Maisha yanachanganya sana

Kaka ww umeyawezaje maisha ya mtaani🤔
 
Huko kisemvule Kuna viwanda vya kutengeneza bidhaa gani na bidhaa gani hasa [emoji1666][emoji1666]
 
Ninachokiongea sio kitu cha kutunga na hizi ndio baadhi ya vitu anavyomiliki brother
Hiki ulichokifanya sio kizuri...Kama Kuna uwezekano wa kufuta futa.sio sawa kuanika Mali za Kaka yako mtandaoni ni hatari halafu hapa jf watu wengi so wanaweza kuona huu Uzi na hii picha wakampa taarifa bro..utaonekana limbukeni
 
Inasikitisha sana, labda anakupima uvumilivu wako, akili na upambanaji wakati anakuandalia kitu kikubwa cha kukutoa coz naamini damu nzito kuliko maji.
Sijui lakini sina imani na hicho unachokisema maana mara nyingi amezoea kusema kwamba pesa zake katafuta mwenyewe na hiyo kauli huwa anamwambia sana mama pale anapomsihi awasaidie sisi ndugu zake
 
Sawa kaka nimekuelewa
 
Hiki ulichokifanya sio kizuri...Kama Kuna uwezekano wa kufuta futa.sio sawa kuanika Mali za Kaka yako mtandaoni ni hatari halafu hapa jf watu wengi so wanaweza kuona huu Uzi na hii picha wakampa taarifa bro..utaonekana limbukeni
Nimeshafuta mkuu
 
Nipo fizikali fiti kaka na malipo yao huwa yapoje
Kwa wastani ni elfu kumi kwa siku (maana kuna vitengo mbalimbali), siku moja nenda ukajiridhishe (kwa kuuliza kazi zilizopo na malipo yake) kwanza kisha ndo uchukue maamuzi ya kuanza hicho kibarua
 
Nakazia hapa naufahamu mziki wake hahahaha kibeba viroba kutoka kwenye mkanda wa mashine s mchezo bado matusi ya wakongwe pale
Kuna jamaa angu wa karibu alikwenda pale alinipa habari za pale na namna alivyokua (alianza kuumwa mwili hasa mgongo na mabega), nilighairi kujiunga nae pale kiwandani baada ya kuona naweza kukata moto hivi hivi, maana yeye alikua baunsa 6 pack flani afu mi one pack[emoji23]
 
Asee, Familia zetu za kiswahili roho mbaya zinaanzia hata kwa walokusomesha, mzazi ana uwezo ila ni bandidu hatariii, sijui anadhan akinisaidia nitampita!
Inasikitisha sana kaka na ndio maana familia zetu hizi kukuwa kiuchumi inakuwa ngumu sana
 
Kwa wastani ni elfu kumi kwa siku (maana kuna vitengo mbalimbali), siku moja nenda ukajiridhishe (kwa kuuliza kazi zilizopo na malipo yake) kwanza kisha ndo uchukue maamuzi ya kuanza hicho kibarua
Ahsante kaka kwa kunipa mwanga kesho nitaenda huko
 
Kaka mbona unanivunja moyo aisee maana mimi sina six pack hata moja yani ni half pack sasa sijui hizo kazi ntaziweza kweli
 
Kaka mbona unanivunja moyo aisee maana mimi sina six pack hata moja yani ni half pack sasa sijui hizo kazi ntaziweza kweli
Hapana mkuu sina lengo la kukuvunja moyo ila nilikua namdadavulia huyo jamaa kitaswira zaidi. Unaweza kua one pack au half ila ukazimudu hizo kazi maana kinachotumika ni nguvu zaidi na si unajua kila mwanadamu ana nguvu tofauti na mwenzie, jitahidi hiyo kesho uliosema utaenda ukajiridhishe. Pia kumbuka nilisema vitengo vinatofautiana hivyo utakuta kuna vitengo vina unafuu na utumiaji wa nguvu so sana kama vitengo vingine.
 
Mkumbushe huyo ^nduguyo^ ajfunze kuweka nukta kila baada ya sentensi moja kamili. Au ndivyo anakufundisha kujichanganya mjini, maana nawe ushamwiga tayari?
 
Kila la kheri, ngoja waje kukupa miongozo...
 
Matatizo mengi ya ajira katika nchi yetu yanasababishwa na vijana kung'ang'ania dar badala ya mambo kuyaendea kombo kuna jamaa mmoja alipata kazi serikalini akapangiwa shinyanga akasema mi kijana siwezi kuishi porini huko wanaishi wazee kipindi hicho anafanya kazi private sector mkataba private umeisha kaja boss mpya hajamuongezea sasa hivi anataka kazi yoyote na mke na watoto.

Tusing'ang'anie dar maana mpaka tukija kushtuka mda umeenda na tumeshachelewa.
 
Ahsante mkuu ntaenda kujiridhisha
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…