Maisha: Ukikukatana marafiki wa "high class" usikimbilie kuomba hela, kutangaza shida zako ama kuwalaumu pindi mnakutana

mambo ya kuombana hela hakuna anayeyataka siku hizi... mimi mwenyewe sina hela hapa ila nakufa na roho yangu tu
Wenye Pesa, ndio hao hao ukiwatajia shida wanakutema

FB_IMG_15259489250757807.jpg
 
Shikamooni wakibwa zangu wa hapa JF......

Hii issue niliwahi kuambiwaga na mama yangu nikiwa mdogo sana ya kwamba watu wengi wa hali ya juu kiuchumi huanza kuwakwepa wale wenye uwezo wa chini kwa maana hawa wenye uwezo wa chini wakikutana na hawa wenye pesa cha kwanza kukimbilia ni kuwaomba hela, kutangaza shida walizonazo pamoja na kuwalaumu mbona siku hizi hawawatembelei kama zamani. Aliniambia ukitaka marafiki wa high class, kwepa sana kuwalaumu na kuomba omba pesa. Keep your problems in your heart. Sio umeenda kwenye msiba umekutana na mjomba anafanya kazi UN baada ya salamu ushaanza kutiririka shida zako. Mtachokwa.

Jamani mbona kuna mambo mengi sana yanayohusu maisha, siasa za ndani na nje ya nchi mnaweza kuzungumza pamoja na masuala ya kijamii badala ya kukimbilia kutangaza shida na kuomba hela?

Kama kuna jambo linaloweza kumjengea heshima mtu wa kipato cha chini kisha akapendwa na kupata marafiki wale wa high class basi ni kujiwekea mipaka ya mazungumzo na kujua ni kipi cha kuongea na kipi si cha kuongea mbele ya watu wa namna fulani. Hiyo inajenga sana heshima and they won't feel bored around you.

KIJANA KUWA MZALENDO. IPENDE TANZANIA. USITUMIKE KUICHAFUA NCHI YAKO.
Kama Yule mwanaume baada ya kumwona mkuu Na kuanza kulia Lia ety hana nauli.
Pale angemsifia kuwa mchapa kazi.na kuanza kuchomekea Hali HALISI.
Nadhan mkuu Ange guswa Na kupata zaidi ya pesa ya nauli.
 
Naunga mkono hoja yako, lakini umezungumza mambo ya mtu binafsi mwisho umemalizia kitaifa. Uzi wako mzuri hayo mambo ya uzalendo na kuipenda nchi yako hayahusiani na ulichoandika.

Nakubaliana na wewe kuficha shida zako ni kuficha thamani yako. Binadamu yoyote ana thamani kubwa awe tajiri au masikini. Hapa unaizungumza subra, Mwenyezi Mungu katika quran ameitaja sana subra unapokuwa na haraka unakosa mengi.
 
Labda kitu ambacho sikipendi ni lawama tu lakini kuombwa napenda sana, kama ninacho nitakupa hata kama siyo ndugu yangu. Siyo vizuri kumtenga mtu kwa sababu ya shida zake. Kutoa ni jambo jema sana, hata Mungu anapenda. Kama hutaki kumsaidia basi kaa na mali zako na uchoyo wako lakini siyo kumchukia mtu kisa kakuomba jamani!!!
 
Labda kitu ambacho sikipendi ni lawama tu lakini kuombwa napenda sana, kama ninacho nitakupa hata kama siyo ndugu yangu. Siyo vizuri kumtenga mtu kwa sababu ya shida zake. Kutoa ni jambo jema sana, hata Mungu anapenda. Kama hutaki kumsaidia basi kaa na mali zako na uchoyo wako lakini siyo kumchukia mtu kisa kakuomba jamani!!!

Kuna wengine hawataki kujishughulisha kutwa kupiga vizinga kwa nini usikimbiwe.
 
Back
Top Bottom