Maisha haya acheni tu unaweza kukufuru

Maisha haya acheni tu unaweza kukufuru

Marry Diana

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2025
Posts
970
Reaction score
2,360
Habari za jioni

Maisha mnayaonaje ndugu zangu,dada zangu,Kaka zangu.

Kila nilichopanga kufanya mwaka huu naona kabisa hakitimii.

Dada yangu mmoja hapa mtaani anasema nisijipe presha bado mdogo,nitafanikiwa tu kwa uwezo wa Mungu, lakini Mimi mwenyewe nina marafiki kibao,naona kama wanaendelea vizuri na mambo yao.

Na Mimi kila siku najiuliza nawezaje kufanikiwa na Elimu yangu ya kuunga unga ?

Kudanga siwezi,
Kutapeli ni mwiko kwangu,

Pamoja na hivi nilivoo naenjoy Kula pesa ya jasho halali iliyo na Baraka za Mungu. Je nitafanikiwa vipi.
Nawaombeni ushauri.
Maria D.
 
Back
Top Bottom