Na wasiwasi wewe ni atheistZinaweza
Kweli kabisa. Mara nyingi tunahukumu jambo kwa tunachokiona leo, kumbe Mungu anaiona kesho yake. Wakati mwingine tunachokiona kama “mshangao” leo, kesho kinakuwa baraka kubwa. Tusihukumu haraka, muda utaeleza kila kitu.Nikiwa kijana mkubwa wa secondary,kama unavyojua kuna kipindi kinafika unaona kabisa hapa wazazi inabidi wasiendelee kuzaa sasa,kwanza kutokana na umri wao lakini pili ile kuona inakuwaje bimkubwa na umri huu anabeba mimba
Ilikuwa inanipa shida kidogo,lakini sikujua kwamba Mwenyezi Mungu anasababu kubwa sana ya kumleta yule dogo akiwa kama last born pale nyumbani
Miaka kadhaa baadae, huku ukubwani dogo huyo ndio kawa nguzo ya familia kwa kiasi kikubwa sana,yeye ndio kajaliwa uchumi mzuri sana na anaisadia familia kwa kiasi kikubwa sana
Hakika kuna mambo Mwenyezi Mungu pekee ndio anajua,nimejifunza kitu kimoja kikubwa kwamba,kila kitu hutokea kwa sababu
Kwahiyo si kazi yako kujaji mambo ambayo huwa yanatokea hapa duniani just wait and see,utashangazwa na hekima ya Mwenyezi Mungu.
Silent king
Issue sio alichokifanya yule Babu bali alivyofanikiwa kwa alichokifanya coz uzi unaongelea surprise za kwenye maisha kimafanikio.Ule ni utapeli na ujinga wa watu,naweza sema hivyo kwa maoni yangu
Hizo ni siasa tu za watu walioshindwa kupambana na maisha yaoHuwezi kusema ni makusudio ya Mungu kuwafanya wawe wakorofi na kusumbua wazazi
Lakini hatuwezi kuweka kila kitu kwenye kapu moja,hapa nazungumzia uwezo wa Mungu kuinua baadhi ya familia kupitia viumbe wake au kupitia wanafamilia wengine
Hapa naona kuna mambo mawili au matatuKama mungu ndio anawajibika kuinua watu kwa ajili ya kutumikia familia zao basi pia ndiye anawajibika kwa wale watu waliokuwa mizigo na mateso kwenye hizo familia. Mfano rahisi ni kama vile kiongozi akijenga barabara anasifiwa na asipojenga anapaswa kulaumiwa na kuwajibishwa.
Village in,Hakuna kitu kama hicho. HIYO INATOKEA NI KWA TANZANIA TU. MTU UNAJITUMA SANA KTK KAZI ZAKO IWE KILIMO AU BIASHARA ZAKO. LAKINI UNACHOAMBULIA NI HAMNA KITU UKILINGANISHA NA NGUVU ULIYOTUMIA. HAYO NDIO MATOKEO YA SIASA MBOVU ZA CCM.
Mfano unafanya biashara kwa kutumia mtaji wako. Lakini zinakuja kodi nyingi, makusanyo ya TRA hata kabla ya kupata faida inatakiwa ulipe. Hawajali utapata faida au la. Hawana muda wa kuwekeza kwenye kukufundisha kupata faida. Wanawekeza kwenye kukusanya tu bila kujali faida umepata au una hasara.
Ukija kwenye kilimo unaweza kulima lakini soko lake ni la chini kabisa,kwa hiyo nguvu uliyotumia ni bure kabisa.
Kazini fikiria waalimu wana kazi ngumu sana kuliko wabunge. Linganisha mishahara na malupulupu yao. Mwalimu ni kama yupo yupo tu,mshahara wake hata hautoshi kuishi mpaka mwisho wa mwezi. Ili-hali wabunge wanaogelea kwenye mamilioni kwa kazi bure kabisa.
Lakini nenda nchi zingine nguvu utakayotumia kujitafuta ndio malipo yake yatalingana na nguvu uliyowekeza humo.
Siasa za CCM ndizo zimetufikisha hapa
Nimekupata chief, ni kweli kabisa kwasababu kuna wengine walijaribu lakini hawakupata vibe kama yule mzeeIssue sio alichokifanya yule Babu bali alivyofanikiwa kwa alichokifanya coz uzi unaongelea surprise za kwenye maisha kimafanikio.
Yani kama tungefahamu haya unayosema na kuyazingatia tungebarikiwa sanaKweli kabisa. Mara nyingi tunahukumu jambo kwa tunachokiona leo, kumbe Mungu anaiona kesho yake. Wakati mwingine tunachokiona kama “mshangao” leo, kesho kinakuwa baraka kubwa. Tusihukumu haraka, muda utaeleza kila kitu.
Kabisa. Mara nyingi tunatamani baraka zaidi huku tunasahau kushukuru tulichonacho tayari. Shukrani huleta utulivu, na kulalamika kunaweza kutufanya tusione thamani ya tulichopewa. Ni ujumbe mzito sana huo.Yani kama tungefahamu haya unayosema na kuyazingatia tungebarikiwa sana
Tunaambiwa tusikufuru bali tushukuru tutazidishiwa,lakini tunaharibu baraka zetu kwa kulalamika na kukufuru
Mafanikio binafsi yanatokana zaidi na bahati inayohusisha genetics, familia uliyozaliwa, mahali ulipozaliwa, connections, black swan events n.k Mfano mmojawapo ni wanozaliwa uswahilini kwenye familia masikini inavyokuwa vigumu sana kwao kufanikiwa na wanaishia kuwa waendesha bodaboda kuliko wanaozaliwa familia Bora/za kishua wanaoishi Mbweni, Msasani n.kNapenda kutofautiana na wewe kidogo, unaposema kufuata details au taratibu au formula ya mafanikio
Sio kwamba watu hawazifuati,ila naamini mafanikio sio kupambana tu,kwasababu kuna watu wanapambana sana lakini mafaniko yao sio makubwa
Naamini rikizi ni kutoka kwa aliyetuumba,tunazo fanya ni sababau tu
Maisha yetu yanategemea bahati nasibu zaidi kwa asilimia 70%(umezaliwa wapi, wazazi wa aina gani, wakati gani, matukio, afya, umbo, rangi n.k)Hapa tuna mawazo pishani
Maisha yetu yanategemea ridhaa ya Mwenye Enzi Mungu
Hakuna mwenye uhakika wa nini kitakachomkuta sekunde inayofuata ya maisha yake
Tuendelee kumuomba Mwenye Enzi Mungu atupe ridhiki, afya njema na mwisho mwema
Stop using riziki kama excuse ya kufeli kwa mifumo ya watu. Kila mtu anapambana, lakini swali la msingi ni are they solving the right problems?Napenda kutofautiana na wewe kidogo, unaposema kufuata details au taratibu au formula ya mafanikio
Sio kwamba watu hawazifuati,ila naamini mafanikio sio kupambana tu,kwasababu kuna watu wanapambana sana lakini mafaniko yao sio makubwa
Naamini rikizi ni kutoka kwa aliyetuumba,tunazo fanya ni sababau tu
Ngoja tukubaliane kutokukubaliana,itakuwa imekaa poa sanaStop using riziki kama excuse ya kufeli kwa mifumo ya watu. Kila mtu anapambana, lakini swali la msingi ni are they solving the right problems?
Muumba alituwekea akili ili tugundue codes za maisha, ukizikosa hizo utakwama tu hata upige goti vipi.