Melancholic
JF-Expert Member
- Oct 12, 2018
- 3,545
- 6,499
Daaah!! Maisha yanachanganya sana.
Nipo Dar takriban miez 6 sasa nililetwa na ndugu yangu toka mkoani kwa ajili ya mchongo fulani ila kwa bahati mbaya mambo hayakwenda kama tulivyopanga nikawa nimefeli.
Ndugu yangu sio kinyonge ni mtu mwenye maisha yake safi tu sio tajiri ila ana magari kama matatu hv na taasisi yake inayojishughulisha na masuala ya elimu.
Sasa Baada ya ule mchongo kufeli ndugu yangu huyo jana akaniweka chini akaniambia, "Mdogo wangu nishakuleta mjini tayari na mji ushaujua sasa usikae tu home inabidi ujichanganye hata mimi nilianzia maisha duni sana nililala nje lakini leo mambo yangu yamenyooka hivyo na wewe anza kujitafuta mapema, kuhusu kulala nitakusimamia mimi ila vitu vingine inabidi ujitafutie mwenyewe ili akili yako ikae sawa na pia uanze kujitegemea mapema maana ushakuwa mtu mzima, Sifanyi hivi ili nikutese hapana nafanya hivi ili nikusaidie na usiwe tegemezi.
Nikamwambia sawa kaka nimekuelewa wazo lako nitalifanyia kazi.
Sasa ndugu zangu hili suala nimelileta kwenu mnisaidie idea, mawazo yoyote ni vipi nitaweza kusurvive hapa mjini, hata kama kuna viwanda vinavyotoa kazi za kulipwa kwa siku mnielekeze vinapatikana wapi. Maana mimi bado sijawa mwenyeji sana hapa jijini. Kiufupi ni kwamba sichagui kazi yoyote ili mradi tu nisiwe nimevunja sheria za nchi.
Naombeni mawazo yenu ndugu zangu kiukweli napitia nyakati ngumu sana, sijui nianzie wapi kutafuta hata pesa yakula natanguliza shukrani na karibuni kwa mawazo yenu.
Nipo Dar takriban miez 6 sasa nililetwa na ndugu yangu toka mkoani kwa ajili ya mchongo fulani ila kwa bahati mbaya mambo hayakwenda kama tulivyopanga nikawa nimefeli.
Ndugu yangu sio kinyonge ni mtu mwenye maisha yake safi tu sio tajiri ila ana magari kama matatu hv na taasisi yake inayojishughulisha na masuala ya elimu.
Sasa Baada ya ule mchongo kufeli ndugu yangu huyo jana akaniweka chini akaniambia, "Mdogo wangu nishakuleta mjini tayari na mji ushaujua sasa usikae tu home inabidi ujichanganye hata mimi nilianzia maisha duni sana nililala nje lakini leo mambo yangu yamenyooka hivyo na wewe anza kujitafuta mapema, kuhusu kulala nitakusimamia mimi ila vitu vingine inabidi ujitafutie mwenyewe ili akili yako ikae sawa na pia uanze kujitegemea mapema maana ushakuwa mtu mzima, Sifanyi hivi ili nikutese hapana nafanya hivi ili nikusaidie na usiwe tegemezi.
Nikamwambia sawa kaka nimekuelewa wazo lako nitalifanyia kazi.
Sasa ndugu zangu hili suala nimelileta kwenu mnisaidie idea, mawazo yoyote ni vipi nitaweza kusurvive hapa mjini, hata kama kuna viwanda vinavyotoa kazi za kulipwa kwa siku mnielekeze vinapatikana wapi. Maana mimi bado sijawa mwenyeji sana hapa jijini. Kiufupi ni kwamba sichagui kazi yoyote ili mradi tu nisiwe nimevunja sheria za nchi.
Naombeni mawazo yenu ndugu zangu kiukweli napitia nyakati ngumu sana, sijui nianzie wapi kutafuta hata pesa yakula natanguliza shukrani na karibuni kwa mawazo yenu.

