Maisha ya sasa Mwanaume na Mwanamke ni maadui wakubwa, tusitegemee tena ndoa kudumu

Mr Why

JF-Expert Member
Nov 27, 2019
1,118
1,915
Maisha ya sasa mwanaume na mwanamke ni maadui wakubwa sana tusitegemee tena mahusiano ya kimapenzi au ndoa kudumu.

Uhalisia ni kuwa maisha ya sasa yamejaa uadui mkubwa sana kati ya mwanamke na mwanaume ndio maana mahusiano hayastawi tena. Wapenzi wataanza mahusiano lakini baada ya muda mchache watatengana kwasababu tofauti lakini sababu zote zitakazotelewa na hao wapenzi kiini chake ni uadui ulioko katika ulimwengu wa sasa kati ya mwanaume na mwanamke.

Mwanamke hana tena upendo kwa mpenzi wake anamuona mpenzi wake kama gonjwa hali kadhalika kwa wanaume.

Hakuna tena uaminifu kati ya mwanamme na mwanamke matokeo yake ni ubaya kwa ubaya tangu mwanzo wa mahusiano mpaka kuvunjika.

Wanawake wa sasa katika maongezi yao yote yamelenga kumzungumzia mwanaume kama kiumbe mbaya duniani hali kadhalika kwa wanaume ndivyo hivyo.

Sababu ya ongezeko la mapenzi ya jinsia moja kama tunavyowaona watu mfano mama wa Jay Z, ni watu kujaribu kujua je mapenzi ya jinsia moja pengine yana unafuu kuliko haya ya jinsia tofauti?

Hii ndiyo sababu kubwa ya ongezeko la mapenzi ya jinsia moja ingawa athari zake ni kubwa zaidi kwasababu hakuna uzao kati yao.

Mahusiano kati ya mwanamke na mwanaume yatakuwa mazuri endapo jinsia zote mbili zitajirekebisha na tabia mbaya ikiwemo usaliti ambazo zinasababisha utengano wa wapenzi kila kuchwao.

Upendo umepotea kabisa kati ya Mwanaume na Mwanamke madhara yake ni kuwa mahusiano ama ndoa hazitadumu tena.
 
Mimi na mke wangu tulianza kua marafiki, na mabaya yangu pamoja na upuuzi wangu wote aliujua kabla hatujafunga ndoa.

Leo tunaendeleza urafiki wetu na tunaishi kwa furaha iliojaa amani tele, pamoja na kwamba kuna wakati tunatofautiana lakini tunakaa chini na kuzungumza kisha maisha yanaendelea.
 
Kuna rafiki yangu flani mdada ni msagaji, yaani yeye ni dem na anadem wake. Aiseeee wale watu wanapitia changamoto nyingi sana za magomvi, wivu uliopitiliza na hata imefikia yule rafikiyangu hawezi tena hata kufanya kazi ama biashara sababu dem wake hataki kumuona kabisa na dem mwingine hata wakiongea (kwamba anamla) na hataki kumuona na mwanaume hata wakisalimiana kwamba (analiwa).....😂 yaani hawa watu wanamaisha magumu sana kwakweli....🤣

Kwahiyo watu msiamini kwamba mapenzi ya jinsia moja ndio yanaamani, bakini njia kuu then itengenezeni furaha na amani kama tulivyo fanya mimi na mai waifu...😊
 
Back
Top Bottom