Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 709
katika miaka ya tisini hadi 2000 kulikuwa na majarida mbalimbali yaliyokua yakituburudisha sana.Moja ya majarida hayo yalikua kama vile,BONGO,TABASAMU na SANI.Humo ndani kulikua na watunzi wazuri sana na wenye ubunifu wa hali ya juu sana,watunzi kama vile,DAUDI MASASI,FORTUNATUS NDILA(4T NDILA),na wengineo kibao.Hakika majarida haya yalikua yanatuburudisha sana na ilikua kila mwezi lazima upate kopi yako. Unakumbuka stori kama zifuatazao:- -Anga za wenyewe -Pablo Zungu -Bush Stars vs Born Town -Zena na Betina Kipepe na Mkasa wa masokwe unakumbuka watu wafuatao:- -Mapung'o -Njomba Nchumbari -Bob Mikwara Je wewe binafsi unazikumbuka stori hizo,watu hao na watunzi wake?hebu ongezea wengine bac na stori nyingine ili tukumbushane enzi.