Maisha yamenichapa haswa

Kama hauna aibu kama mimi au sio bishoo. Uza simu hiyo ingia sokoni asubuhi ununue tenga la nyanya utembeze na baiskeli hapo mjini daslam lazima utapata hata 5000 ya kula kila siku.

Regret haitakutatulia matatizo. Tushapitia hizo shida na sisi. Nilianza kuuza simu ili nipate hela ya kula, nikanunua kitochi. Hela ilivyokata nikauza jiko la gesi. Ahahahhahaaa

Jamani maisha magumu yasikieni kwa watu tu mkihadithiwa... maana unaishi kwa stress hatari, ukiwa na buku kumi mfukoni unaogopa hata kuichenchi maana unakuwa unawaza ikiisha sijui ndo utakufa...

Ila itabidi upambane mkuu hamna namna, ukishindwa kabisa rudi kijijini ukaanza moja kabisa, maana haina maana upo mjini halafu unaishi maisha ya digidigi... ikiwa ngumu sana usifosi, rudi kijijini hata ukalime.
 
Sio rahisi kihivyo hasa kwa mtu ambae Hana uzoefu na biashara, ninachomshauri ajiripue tu aondoe aibu afamye anachoweza kufanya atatoboa kwa uwezo wa Allah
 
Wewe ni tapeli
 
Pole sana hauko peke yako ndugu yangu unajua nini cha kufanya............Fungia vyeti vyote ulivyokua navyo halafu ingia mtaani ki ukali, usichague kazi, hakikisha unatumia kidogo kuliko unachokipata nitafute baada ya miezi 6 ni matumaini utakuja kunishukuru ndugu pole sana uchaguzi ni wako!!!!!
 
Yatapita tu, usikate tamaa
 

NAKAZIA
 
Siku zote kwenye maisha, wekeza hela kwenye mali ambayo hata ukiyumba itakusaidia wewe ila usiwekeze kwa wanawake na marafiki.
Mwanamke akikuomba 50,000 mpe 10,000 nyingine bora ununue pazia mlangoni maana hutokea pazia likawa linathamani sana kuliko mpenzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…