Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,349
Habari za leo wandugu,
Dunia hii kuna wengine hawajawahi kabisa kuishi katika nyumba za kupanga, wengine maisha ya uswazi hawayajui kabisa, basi leo nimeona tuangalie maisha katika nyumba za kupanga. Ukweli ni kuwa maisha katika nyumba za kupanga si mabaya, ni wewe mwenyewe utakavyoiweka akili yako.
Unaweza kujifunza mapishi katika nyumba za kupanga, kwani kupika wote mnapika pamoja, kama ulitoka kwenu hujui kipika chapatti, utakutana na wapangaji wenzako ambao tena wanapika chapatti za biashara, na utajifunza kukanda unga hapo. Si chapatti tu, ni mapishi mengi.
Ukitaka kuishi vizuri kwenye nyumba za kupanga usiwe mbea na mfuatiliaji wa mambo ya watu pia usipende kuanika ya kwako. Ukikuta unaongelewa wewe dharau tu, kama hujaanika sana yako watakayo kuwa wanaongea watakuwa wanahisi.
Rafiki zangu wa kiume kama watatu hivi waliniambia bikra zao zilitolewa na wapangaji wengine wakati wakiwa wadogo kwenye nyumba za kupanga, mimama isiyokuwa na haya anamsubiri mama wa kijana ametoka, ndipo kijana anapoitwa chumbani, huko anakuta ameandaliwa chai na vitafunwa na akapewa mchezo. Kama vile wale wa ushuani wanaposema bikra zimetolewa kwa ma housegirl huku kwetu kwa Mtogole kuna mengi pia yanaendelea.
Dhumuni la waraka huu ni kufahamishana dunia inavyoendelea katika nyumba hizi, kuna mengi yanayoendelea ambayo wazazi hawayafahamu. Fikiria kama hili li mama linalomuitia kijana wako chai lina magonjwa, mpaka uje uhfahamu mtoto ameathirika kabla hajafikisha miaka 20.
Siku njema.
Dunia hii kuna wengine hawajawahi kabisa kuishi katika nyumba za kupanga, wengine maisha ya uswazi hawayajui kabisa, basi leo nimeona tuangalie maisha katika nyumba za kupanga. Ukweli ni kuwa maisha katika nyumba za kupanga si mabaya, ni wewe mwenyewe utakavyoiweka akili yako.
Unaweza kujifunza mapishi katika nyumba za kupanga, kwani kupika wote mnapika pamoja, kama ulitoka kwenu hujui kipika chapatti, utakutana na wapangaji wenzako ambao tena wanapika chapatti za biashara, na utajifunza kukanda unga hapo. Si chapatti tu, ni mapishi mengi.
Ukitaka kuishi vizuri kwenye nyumba za kupanga usiwe mbea na mfuatiliaji wa mambo ya watu pia usipende kuanika ya kwako. Ukikuta unaongelewa wewe dharau tu, kama hujaanika sana yako watakayo kuwa wanaongea watakuwa wanahisi.
Rafiki zangu wa kiume kama watatu hivi waliniambia bikra zao zilitolewa na wapangaji wengine wakati wakiwa wadogo kwenye nyumba za kupanga, mimama isiyokuwa na haya anamsubiri mama wa kijana ametoka, ndipo kijana anapoitwa chumbani, huko anakuta ameandaliwa chai na vitafunwa na akapewa mchezo. Kama vile wale wa ushuani wanaposema bikra zimetolewa kwa ma housegirl huku kwetu kwa Mtogole kuna mengi pia yanaendelea.
Dhumuni la waraka huu ni kufahamishana dunia inavyoendelea katika nyumba hizi, kuna mengi yanayoendelea ambayo wazazi hawayafahamu. Fikiria kama hili li mama linalomuitia kijana wako chai lina magonjwa, mpaka uje uhfahamu mtoto ameathirika kabla hajafikisha miaka 20.
Siku njema.