotee.....kwahiyo hili tatizo lipo kila dini sio kwa wakristo au waislam pekee hata wenye dini nyingine wanaface hili tatizo
 
Kama hata wapentekoste wameingia kwenye mtego huo ni wapi sehemu salama ya kuabudia?
 
Wazishikao amri za Mungu Na imani ya Yesu
Mfumo wa kiuendeshaji wa kisabato hauna kiongozi Mkuu wa sehemu kwa mfano Kijiji, kata, wilaya, Mkoa , Taifa au kikanda kama Afrika Mashariki. Ambao hukutana kwa kipindi fulani kupeleka taarifa.?
 
Usibishe kitu Kama hujui , nitaanza na Moja Moja hapo kukuonesha ,Majesuit wameshayateka


Kwanza unajua hao wote uliowataja hapo Juu Wana chama Chao CPCT ,na mwakilishi wao huenda kwenye mkutano na vikao vya eukumen ?

(1.) Makanisa ya TAG;


(2.) Makanisa ya PAGT;

(3.) Makanisa ya VICTORIUS;

(4.) Makanisa ya CALVARY;

(5.) Makanisa ya FGBF;

(6.) Makanisa ya EAG(T);

(7.) Makanisa ya FPCT;

(8.) Makanisa ya RGC;

(9.) Makanisa ya GCCT;
sibishi, ila miaka ya nyuma makanisa haya yalikuwa na misimamo migumu kuhusu kujiunga na jumuiya za kikristo. Hii CPTC wameianzisha miaka ya hivi karibuni baada ya kuona wenzao wa CCT wako pamoja na wanatambuliwa na serikali kiasi cha kupewa airtime kwenye media za umma
 
Mwandishi ni msabato,mkuu unapoteza energy pasipo sababu yoyote ya msingi dini zote iwe ya kiislamu au ukristo tumeletewa na watu weupe relax kunywa maji mengi na punguza chuki kwa ukatoliki unajisumbua na kuhangaika bure.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna kiongozi mmoja wa juu wa kanisa moja la kipentekoste kapata ukuu ameleta mambo yake mapya, hakuna wa kumpinga, mmojawapo ya mambo mapya ili uwe mzee wa kanisa lazima uwe na diploma
Makanisa yote sasa yapo hivo
 
Back
Top Bottom