Hornet
JF-Expert Member
- Apr 29, 2013
- 26,155
- 49,654
Fohadi hakuna buree kilichopo ni utofauti wa garama... dar kila matumizi ya hela yapo juu sana kutofautisha na mkoani
usafiri: dar mtu anaweza kupanda daladala 2 kwenda sehemu ya kazi ambapo anaweza tumia mpka 3000 kila siku, mkoani akuna habari za kuunga route au usafiri watabu so unaeza tumia ata nudu ya iyo 3000 kwa siku
makazi; dar kupangisha ka chumba kamoja kibachela kwa mwezi ni 60 hadi 80 kama kisela sana utapata vyumba vya 40, lakini mkoani utapanga hata kwa 30 au 25 hapo unasevu unaona ukiwa mkoani unasevu nusu pesa ya dar
chakula; hapa ndo raha ya mkoa, ulaji wa mema ya nchi inategemea upo mkoa gani, kama mbeya utajaza viazi ndani vya kula ata wiki 2 kwa shil elfu 5 ambazo kwa dar ungeimaliza kwa siku moja
ukiishi dar kama una mishe za kuunga unga utaishia kuwa msaka tonge tu, lakin ufanyi maendeleo hata siku 1, dar kama unakipato kidogo alafu hauna heshima na pesa hela itakua auioni, yani unapata unaitumia unapata uinaitumia. excuses za kutumia hela nyingi
mkoani ukisema mwaka hauishi nataka niwe na 20 millions. unaweza kufanya ivyo
Kuhusu vyakula jitahidi uhudhurie masokoni maisha ni simple tu