Wakatoliki mjiandae majaribu yataendelea sana

Wakatoliki mjiandae majaribu yataendelea sana

Life2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,387
Reaction score
4,880
Ndugu Wakristo Tumsifu Yesu Kristo.

Poleni sana kwa imani yenu kuguswa na kujaribiwa, kumbukeni hata Bwana Yesu alijaribiwa mno na Shetani na mwishowe akashinda.

Hata hawa mashetani wanaoibuka dhidi ya dini yenu Karne hizi watashindwa tena vibaya sana.Giza hajiwahi kushinda mwanga hata siku moja.

Wanachosema maaskofu/mapadre wa kikatoliki na ukweli 100% mbele za Mungu wametenda haki ila kwa wanadamu ukweli wao umekua ni chukizo kubwa sana.

Kama ni majaribu 50 hili ndo kwanza jaribu la 3, shetani na jeshi lake naye amejipanga sana, endelee kusali na kumlilia Mungu wa Haki ushindi utakua kwa watenda haki.

Siku zijazo watatumwa mawakala wengine wa shetani kwenda kwenye media na kuwachafua viongozi wenu kwa propaganda za ukweli hilo nalo litapita.

Mtakatifu mmoja alipata kusema kila kwenye Padri mmoja kuna mashetani 1000, kwa hiyo Padri mmoja kazungukwa na mashetani 1000 tuwaombee sana.

Utawala umeamua kupambana na ukweli, utawala huu umeamua kupambana na Haki, Utawala huu umeamua kupambana na kanisa la Mungu.

HAWATAWEZA.
 
Sahihi kabisa. Hata Mapadre, Maaskofu na Watawa wetu wanatakiwa kuishi kwa tahadhari na umakini mkubwa sana awamu hii. Hii vita dhidi ya wahuni, siyo vita nyepesi hata kidogo. Watatumia kila aina ya mbinu, ili tu kulichafua Kanisa la Mungu.
 
Majaribu yataendelea lakini kamwe hayatafikia yale yaliyotendwa dhidi ya Yesu Kristo, nafsi ya Mungu, aliyeruhusu kutendewa ili kutuonesha majaribu tunayoweza kupitia. Hata yaje ya namna gani, kamwe hayatafikia yale yaliyotendwa dhidi ya mitume wale na mashahidi watakatifu wa Mungu wa kale. Na pamoja na majaribu ya kutisha, lakini kanisa liliendelea kustawi na kusambaa Duniani kote. Ushindi kwa watu wa Mungu na Kanisa lao ni lazima kwani wapo chini ya mshindi mkuu, mshindi wa mauti, yaani Bwana wetu Yesu Kristo, aliyepewa mamlaka yote Duniani na Mbinguni.
 
Majaribu yataendelea lakini kamwe hayatafikia yale yaliyotendwa dhidi ya Yesu Kristo, nafsi ya Mungu, aliruhusu kutendewa ili kutuonesha majaribu tunayoweza kupitia. Hata yaje ya namna gani, kamwe hayatafikia yale yaliyotendwa dhidi ya miyume wale na mashahidi watakatifu wa Mungu wa kale. Na pamoja na majaribu ya kutisha, lakini kanisa liliendelea kustawi na kusambaa Duniani kote. Ushindi kwa watu wa Mungu na Kanisa lao ni lazima kwani wapo chini ya mshindi mkuu, mshindi wa mauti, yaani Bwana wetu Yesu Kristo, aliyepewa mamlaka yote Duniani na Mbinguni.
hizo dini za kikoloni hazina nafasi
 
Na sisi tutalazimika kumwandikia barua Trump kumweleza jinsi ambavyo Wakristo Tanzania tunanyanyaswa! Tunaandamwa na serikali,makanisa yanafungwa na kuzuiwa kufanya ibada!
 
Sahihi kabisa. Hata Mapadre, Maaskofu na Watawa wetu wanatakiwa kuishi kwa tahadhari na umakini mkubwa sana awamu hii. Hii vita dhidi ya wahuni, siyo vita nyepesi hata kidogo. Watatumia kila aina ya mbinu, ili tu kulichafua Kanisa la Mungu.
Ila wahuni wajue unyakuo upo,ila lini na wakati upi ni kitendawili!
 
Back
Top Bottom