UHAMIAJI ndio kumeoza. Wahindi, wachina na wageni wengine wanapewa "working permits" pasipo hata kutia saini.
Pale akiba Dar, pale makao makuu ya Mambo ya ndani, pale Samora nyuma, hapa ofisi ndogo ya uhamiaji Nyerere jirani ya mnazi mmoja, na sasa kule kurasini...yaani nawajua washkaji zangu kibao wanapiga dola kwa kuchezesha dili za kuwatafutia working permits na kuwafanyia renewal ya working permits zao.
Nawajua wahindi na wanyarwanda wengi sana wasiokuwa na vibali hapa nchini, tena Mwanza na Dar ndo usiseme.
Central govt ishughulike zaidi na Uhamiaji, yaani idara hiyo ibanwe vilivyo.
JK: tafadhali tupatie links tusaidie TISS na idara zako nyeti tuwamwagie mambo yaliyopo na yanayojiri, data tunazo na tuwaelekezeni walipo mjionee madudu ambayo yanaligharimu taifa sasa.
Ukienda pale Mbeya hususan wilaya ya Chunya na maeneo ya Makongolosi, matundasi, Saza, Mkwajuni...huwezi kuamini yaliyopo huko. Wazambia, Wazimbabwe na wachina wamejazana mno kule na siku hizi wanaongea viswahili na huwezi kuwakuta Dar au Mwanza. Wapo na tunawajua fika.
Tuwekeeni links kama alizotuwekea RC wa Geita, ila muweke na emails bana tuwasaidie sisi wananchi.