Maiti afufuka chumba cha maiti - Iringa

Soma habari yote kabla ya kutoa comment. Madaktari walithibitisha kuwa ameshakufana na kuruhusu kwamba maiti apelekwe mortuary kama ifuatavyo hapa chini:

kama unavyoeleza hapa ndio unataka ieleweke hivyo basi inabidi uipange upya habari yako
 
Inavyoonyesha reporter wa hii habari hajaelewa makosa yake. Anaeleza kwamba wakiwa kwenye foleni mgonjwa aliomba kwenda chooni na ghafla akakata kauli na wakaamua kumpeleka motuary, inaonyesha hata daktari hapo hawajamuona na wakati wakimpeleka motuary aliamka na kuanza kujipigapiga ''nafikiri kwa maoni yangu hapo ndo alikua anakufa'' wakaamua kumpeleka kwa Dk ambaye alithibitisha kifo chake. Habari ilivyokaa inaonekana baada ya hapo akaitwa ''marehemu'' na yule mama akawa ''mjane''. Sasa huko kufufuka kuko wapi? Mtoa taarifa hajui kupanga maelezo yake.
 
Hizi ni hallucination, mwandishi wa habari hajaonyesha kama kuna Dr aliyethibitisha kuwa kafa na wala hakumhoji Dr huyo. Huu ni udhaifu wa waandishi wa habari na hii mada tulishawahi kuijadili tunaomba muwe mnaelimika. Kwa hiyo habari haijakamilika, na wala hajasema mgonjwa alikaa mochwari kwa muda gani. Mod habari kama hizi ninaomba ziwe zinatolewa coz watu wanatafuta umaarufu kupitia JF. Nawasilisha
 
:eyebrows:Inavyoonyesha reporter wa hii habari hajaelewa makosa yake. Anaeleza kwamba wakiwa kwenye foleni mgonjwa aliomba kwenda chooni na ghafla akakata kauli na wakaamua kumpeleka motuary, inaonyesha hata daktari hapo hawajamuona na wakati wakimpeleka motuary aliamka na kuanza kujipigapiga ''nafikiri kwa maoni yangu hapo ndo alikua anakufa'' wakaamua kumpeleka kwa Dk ambaye alithibitisha kifo chake. Habari ilivyokaa inaonekana baada ya hapo akaitwa ''marehemu'' na yule mama akawa ''mjane''. Sasa huko kufufuka kuko wapi? Mtoa taarifa hajui kupanga maelezo yake.
 
Nina wasiwasi na taaluma ya hao madaktari huenda walifoji vyeti...
 
Wakati ndugu yangu alipofariki recently how l wished muujiza kama huo ungetokea! Yaani hata siku ya pili tunavalisha Nguo ready kwa safari kuelekea kwetu bado nilikuwa nawish pamoja na kwamba mwili wake ulikuwa na baridi ya kutoka kwenye jokofu!

Mungu ampe miaka zaidi huyo mkaka; ni relief kubwa kwa familia! Haijalishi ni muujiza au alikuwa kwenye coma kikubwa ni mzima sasa!

Zamani nilijiuliza kwa nini mtu anaweza kufeli swali doooogo la kitoto ktk mtihani. Jibu ni kwamba, hasikilizi maelekezo kwa makini. Sasa wewe nani kakwambia kwamba yupo hai mpk umuombee maisha marefu? Hebu soma tena, A to Z.
 
Mauaza uza yaibuka mjini Iringa baada ya mgonjwa ambaye alifika kufanyiwa maombi kwa mmoja kati ya wahubiri maarufu mkoani Iringa kukata kauli yake akiwa nje ya ukumbi huo maarufu wa maombi mjini hapa na baada ya kufikishwa chumba cha kuhifadhiwa maiti (Mochwari) katika hospital ya mkoa wa Iringa maiti hiyo iliamuka na kupelekea ndugu kuupeleka mwili huo kwa madaktari kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
..Hata hivyo alisema kuwa akiwa katika foleni ya kuingia ndani ya ukumbi ghafla mgonjwa huyo aliomba kupelekwa chooni na kabla ya kuingia chooni alikata kauli na hivyo kulazimika kuupeleka mwili wake mochwari katika hospital ya mkoa ambako kabla ya kuingizwa Mochwari ghafla marehemu aliamuka na kuanza kurusha rusha mikono yake hali iliyopelekea kurudishwa tena mapokezi kwa ajili ya kuchunguzwa zaidi na kumtaja mjane wa marehemu Bi Amina Ramadhan alimtaja marehemu kuwa ni Gerald Tadei Ngusi
Kukata kauli ni sawa na kufa? Kuna kitu katika stori yako kina miss....mwili umetolewa eneo la ukumbi (alipokatia kauli!) na kupelekwa mochwari moja kwa moja bila kupitia kwa daktari? Kama ni hivyo hayo ndio yalikuwa mauzauza!
 
Katavi, si taaluma ya Madaktari. Taaluma ya huyu aliyeleta taalifa. Madaktari walivyopelekewa wamefanya kazi yao vizuri na kugundua amekufa na ndio maana anaitwa marehemu. Huyu reporter hajaeleweka. Soma vizuri taarifa yake.
 
Hii sisi tunaita kuzirai hakufa. ila kwa uelewa wa mwandishi ni kwamba alikufa. Si kitu cha ajabu wazee kuna jamaa aliwahi kupimwa VVU Agkhan hospital ni naikwakathibitisha kwamba jamaa ni mwathirika. Lakini jamaa hakuamini matokeo kwa sababu mchumba wake waliekuwa wafunge nae ndoa alipimwa akakutwa mzima wakati jamaa alikuwa anabanjua amri ya sita matra kibao pekupeku. Jamaa alienda kupima sehemu nyingine 3 tofauti akakutwa ni safi hajaathirika. Kwa ufupi ni kwamba inawezekana dr alijichanganya au vipimo vilimzenguo akona jamaa kafa kumbe kazimia tu. Sio cha ajabu hapa.
Ijumaa njema.
 
Stori iko sawa soma ile paragraph ya mwisho
iko kama ifuatavyo: Red

Tukio hili limetokea majira ya saa 10 za jioni katika ukumbi huo wa IDYDC mjini Iringa na hadi mtandao huu wa Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima unatoka hospital hapo majira ya saa 11 .20 jioni madaktari walikwisha mpima na kuthibitisha kifo cha mgonjwa huyo.


Maiti haipokelewi mortuary mpaka dr a_certify! Stori haijatulia hii
 
Back
Top Bottom