a sinner saved by Christ
JF-Expert Member
- Feb 19, 2017
- 1,966
- 2,200
13
Yer 17:5 SUV
BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.
Mtumishi wa Mungu mmoja alianzisha huduma yake ya kiroho kanisa katika moja ya vijiji(Ukerewe)..eneo hilo lilikuwa na nguvu za giza kwa kiasi kikubwa na idadi kubwa ya washirikina.
Huduma yake ikafanikiwa kwa kiasi kikubwa alifanikiwa kuwafungua wengi waliofungwa na vifungo vy kishirikina uchawi..akapata waumini wengi sana kanisa likaendelea kukua kila siku na idadi ya waumini kuongezeka kila uchwao.
Washirikina wa eneo hilo wakapata pigo kubwa maana wanakijiji wengi waliponywa.
washirikina hao hawakufurahi wakaweka kikao wakamtengenezea UGONJWA wa kansa...wakamtupia ukampata..
Na Mungu aliruhusu hilo jaribu limpate kama ilivyokuwa kwa AYUBU wa kwenye biblia (Jaribu ni mtaji wa kuongeza imani)
Mungu hataruhusu jaribu lililo nje au juu ya uwezo wa mwanadamu,majaribu tinayopata ni yale ambayo ni ya kawaida kwa mwanadamu,na Mungu huwa anaweka na njia za kutokapo,mlango wa kutokea kwenye hilo jaribu..
Sasa mtumishi wa Mungu yule alipopata huo uginjwa wa KANSA alipokwenda hospitali madokta wakamwambia huu ugonjwa hauponi hauna tiba hospitali..
Mtumishi wa Mungu akahuzunika sana akakata tamaa ,akamkasirikia Mungu...akasema yani Mungu umeruhusu huu ugonjwa wa kansa unipate mimi mtumishi wako pamoja na kikutumikia kwa kiasi hiki chote..kujitoa kwangu kote ..kufanya kazi yako ina maana huioni ..ndio ukaamua ukubali nipate huu ugonjwa...akamchukia sana Mungu..
Katika wale wachawi mmoja wapo ni mtu wake wa karibu kanisani..
Akamfuata mtumishi akamshauri...kama hospitali wamwshindwa kukutibu..jaribu nikupeleke kwa MTAALAMU anaweza kukuponya kama huko kwingine wameshindwa ...
Mtumishi akamkasirikia Yesu akasema ..Kama wewe Yesu umeruhusu niumwe basi ..acha nijarubu kwingine..
Akaenda kwa mtaalamu sangoma mganga wa kienyeji..ambaye naye ni mshirikina ..ambaye alikuwa anamsubiri kwa hamu kwakua ..kanisa lake na maombi ya kanisa lake yalikuwa yanaleta uharibifu mkubwa katika kuathiri nguvu zao na mambo yao ya kishirikina ..alikuwa maombi ya walokole yanavuruga na kuharibu kabisa kazi zao za kishirikina..
Siku ya nne tu toka aende kwa mtaalamu mtumishi akafariki..
Mungu ni Mwaminifu: 1 Wakorintho 10:13 inasisitiza kuwa Mungu hataacha ujaribiwe kupita uwezo wako, bali atafanya mlango wa kutokea.
Yakobo 1:2-18
Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali, kwani mwajua kwamba imani yenu ikisha stahimili, itawapatieni uvumilivu. Muwe na hakika kwamba uvumilivu wenu utawategemeza mpaka mwisho, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote
1 Kor 10:13
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
Mwanzo 22:1-2 ”Ikawa baada ya mambo hayo MUNGU alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
Mathayo 24:13 ” Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”
Zaburi 11:5 ‘’BWANA humjaribu mweyehaki Bali nafsi yake humchukia asiye haki na mwenye udhalimu’’
Jaribu la MUNGU ni kipimo tu cha MUNGU kama kweli unampenda.
AYUBU ALIJARIBIWA AYUBU NI MFANO BORA WA MWANADAMU ALIYESTAHIMILI MAJARIBU NANKUSHINDA ...soma kitabu cha AYUBU katika biblia.
Yer 17:5 SUV
BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.
Mtumishi wa Mungu mmoja alianzisha huduma yake ya kiroho kanisa katika moja ya vijiji(Ukerewe)..eneo hilo lilikuwa na nguvu za giza kwa kiasi kikubwa na idadi kubwa ya washirikina.
Huduma yake ikafanikiwa kwa kiasi kikubwa alifanikiwa kuwafungua wengi waliofungwa na vifungo vy kishirikina uchawi..akapata waumini wengi sana kanisa likaendelea kukua kila siku na idadi ya waumini kuongezeka kila uchwao.
Washirikina wa eneo hilo wakapata pigo kubwa maana wanakijiji wengi waliponywa.
washirikina hao hawakufurahi wakaweka kikao wakamtengenezea UGONJWA wa kansa...wakamtupia ukampata..
Na Mungu aliruhusu hilo jaribu limpate kama ilivyokuwa kwa AYUBU wa kwenye biblia (Jaribu ni mtaji wa kuongeza imani)
Mungu hataruhusu jaribu lililo nje au juu ya uwezo wa mwanadamu,majaribu tinayopata ni yale ambayo ni ya kawaida kwa mwanadamu,na Mungu huwa anaweka na njia za kutokapo,mlango wa kutokea kwenye hilo jaribu..
Sasa mtumishi wa Mungu yule alipopata huo uginjwa wa KANSA alipokwenda hospitali madokta wakamwambia huu ugonjwa hauponi hauna tiba hospitali..
Mtumishi wa Mungu akahuzunika sana akakata tamaa ,akamkasirikia Mungu...akasema yani Mungu umeruhusu huu ugonjwa wa kansa unipate mimi mtumishi wako pamoja na kikutumikia kwa kiasi hiki chote..kujitoa kwangu kote ..kufanya kazi yako ina maana huioni ..ndio ukaamua ukubali nipate huu ugonjwa...akamchukia sana Mungu..
Katika wale wachawi mmoja wapo ni mtu wake wa karibu kanisani..
Akamfuata mtumishi akamshauri...kama hospitali wamwshindwa kukutibu..jaribu nikupeleke kwa MTAALAMU anaweza kukuponya kama huko kwingine wameshindwa ...
Mtumishi akamkasirikia Yesu akasema ..Kama wewe Yesu umeruhusu niumwe basi ..acha nijarubu kwingine..
Akaenda kwa mtaalamu sangoma mganga wa kienyeji..ambaye naye ni mshirikina ..ambaye alikuwa anamsubiri kwa hamu kwakua ..kanisa lake na maombi ya kanisa lake yalikuwa yanaleta uharibifu mkubwa katika kuathiri nguvu zao na mambo yao ya kishirikina ..alikuwa maombi ya walokole yanavuruga na kuharibu kabisa kazi zao za kishirikina..
Siku ya nne tu toka aende kwa mtaalamu mtumishi akafariki..
Mungu ni Mwaminifu: 1 Wakorintho 10:13 inasisitiza kuwa Mungu hataacha ujaribiwe kupita uwezo wako, bali atafanya mlango wa kutokea.
Yakobo 1:2-18
Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali, kwani mwajua kwamba imani yenu ikisha stahimili, itawapatieni uvumilivu. Muwe na hakika kwamba uvumilivu wenu utawategemeza mpaka mwisho, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote
1 Kor 10:13
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
Mwanzo 22:1-2 ”Ikawa baada ya mambo hayo MUNGU alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
Mathayo 24:13 ” Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”
Zaburi 11:5 ‘’BWANA humjaribu mweyehaki Bali nafsi yake humchukia asiye haki na mwenye udhalimu’’
Jaribu la MUNGU ni kipimo tu cha MUNGU kama kweli unampenda.
AYUBU ALIJARIBIWA AYUBU NI MFANO BORA WA MWANADAMU ALIYESTAHIMILI MAJARIBU NANKUSHINDA ...soma kitabu cha AYUBU katika biblia.