Huku kijijini na mimi maisha yananishinda.
Nataka niuze mahindi nije mjini, mjini kuna nyumba nzuri na magari. Nasikia magari madogo ila yanakimbia hayo. Yakikua makubwa ndio yanazidi kukimbia. Nikiyaona nitahamasika kutafuta vyangu.
Huku kijijini tunacheza na ngedere tu.
duuh, halafu kumbe huu uzi ni wa 2011 mtu alikua anachukua zaidi ya nusu milioni alikua analalamika??? nilifikiri hata ni mwaka huuHuyu jamaa amenishangaza sana, yani mshahara was 524,000Tsh/ bado analalama plus 300,000 ya wife kwa mwez uhakika was 824,000/Tsh. Hapa hesabu inahitajika kwanza matumizi ya home per day yapunguze kutoka 8000 mpaka 5000-6000
Pili nauli pamoja na msosi wa mchana mkiwa kazin wewe na mke wako punguza kutoka 10000 mpaka 6000 kwa mahesabu ya haraka kwa mwez uta save 210,000 kwa mwaka 2.5M pia jaribu kupunguza matumiz mengne na kugundua maeneo/masoko ya kununulia vitu bei nafuu hasa vyakula. Mwisho usiwe mvivu wa kufikiri
mkuu nilikua sijacheki vizuri, kumbe ilikua ni 2011, eti 542,000, 2011 unalalamika!? hahaaaAachane nayo afanye jambo lingine sio [emoji1] [emoji1]
We rudi tu kijijini...sisi hata tushindie mihogo...hata yaje mafuriko haturudi kijijini ng'oWakuu Maisha ya Mjini yamenishinda, yaani nikiangalia kipato changu na majukumu niliyonayo naona siwezi kabisa.
Maisha kama haya naona afadhali yale maisha niliishi kwa wazazi wangu enzi za mwalimu pamoja na kuwa babangu alikuwa mkulima lakini tulienda shule na tuliishi maisha mazuri.
Mimi sijui wenzangu mnaishije? mnapata haya machungu nayoyaona mimi? nasimama asubuhi kituoni kwenda kazini naona magari yanapita tu huku mmefunga vioo hivi kweli mna matatizo kama yangu kweli? Hivi nyie pesa mnazipata wapi? mbona najiona mpweke katika nchi yangu hii?
Wakuu siyo siri natafakari kama mambo yakizidi kuwa magumu basi nitafute nauli nirudi kwetu angalau huko nitakuwa na uhakika wa kusogeza siku.
Kipato changu wakuu ni Tshs 542,000/- Nina Mke na mtoto mmoja (5), nimepanga nyumba viwili na sebure - Mambo yamegoma kabisa.
Nipeni ushauri nateketea mtanzania mwenzenu.