Asante sana sanaHakuna kitu mbaya kinacho maliza pesa kama kununua vitu vidogo vidogo bila mpangilio,pipi, pombe, vyakula pasi na njaa, kumsaidia tu yoyote bila sababu za msingi, kununua tu viatu ilihali una pea za viatu vingine kama kumi na ni viatu vigumu tu, akili kubeba maoni yasiyo na tija, wewe ni mmoja kati ya wale wanaoamini kujenga ni mpaka uwe na Milion 100.
Jifunze kuweka akiba, tumia pesa ktk mahitaji ya msingi pekee na achana na mambo yasiyo na tija, rejea nyumbani mala tu utokapo kazini ili usiingie kwenye tamaa za Dunia ukiwa mitaani, mtengeneze mke awe mwenye uchungu na familia na maendeleo, akiweza utaona matumizi ya ndani ya elfu 50 per week, badala ya matumizi ya laki mbili per week... Tengeneza miezi yako ya kununua kimoja baada ya kingine, toka nje ya mji tafuta kiwanja nafuu nunua na anza ujenzi taratibu bila kuathili watoto wako swala la chakula na shule, pia hapo kwenye shule, usipeleke watoto kwenye shule ambazo zinakupa umasikini kwa sababu tu unataka watu wakuone umepeleka watoto shule za kulipia pesa nyingi,zenye raha ilihali watoto watakuja kuishi Afrika yenye majeraha yasiyo angalia mtoto alikula mkate shule na kubebwa na Coaster asbh na jioni, naweza kuendelea lakini naamini kwa uchache utakua umejua namaanisha nini.
N.B - mawazo yako yabebe kufanikiwa kimaisha, kutengeneza pesa na vyote unavyo vitaka maishani, utaona vinakuja kimoja kimoja maana utaweka bidii, achana na mambo ya Simba na Yanga huo ni upuuzi mkubwa unaokula muda wa waTanzania wengi mitaani
Namba 8 ni tatizo , hebu toa zaka ya 130000 Kwa Mungu alaf uone kama utakua unaliaHabari.
Nina miaka 37. Sifurahii maisha katika umri huu. Kama kuna mtu anaweza kutoa ushauri wa kunikomboa asisite, Mshana Jr n.k. Mtiririko wa matukio ni kama ufuatavyo;
1. Ninafanya kazi serikalini mshahara take home ni 1.3 m., hapo nina mkopo wa miaka 5 NMB.
2. Kazi nimeanza tangu 2012, hivyo nina miaka 9+ kazini.
3. Naishi Dar es Salaam.
4. Nina mke na watoto wanne, mtoto wa nne bado ni kichanga.
5. Tangu nianze kazi sijui pesa zangu zinapoenda, sina kiwanja, sina akiba, bado nimepanga, kodi laki tatu kwa mwezi.
6. Mahusiano yangu na mke siyo mazuri sana kwa sababu ya ugumu wa maisha, lakini bado tunasonga.
7. Mke hana kazi, hana biashara.
8. Nakunywa pombe mara kwa mara.
9. Siendi kanisani kabisa ila kwa matukio maalum mfano ndoa, ubatizo wa mtoto, n.k.
10. Sina gari, niliyoanza nao kazi wana nyumba kubwa na magari mawili, moja la mke.
Nahisi nina mkosi, nifanye nini? Yapo mengi kuonesha hasara ninayoihisi. Kazini napata marupurupu ya hapa na pale, ila najiona sitoboi. Wadogo zangu wenye mshahara wa laki tano wametoboa mi nipo nipo tu mpaka mama yangu amekata tamaa. Faraja yangu iliyobaki ni binti zangu ambao hawaelewi chochote kwenye hii Dunia ya vita.
Duh!hapo niko bar..Safi sana. Itabidi niwe napiga vitu home maana mbili tatu zikiwa kichwani nakuaga na roho ya kitajiri....kutoa hata kiti moto kwa mhudumu ni dakika sifuri
Nini maana ya uzazi wa mpango?Mkosi ni akili yako tu kaka.
Fanya mambo kadhaa muhimu:
1.Kaa na mkeo na mpange budget ya matumizi ya fedha mnayopata…kwenye mshahara wako jitahidi uwe unaweka 10% kama dharura na 5% iwe budget yako ya gambe na matumizi yako binafsi (jipende).
2.Tenga kiasi cha akiba kila mwezi kwa ajili ya kufungua kitega uchumi kingine; anza na wife mwambia anaweza kujishughulisha na nini. Weka malengo ya akiba kiasi gani ya kuweka na kwa muda gani mpaka wife awe na bishara.
3.Wakati unaweka akiba kwa ajili ya biashara ya wife, fanya utafiti wa kina kuhusu hiyo biashara kumbuka kuwa tuna fedha kichele hivyo ni vyema tusiipoteze kwa kutokuwa na uelewa na tunachokifanya.
3.Punguza matumizi yasiyo ya lazima; birtdhay za kifahari, michango isiyo ya lazima, pombe n.k punguza.
4.Wakumbuke wazazi na kuwatunza: Baraka zao zitakufungua sana hutaamini.
5.Usijilinganishe na wengine. Kujilinganisha kutakufanya ukate tamaa na kuona umechelewa.
6.Jitahidi utumie uzazi wa mpango, watoto uliobarikiwa wanatosha.
7.Hakikisha familia nzima mna bima ya afya, gharama za matibabu huwa zinarudisha watu nyuma sana.
Kila la Kheri
1.3 million mshahara mdogo?Kazi gani hiyo unalipwa ujira Mdogo hivyo ?
Tafuta Kazi ya maana au Biashara kubwa Stress zinasababishwa Na low income earning
AhahahaSafi sana. Itabidi niwe napiga vitu home maana mbili tatu zikiwa kichwani nakuaga na roho ya kitajiri....kutoa hata kiti moto kwa mhudumu ni dakika sifuri
Hapo kwenye hela ya Loan Board ndo tatizo lilipoanzia.Huo mkopo ndo vituko kabisa sitaki hata kukumbuka. Nilikopa 36m. Hapo Hela ya LOAN BOARD ikakatwa. Nikabakiwa na 20. Ukiniuliza nilichofanya sijui... Iliisha kiutani utani
Loan Board huwa wanakata hela zote kwa mara moja?Nahisi ni chai unatudanganya
Unachangamsha kijiwe..
Huo mshahara si mbaya, ukijipanga unatoka tu. Maximize muda wako kwenye maendeleo.Habari.
Nina miaka 37. Sifurahii maisha katika umri huu. Kama kuna mtu anaweza kutoa ushauri wa kunikomboa asisite, Mshana Jr n.k. Mtiririko wa matukio ni kama ufuatavyo;
1. Ninafanya kazi serikalini mshahara take home ni 1.3 m., hapo nina mkopo wa miaka 5 NMB.
2. Kazi nimeanza tangu 2012, hivyo nina miaka 9+ kazini.
3. Naishi Dar es Salaam.
4. Nina mke na watoto wanne, mtoto wa nne bado ni kichanga.
5. Tangu nianze kazi sijui pesa zangu zinapoenda, sina kiwanja, sina akiba, bado nimepanga, kodi laki tatu kwa mwezi.
6. Mahusiano yangu na mke siyo mazuri sana kwa sababu ya ugumu wa maisha, lakini bado tunasonga.
7. Mke hana kazi, hana biashara.
8. Nakunywa pombe mara kwa mara.
9. Siendi kanisani kabisa ila kwa matukio maalum mfano ndoa, ubatizo wa mtoto, n.k.
10. Sina gari, niliyoanza nao kazi wana nyumba kubwa na magari mawili, moja la mke.
Nahisi nina mkosi, nifanye nini? Yapo mengi kuonesha hasara ninayoihisi. Kazini napata marupurupu ya hapa na pale, ila najiona sitoboi. Wadogo zangu wenye mshahara wa laki tano wametoboa mi nipo nipo tu mpaka mama yangu amekata tamaa. Faraja yangu iliyobaki ni binti zangu ambao hawaelewi chochote kwenye hii Dunia ya vita.
Kipato cha milioni 1 na laki 3 sio kidogo kwa maisha ya Kitanzania..
Zaidi ya 80 % wa raia .. hawafikii hicho kipato
Tafuta Kazi ya maana hiyo hela hutoboi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119] kwakweli wewe ni changamoto kwenye jamiiHuo mkopo ndo vituko kabisa sitaki hata kukumbuka. Nilikopa 36m. Hapo Hela ya LOAN BOARD ikakatwa. Nikabakiwa na 20. Ukiniuliza nilichofanya sijui... Iliisha kiutani utani
Take home ya 1.3m ingawa siyo nyingi, lakini si haba. zaidi ya nusu ya waTZ hulipwa chini ya 0.5m. Nafikiri hapa uwe na mpangilio mkubwa wa saving. Weka lengo la kuweka angalao laki 3 ukitegemea kuzitumia kuzalisha baada ya miaka. Ukitunza laki 3, miaka miwili utakuwa 7.2m, angalia ni biashara gani mkeo anaweza kufanya na 7.2m.Kazi gani hiyo unalipwa ujira Mdogo hivyo?
Tafuta Kazi ya maana au Biashara kubwa Stress zinasababishwa Na low income earning
Nitafungua kioksi soon...kama ulikopa mil 20 ukazinyea bia unategemea nini? mchawi ni wewe mwenyewe kwanza una watoto wengi, usawa huu watoto wanne na umri wako 37 duh, umetisha. Pole sana komaa tu usife maana hicho kibarua na chenyewe kikiisha tu unaokota makopo hata wiki haifiki. mkeo mtafutie hata kimtaji cha kuuza hata maji tu na maandazi anaweza akakuokoa kwenye msongo maana kula ndio kunaleta stress kwenye majamaa yenye watoto wengi kama wewe. POLE sana.