Nimerejea Bukoba kwa likizo baada ya miaka kadhaa, na kwa masikitiko makubwa nilikumbana na hali iliyonishtua sana. Nilimkuta msanii nguli wa muziki wa asili, Saida Karoli aliyewahi kutoa nyimbo zilizopata umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi, hadi kuvuka mipaka ya Tanzania akiishi maisha ya dhiki yasiyoendana kabisa na hadhi na mchango wake mkubwa katika sanaa na utamaduni wa taifa.
Kwa sasa, Saida Karoli anaishi katika nyumba ya kupanga ya vyumba viwili, katika mazingira yasiyofurahisha, hali ambayo haistahili hata kidogo kwa msanii aliyewahi kuiwakilisha nchi yetu kimataifa kwa heshima kubwa. Hali hii inanifanya nijiulize maswali mazito kuhusu mfumo wetu wa kulinda wasanii, hasa wale waliotoa mchango mkubwa kabla ya enzi ya mifumo ya sasa ya kidijitali.
Kwa wajuzi wa masuala ya commercial entertainment, je, hakuna njia ya kusaidia wasanii kama Saida Karoli kufaidika na royalties za kazi zao walizofanya miaka ya nyuma? Je, sheria na taasisi zetu za hakimiliki zinawafikia kwa vitendo, au zipo tu kwenye maandishi?
Zaidi ya hapo, tukio hili linapaswa kuwa funzo kwa wasanii wanaong’ara kwa sasa. Umaarufu ni wa muda, lakini maisha ni ya kudumu. Ni muhimu kwa wasanii wa kizazi cha sasa kupambania sera imara za kulinda kazi zao, kudai haki zao za kisheria, kusaini mikataba yenye kuwanufaisha hadi baadaye
Kwa kweli, hali niliyoikuta imenihuzunisha sana.
Kwa sasa, Saida Karoli anaishi katika nyumba ya kupanga ya vyumba viwili, katika mazingira yasiyofurahisha, hali ambayo haistahili hata kidogo kwa msanii aliyewahi kuiwakilisha nchi yetu kimataifa kwa heshima kubwa. Hali hii inanifanya nijiulize maswali mazito kuhusu mfumo wetu wa kulinda wasanii, hasa wale waliotoa mchango mkubwa kabla ya enzi ya mifumo ya sasa ya kidijitali.
Kwa wajuzi wa masuala ya commercial entertainment, je, hakuna njia ya kusaidia wasanii kama Saida Karoli kufaidika na royalties za kazi zao walizofanya miaka ya nyuma? Je, sheria na taasisi zetu za hakimiliki zinawafikia kwa vitendo, au zipo tu kwenye maandishi?
Zaidi ya hapo, tukio hili linapaswa kuwa funzo kwa wasanii wanaong’ara kwa sasa. Umaarufu ni wa muda, lakini maisha ni ya kudumu. Ni muhimu kwa wasanii wa kizazi cha sasa kupambania sera imara za kulinda kazi zao, kudai haki zao za kisheria, kusaini mikataba yenye kuwanufaisha hadi baadaye
Kwa kweli, hali niliyoikuta imenihuzunisha sana.