ipo talaka kwa wakristu kama sababu ni uzinzi,ukifanya uzinzi ukakamatwa au ukimkamata mwenzio na uzinzi na ushaidi uliokamilika talaka inakuhusu,hata kanisa ikigoma kuvunja ndoa talaka ipo,ukiishi na mtu mzinzi ni kufurahisha watu uambiwe ndoa bado ipo lakini ndoa ina muhusisha mungu,mungu anaona uzinzi hata ukaufanyie Kenya,na ukiachwa kwa uzinzi ukiolewa anayekuoa ana zini tu hata mkifunga ndoa kanis la uingereza ambapo hujulikani!
From the very beginning, Mungu hakutaka kabisa talaka iwepo. Isipokuwa, kutokana na ugumu wa mioyo yetu, basi aliruhusu talaka under certain circumstances. Ingawa pia talaka sio kitu cha kuwa encouraged, isitokee tu kosa na mtu aka-opt talaka. Talaka inatakiwa kuwa last option baada ya series za vikao vya "kukiri, misamaha, kupatanishwa na kujirudi" kushindwa kabisa (unrepentant, serial cheater)
Malaki 2:16
Maana mimi nachukia kuachana, asema BWANA, Mungu wa Israel......
Kwa hiyo Mungu hataki kabisa wanandoa kuachana. Ila akaruhusu tu kuachana kwenye situation hizi
1. UASHERATI
Mathayo 19:3-9
6: Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
7: Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8: Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
9: Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
#(Mathayo 5:32)
Kwa hiyo kumbe kuna talaka kuja inayoruhusu kuoa/kuolewa tena (Re-marry), na kuna talaka isiyoruhusu kuoa/kuolewa tena
2. KUTELEKEZWA NA MKE/MUME ASIYEAMINI
1 Wakorintho 7:12-15
13: Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.
14: Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.
15: Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.
Kwa situation ya huyo dada aloletewa thread, japo Mungu hajaruhusu talaka, nafikiri hata Mungu hapendi wala hafurahishwi na vipigo. "Mke ni mwili wako", sasa mtu anayempiga mkewe hadi kuzimia siku 3 ni anamconsider kweli mkewe kuwa ni mwili wake? Nani anayeweza kuupiga hivyo mwili wake?
Nafikiri mke after series za kuonyana, misamaha na kupatanishwa kushindikana, anaweza akaondoka na wanae kukimbia hizo abuses (kutengana kwa muda), but sio kuomba talaka. Anaondoka ili ampe huyo mume muda wa kujitafakari, kuomba msamaha na kujirudi, aachane na hizo habari za kupigana kabisa. Akisema abaki tu, hatuna uhakika na usalama wa maisha yake+ vile vipigo vinatraumatize sana watoto. Under this situation sidhani hata kama wakiachana wataruhusiwa kuoa/kuolewa tena
N:B baada ya kuachana make sure umetubu + maombi ya rehema, kwa kushindwa kutimiza Agano mliloliweka mbele za Mungu (mpaka kifo kiwatenganishe), coz honestly hatutakiwi kuweka Agano then tukashindwa kulitimiza. Mungu wetu ni mwaminifu anatimiza ahadi zake zote juu yetu, inakuwaje wewe umdanganye na kutotimiza ahadi yake kwako? So ikitokea basi make sure unavunja nguvu ya Agano lile, otherwise Agano litakutesa maisha yako yote
Kumbukumbu 23:23
Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.
Mathayo 12:36-37
36: Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.