Majeshi ya Tanzania na huduma za dezo

big up kwa dereva anaejiamini mbele ya haki yake japo huyu MJEDA MPUMBAVU BADAE ALIPIGIA WENZAKE CM WATEKE GARI NJIANI KUA KAFANYIWA FUJO, bila hata kujua watu mle kwenye gari wana nyadhfa zao walikua wanangoja gari itekwe ili badae wawe mashahdi mahakamani isitoshe kulikua na majaji kama 2 waliokua washarekodi mkanda mzima wa tukio
RAI YANGU..msifanye fujo kwenye magari kabla hamjajua nyadhifa za watu waliopo ndani ya gari
 
Mkuu ni kawaida ya sisi waafirika kupenda vitu vya bure kwa hivo msimsimange mwacheyeni tu
 
Mkuu ni kawaida ya sisi waafirika kupenda vitu vya bure kwa hivo msimsimange mwacheyeni tu

Hakuna ukweli wowote wa hiyo taarifa kutafuta kick tu we ujaelewa anavyosema watu wananyadhfa zao kwamba na yeye aonekane yumo kumbe tapeli tu.
 
Mshahara wa askari private kabla ya kukatwa kodi ni Tshs 170,000 approx. Na allowance ya chakula kama Tshs 50,000 hivi kwa mwezi! Ofisa wa ngazi ya chini ni sh 350,000 kabla ya kodi!!! Huko ni kulipwa vizuri??? Na Jenerali ana 1.5M, gari + extra allowances whats the difference nafikiri mishahara mizuri ni ya wanasiasa sio wanajeshi. Hawasemi kwa vile ndio maadili yao lakini hawana amani hata kidogo na hawana wa kuwasemea, Hata wabunge wanakwenda maeneo ya wanajeshi wakati wa campaign tu then mbunge gani ulimsikia akitetea maslahi ya wanajeshi? Viongozi wao ni mabilionea, remember Mb..ma with meremeta na Tanzanite + Wa...tara ni mwenye pesa nyingi sana lakini wanajeshi sasa hata kuipata kombati unatoa rushwa!

Mkuu ni wazi kabisa huna idea yeyote kuhusu mishahara ya jeshi, Nadhani umetaja mshahara wa Mgambo na KK SECURITY ila sio JWTZ . In short hakuna Private wa jeshi anayelipwa chini ya 600000/= per month.
 
big up kwa dereva anaejiamini mbele ya haki yake japo huyu MJEDA MPUMBAVU BADAE ALIPIGIA WENZAKE CM WATEKE GARI NJIANI KUA KAFANYIWA FUJO, bila hata kujua watu mle kwenye gari wana nyadhfa zao walikua wanangoja gari itekwe ili badae wawe mashahdi mahakamani isitoshe kulikua na majaji kama 2 waliokua washarekodi mkanda mzima wa tukio
RAI YANGU..msifanye fujo kwenye magari kabla hamjajua nyadhifa za watu waliopo ndani ya gari

Mkuu ni wazi kabisa ujumbe wako umeuandika kishabiki. Ni lini ulishuhudia Mwanajeshi akipelekwa Mahakama za raia? au ni lini umemsikia au kumuona jaji yeyote au hakimu akienda MAHAKAMA ZA KIJESHI? So kubali kataa Jeshi hata raisi Lazima atumie BUSARA kutoa tamko kwa vyombo hivi coz 90% ya usalama wa raisi uko mikononi mwa JESHI (JWTZ)
 
Je ipo sheria yeyote inayompa askari Polisi, JKT, Magereza, JWTZ, na FFU furusa ya kupata huduma ya usafiri bure katika mabasi yanayofanya biashara katika nchi ya Tanzania? Tabia hii inakwaza wawekezaji wenye uwezo wa kuwekeza katika biashara ya usafirishaji, kama yupo mwenye ushahidi atusaidie tujue kiwango cha madhara ambayo Watanzania wanayapata na wataendelea kuyapata kwa ajili ya kundi la askari ambao kwa sasa ndio wanaolipwa vizuri kuliko watumishi wengine wa uma na bado wanataka huduma ya usafiri wa bure.Kama sheria haipo nini kifanyike sasa kukomesha tabia hii?.

hadi askari wa JKT asielipwa mshahara unataka alipe nauli?
 
Nina shaka na mtoa mada kama yeye ni Mtanzania,hata kiswahili chake kibovu kinathibitisha,mfano pale alipotumia "yeyote" badala ya "yoyote",Jeshi letu la Ulinzi JWTZ/TPDF ni wakarimu sana ukipenda nenda kambini kwao ukale supu ya nyama ya bure,hawa ndio wanaotufanya tulale kwa amani,usingizi mzito waacheni wapate hizo huduma,wewe ni mkenya?
 
Mkuu ni wazi kabisa ujumbe wako umeuandika kishabiki. Ni lini ulishuhudia Mwanajeshi akipelekwa Mahakama za raia? au ni lini umemsikia au kumuona jaji yeyote au hakimu akienda MAHAKAMA ZA KIJESHI? So kubali kataa Jeshi hata raisi Lazima atumie BUSARA kutoa tamko kwa vyombo hivi coz 90% ya usalama wa raisi uko mikononi mwa JESHI (JWTZ)

Kama wanawajali sana serikali iwape magari wasitusumbue au walipe nauli.mwishowe mtadai mchukue na vitu bure madukani kwa kisingizio cha kulinda amani.
 
Kama wanawajali sana serikali iwape magari wasitusumbue au walipe nauli.mwishowe mtadai mchukue na vitu bure madukani kwa kisingizio cha kulinda amani.

Acha Ushabiki Wew,lin Walikusumbua?Unajua Ni Mda Gan Wameanza Kutolipa Naul Mpaka Useme Watachukua Vitu Bure?Acha Ujinga Aman Yako Uliyonayo Shukuru Mungu Isikufanye Uanze Kubeza Chochote Kinachofanywa Na Hao Walinda Aman...We Ni #Mkapavoice
 
eti unaingia gari ya mkoa kwa kua una migwanda yako ukidaiwa nauli hulipi na kujibu jeuri, kuna 1 jana tulimkomalia akalipa nauli vingnevyo dereva asiondoe gari badae kwa aibu alipozidiwa na hoja alilipa nusu ya nauli akambiwa na konda kwa kua hakuonesha heshma nauli yake itakapoishia ndipo anashurhwa na dereva alifanya hvyo kweli

Labda alikuwa mgambo huyo
 



Chonde...mimi binafsi sina tatizo hata kidogo la wana uslama kutumia vyombo vya usafiri bure as long wanazo travel cards au kitu kama oyster cards za endapo watakuwa kwenye nguo za kiraia.

Kama kuna watu niko tayari kuwa wapendelewe basi ni wanajeshi kwani tutakapo hitaji huduma zao kama kujenga madaraja ya dharura wakati wa mafuriko huwa hawatuulizi pesa

So please spare wanajeshi wetu na nadhani mashambulizi yako ungeyapeleka kwa akina SALVA RWEYEMAMU kule ikulu ambako tangu aondoke Bush hawajatoa mchanganuao wa expenses walizozitumia

Mbona huulizi ile tenda ya Vitenge na Kanga alipewa nani?

Ktk nchi hii ni jeshi moja tu ambalo limesemewa tena na tena lipewe msamaha wa kulipa usafiri ktk maeneo ya kazi. Ni jeshi la Polisi. Hii ni kwa sababu Polisi wako kazimi saa zote wakiwa mitaani na wakati wowote wanaingilia matukio ya mitaani.

Hakuna sababu ya Jeshi la Ulinzi na Magereza kupanda vyombo vya usafiri na kukataa kulipa. Anakwenda wapi hadi asilipe? ofisini au kikosini kwake ndo asilipe! Hii siyo mara ya kwanza miaka ya 90 walishaambiwa walipe! Wapo askari wengi tu wenye uelewa ambao hawana tabia hiyo hata siku moja. wao hulipa wakiwa wamevaa kiraia kama kawaida. btw. afisa wa Jeshi la ulinzi haruhusiwi kupanda usafiri wa umma akiwa na mavazi ya kazi.

Upendeleo unaowaombea askari, vipi madaktari? Ebola ikija mbona tunawasukumia hatari yote? tusiwape umuhimu watu wachache kwa woga.
 
mi binafsi daladala yangu nlishamwambia dereva kuwa Jwtz&Jkt wapande bure!!! hata kama wakiwa watano!

Ukitaka Kujua kwanini; nenda congo,sudan au somalia!!

We mzembe tu! Biashara gani hiyo? Ukitaka kujua umuhimu wa kila mtu waulize Liberia wanavyowaheshimu madaktari kuliko wanajenshi. Ebola ingewamaliza bila madaktari!
 
Mleta mada sijuhi kama akili yako iko sawa. Askari yeyote kajitoa maisha yake kwa ajili yako hata mshahara anaolipwa hautoshi maana ni kama ameweka leani uzima wake ka ajili yako wewe
 
Sio kweli hata kidogo GT

Kwa sababu hawa wanajeshi sio kwamba wanatoa huduma za kujenga madaraja bure, no hawa wanalipwa kila mwezi bila kazi yoyote wanayofanya, na ndo maana zikitokea kazi za dhalula wanafanya, unaweza kuniambia wanafanya kazi gani specific hawa jamaa, wakati wanalipwa kila mwezi

Na kama ndo hivyo kila mtu atataka kusafiri bure, nani kama Mwalimu aliyewafundisha watu, kwanini hasisafiri bure?, na Madaktari je wanaokoa Maisha ya watu, mbona nao hawasafiri bure?
Hakuna mantiki katika hili kuwa askari wasafiri bure kwa sababu zipi?
Kwanza askari wa Tanzania wengi hawana nidhamu na maadili hata kwa wananchi wao, wengi wamekuwa wakiwapiga na kuwaonea wananchi, pili kuna makundi makubwa sana ya ujambazi ambayo na Maaskari wanashiriki.

Hivyo basi mimi sioni kama wao ni muhimu sana kuliko watu wengi mpaka waweze kusafiri bure

binafsi nimeona wanajeshi ni wenye nidhamu na msaada mkubwa ,miaka ya 90 mwanzoni kwa wale wanafunzi wa pugu sekondari mutakumbuka kambi ya gongo la mboto mwisho wa lami jinsi wanajeshi walivyotoa huduma ya maji safi bure kwa wanafunzi bila ubaguzi,hali kadhalika huduma ya afya lugalo nk
kwa kiwango cha kujitoa muhanga maisha mwanajeshi ni zaidi ya daktari,suala la nidhamu ni tabia ya mtu binafsi aliyolelewa tangu udogoni haihusiani na jeshi kwani wapi raia wengi ni watovu wa nidhamu
 
Unajua kuna vitu havihitaji Degree kuelewa,Ikulu haitowi taarifa ya mapato na Matumizi kwako wewe unayeandika na wala Usidhani kazi ya Jeshi ni kupigana vita wana kazi nyingi sana ni kwa sababu tu hawawajibiki kwako ndio maana unaweza kusema hawana kazi.
 
2acheni kubwabwanja while ha2jui hata SMG inashikajwe ama kweli amani ya nchi inatufanya tushindwe kujua ya kujadili but siku ukijaona askar anapigwa shaba anakufa na mwenzie anaendelea kupambana sabab ya nchi ndo utajua thaman ya uaskari haipaswi kulinganishwa na vijisenti vya daladala
 
Back
Top Bottom