Maisha ya dada zetu wakiwa vyuoni

Maisha ya dada zetu wakiwa vyuoni

kaka George huyo alikudanganya vingine vilikuwa vya kwake, sema aliogopa tu,

teh teh teh teh

Rom

hamna hicho kitu wewe, ningemchinja ala.
btw, kipindi hicho mi nilikua nimeshamaliza na nina kazi so nilikua namhudumia mie mwenyewe!.
 
Kwa kweli hawa dada zetu wamezidi pale Tumaini Iringa kuna waarabu wanawacharaza hawa wadada kinyume na maadili.
Mbaya zaidi kuna tetesi kuwa ni waadhirika!!!!!!!!!!
Akina dada muache tamaa mtaishia pabaya,lizika na ulichonacho.
Kwa upande wangu I have played my part niliwai kuwaonya watatu hawakunisikia yaliyowasibu kwa sasa Mungu anajua.
 
Wanapractice mafiga ma3 ya kipwanipwani....mmoja wa kusoma naye asiliwe kichwa....mmoja atm(mara nyingi wana umri kama baba zao)....mmoja handsomeboy(presentable wa kutoka naye)
hizi siyo hadithi...ni real. nimeona kwa macho.....watu ambao mna wachumba vyuoni jitahidini kuwa nao karibu though siwafundishi kuwa na wivu kupindukia...


Suali la msingi kwa nini mchumba wako akishaingia na kujiunga chuo mostly mnaachana kwa sababu za ajabu ajabu tu.

Kwa hiyo ndungu yangu we acha tu.

Kuna jama alikuwa anamchumba wake hall three pale.jama akamununulia jiko la mchina(stove) ili liwe linamsidia kujipikilisha badala ya kwenda cafeteria.
Siku moja akaja kumwona mchumba wake akakuta jiko lake linamkaangia mayai jamaa mwingine huku amekaa kitandani!! aise jama alichukiwa na kuchukuwa jiko lake na kuweka kwenye mfuko wa rambo!! aisee usiombe yakukute.

Truee story sio joke.

Kwa hiyo sisi Woman( ni kweli tunakutana na vitamanisho vingi lakini tujitahidi kuwa firm na mahusiano ya awali otherwise tutakuwa tunawalaumu wanaume bila kufikiria nani chanzo cha ajali.
 
Suali la msingi kwa nini mchumba wako akishaingia na kujiunga chuo mostly mnaachana kwa sababu za ajabu ajabu tu.

Hii namhurumia jamaa angu mmoja kitaa anamchumba ake tayari taratibu za msingi zisha fuatwa na anaingia chuo mwaka huu mtoto kasimama balaa akimwona Yo Yo lazima ulokole umtoke. Dah anaweza kumpoteza hivi hivi sijui jamaa apige mimba kabisa ili mtoto atulie?
 
Hii namhurumia jamaa angu mmoja kitaa anamchumba ake tayari taratibu za msingi zisha fuatwa na anaingia chuo mwaka huu mtoto kasimama balaa akimwona Yo Yo lazima ulokole umtoke. Dah anaweza kumpoteza hivi hivi sijui jamaa apige mimba kabisa ili mtoto atulie?

yaani kama anlijuwa hilo bora aweke alama yake kabisa mapema la sivyo anaweza kinyonga au kuua kama yule mkurya alivyomuua mpenzi wake waliyekuwa na mahusiano toka form four ila baada ya kufika chuo na kukutana na jamaa wa TRA na Rav4 yake akaanza kumsema jama yake kuwa ni mlevi wa kupindukia.Wanawake bwana yaani tunoma.

Kwa toka mwanzo hakumwona kama ni mlevi mpaka amusema chuoni?

Ale kitu tena kwa saana tu kwa kuwa hata ukiwa na mimba unaweza endelea soma.
 
Hii namhurumia jamaa angu mmoja kitaa anamchumba ake tayari taratibu za msingi zisha fuatwa na anaingia chuo mwaka huu mtoto kasimama balaa akimwona Yo Yo lazima ulokole umtoke. Dah anaweza kumpoteza hivi hivi sijui jamaa apige mimba kabisa ili mtoto atulie?

hivi Yo Yo ni mlokole??
 
yaani kama anlijuwa hilo bora aweke alama yake kabisa mapema la sivyo anaweza kinyonga au kuua kama yule mkurya alivyomuua mpenzi wake waliyekuwa na mahusiano toka form four ila baada ya kufika chuo na kukutana na jamaa wa TRA na Rav4 yake akaanza kumsema jama yake kuwa ni mlevi wa kupindukia.Wanawake bwana yaani tunoma.

Kwa toka mwanzo hakumwona kama ni mlevi mpaka amusema chuoni?

Ale kitu tena kwa saana tu kwa kuwa hata ukiwa na mimba unaweza endelea soma.

Unajua wanawake mnabadilika mapema mno bora ya mwanaume anaweza akabadilika lakini mkawa mnaendelea na uhusiano kama kawa. Yaani unakuta mtu mmetoka wote mbali lakini akimpata mtu mwenye fedha basi anakuona huna thamani tena anachukuliwa na mwenye fedha na huyo mwenye fedha anamchezea tu hana future nae yoyote tu jamaa ana kata kiu basi anamwachia maugonjwa manini kila kitu.
 
yaani kama anlijuwa hilo bora aweke alama yake kabisa mapema la sivyo anaweza kinyonga au kuua kama yule mkurya alivyomuua mpenzi wake waliyekuwa na mahusiano toka form four ila baada ya kufika chuo na kukutana na jamaa wa TRA na Rav4 yake akaanza kumsema jama yake kuwa ni mlevi wa kupindukia.Wanawake bwana yaani tunoma.

Kwa toka mwanzo hakumwona kama ni mlevi mpaka amusema chuoni

kweli JF ni jamvi kuu lisiloisha ukoko!, bila JF ningejuaje haya?
kumbe hii ndio sababu?, ama kweli ukistaajabu ya musa atayaona ya firauni, hapo kweli mkurya wacha hasira zimpande.
 
"mahitaji yetu ni mengi"

Mimi siamini kama akina dada wana mahitaji mengi kuliko akina kaka. We sema ni tamaa tu ndio zinazowapelekea kujihusisha na ngono mavuoni. Baadhi ya wasichana wanatoka vijijini wakiwa na tabia nzuri, mavazi ya heshima akikanyaga chuo tu anaanza kubadilika na kusahau alikotoka. Msichana kama unasoma nyoa nywele, na kua na mavazi ya kawaida sana. Lakini visista du vinapenda kujinakshi na uwezo hawana. Kitu kikubwa ni kusoma kwa bidii ili ukimaliza chuo ubate kazi nzuri.

Pia iko ile dhana kua mwanamke hawezi mpaka awezeshwe na mwanaume hiyo hupelekea kwaasilimia kubwa pia baadhi ya wanawake kudesa na kuhitaji support ya kiuchumi kutoka kwa mwanaume. Sasa jiulize boom ni lile lile kwa wote iweje wanawake muhitaji vya ziada? Kuchuna hela kupo, ila kuchuna UKIMWI pia kupo
 
Yeah amemrudia Mungu baada ya kufanya madhambi mengi ameona amdondokee Mungu maana siku za mwisho zinakaribia.

aisee kumbe!, au ndio maana huku haonekani sana, pengine atakua kule kwenye mambo ya dini.
hongera sana mkuu Yo Yo!.
 
ni Ushamba tu kuona Ukifika Chuo ndio umeibuka kimaisha...!!!...

Uhuru nao unachangia kwa kiasi Kikubwa MNO...!!! Vijana wa Kiume waliokuwa Boys tupu wakifika Vyuo Moto chini....na Mabinti waliokuwa Girls nao usiseme....Watu wa Geti kali nao mmhhh....!!!

I still believe kuwa Asasi za KIDINI bado zinajukumu la kuwafundisha Vijana Roles zao wanapokuwa vyuoni...!!!

Chuma, naunga mkono hoja yako. Ni kweli uhuru unachangia sana. Mabinti wengi wakiwa sekondari huwa hawapati nafasi ya kufanya ngono kutokana na kubanwa na wazazi au walezi wao lakini wakishatinga vyuoni ni 'full kujiachia'! Na kwa wale waliotoka girls' schools ni mbaya zaidi. Kwa upande wa wavulana pia hali ni hiyo hiyo.
 
aisee kumbe!, au ndio maana huku haonekani sana, pengine atakua kule kwenye mambo ya dini.
hongera sana mkuu Yo Yo!.

Yeah yupo busy na maombi mkuu teh teh teh lakini kumbuka anamshawishi hata Nyani Ngabu nae awe kundini sijui kama ataweza kweli.
 
Suali la msingi kwa nini mchumba wako akishaingia na kujiunga chuo mostly mnaachana kwa sababu za ajabu ajabu tu.

Kwa hiyo ndungu yangu we acha tu.

Kuna jama alikuwa anamchumba wake hall three pale.jama akamununulia jiko la mchina(stove) ili liwe linamsidia kujipikilisha badala ya kwenda cafeteria.
Siku moja akaja kumwona mchumba wake akakuta jiko lake linamkaangia mayai jamaa mwingine huku amekaa kitandani!! aise jama alichukiwa na kuchukuwa jiko lake na kuweka kwenye mfuko wa rambo!! aisee usiombe yakukute.

Truee story sio joke.

Kwa hiyo sisi Woman( ni kweli tunakutana na vitamanisho vingi lakini tujitahidi kuwa firm na mahusiano ya awali otherwise tutakuwa tunawalaumu wanaume bila kufikiria nani chanzo cha ajali.

......... Tena likiwa bado la moto masikini
 
ishu hapa sio kuwa huru!, ishu ni tabia mbaya ambazo hujitokeza mara baada ya kuwa huru. mfano utakuta mwanafunzi anakua na mahusiano na mume wa mtu bila woga hata kidogo, sasa hapo utasema ni uhuru?.
 
ukiwa na demu mwanafunzi wa chuo halafu wewe mwenyewe unavijisenti vya mboga tu yataka moyo mgumu kama plastiki!!!!, otherwise utapata bp bure.
jaribu siku moja kwenda mabibo hostel weekend mida ya jioni pale car parking, balaaaaaaa! utaona gari linatikisika tikisika tu.
siku hizi sema wamebadilisha utaratibu gari za visitors mwisho saa 12 jioni.
 
naomba nitofautiane kidogo na wadau wengine waliochangia hapa nyuma.Ni kwamba nyie mnafanya kitu Inaitwa Hasty Generalization mnaposema hao dada zetu wa vyuo kama vile wote ni matatizo matupu.Sasa basi kuna vitu vichache vyafaa kuangaliwa kwa undani kabla hatujatupa lawama.

1.Exposure-Lawama kwa wazazi: Unakua na wanao wakike hata kuwatoa na kuwapeleka movie (kwa wale wenye uwezo) au kuwaonesha kuwa hivi vitu si vitu vya ajabu hufanyi.Akitokea brazameni wa mfano wa Yo Yo nakumpeleka theatre mtoto anachanganyikiwa. Wito:Wazazi jaribuni kuwapa watoto exposure.

2.Peer Pressure-Lawama kwa marafiki:Msichana katoka Seminari ya Visitation huko moshi (huu ni mfano) anakuja Daslam na kukaa chumba kimoja na Chausiku mtoto wa Aza-Jangwa mabaye bilicanas alikua akienda kwa kutembea na mguu anaanza kumfundisha jinsi ya kuvaa kipedo na kuvaa bra inayoshika maziwa vizuri na kwenda pedicure etc basi mtoto anaona maisha ndo hayo: Hapa namkumbuka yule aliyeingia mlimani baaada ya kupata alama za A tatu high school lakini akadisko mwaka wa kwanza-Mgongochuma wa kitivo cha sheria si mchezo!!

3:Boom-Lawama kwa "Ya" Kaisari- Umetoka boarding school pocket money elfu ishirini kwa term hela unaweka kwa mwalimu au dukani,unaingia chuoni hamadi!! unakuta laki saba kwenye akaunti.Ukitoka kwenye ATM badala ya msichana kupanda daladala atachkua teksi n akuanzia hapo mpaka atakapoishiwa ni kujirusha daily.......Sasa anapoishiwa wale mamaaluni wa kumendea vitoto vya watu ndio wanamuibukia na kuanza kumpa vijihela na kwa kutaka kumaintain status mtoto wa watu lazima aingie 'kingi'

Sasa hayo hapo juu na mengine yafananayo na hayo ndiyo inayowatia dada setu ukichaa.
 
Habari wakuu kwa kweli nakwera sana na tabia ya dada zetu hasa hawa wa vyuoni .kwa miaka minne niliyo kaa mlimani hili jambo limenisumbua sana maana tulipokuwa tunaanza chuo (ntatumia udsm as my reference) wadada wengi walikuwa wastaarabu wanajiheshimu sana. Lakini baada ya kukaa ka semister na kupata kabumu kuanza kutumia vimemake up tu shida inaanza mabadiliko ya ghafla.

Na kunatabia kubwa wanayo dada zetu ya kurubunika kirahisi kwa tamaa za muda mfupi na kupenda makubwa huu umambo sasa(the mordenazation) kwa dada zetu unawaharibu. nina ushahidi kwa hili wasichana wengi pale chuoni wana hii tabia kwangu naona ni chafu sana ya mafiga matatu/Mwanaume zaidi ya mmoja (bwana wa madesa (kisovio)/mtu wakumsaidia kwenye masomo,beedeshe kwa ajili ya pesa ya matumizi akiishiwa bumu na handsome boy kwa ajili ya mitoko na show up za kizembe) kwa kweli dada zetu wanapokuwa vyuoni they are too material ,realistic hakuna wanasahau ulimwengu hauko hivyo.

Kuna maswali ningeomba dada zangu niwaulize hivi:
as intelectual ya kupasa ufanye huu ujinga?
Hivi ukimaliza chuo cant you earn money na wewe uwe na gari lako au ndo mwanamke ameumba kwa utegemezi sawa ,but haki sawa maanake nini?
Huu umambo sasa ni halali tucopy na kupaste kila kitu ?
DADA ZANGU JIHESHIMUNI NYIE NDO MAMA WATOTO ZETU MIAKA MICHACHE IJAYO TAIFA LETU LITAKUWA LA NAMNA GANI JAMANI !!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom