bht
JF-Expert Member
- May 14, 2009
- 10,336
- 1,860
Huu ni mojawapo wa ushauri alopewa .........
Nyie wanawake acheni ujinga! Mdada mwenye topic nakushauri kaa na huyo baba na endelea kula uroda na mtoto ongeza, siku hizi kuna Ndoa? Au mnadanganywa tu! Huyo anayesema unakubali kushea mkuki (hapa nimeondoa neno halisi) tena hiyo anayofikiria yeye kuwa ni ya kwake peke yake basi ndio inaingizwa kwa zaidi ya wanawake watatu kwa taarifa yake. Siku hizi mapenzi ni makbaliano tu. Hakuna mwanaume anaeingiza kwenye xxxx 1. Tena ukitoka kwa huyo baba hutakaa mpate ambae atakujali na kukutimizia kama huyo, au unafikiri ukiolewa ndio huyo atakae kuoa atakuwa wa kwako peke yako? nae atakuwa na wa pembeni (mwenzio) kama ulivyo wewe kwa bimkubwa wako. Hakuna cha Ukristu wala Uislam siku hizi tena hao Wakiristu ndo wanawake zaidi ya watano, mfano ninao kwa kaka zangu, na ni wakristu. Mama X wewe jifariji kama tu ukidhani ni wa kwako peke yako, Halooooooo
Nimechoka
Mwingine amesema ......
Nimerudi babaT , na ninasema hivi wote mnaomshambulia huyu dada ni wale wachache, waoga, msiojiamini.HII NDIO HALI HALISI SASAHIVI MTAKE MSITAKE,. mikuki mtaendelea kushare tu tofauti ni kuwa wengine mnajua mnashare wengine hamjui tu. Sasa mnaosema eti sijui kakunulia vitu, kakulea, leo unamuacha , umempata mwingine, si mseme tu kwa ufupi kuwa aendelee tu kupeana naye company, walee mtoto mradi amheshimu mke mwenzie? mbona mnazungusha sana mambo.
Nyumba ndogo haziishi hata mkeshe mnazipiga vita hapa. Nimependa kuna mdau kasema hapo juu kuwa kutoa ushauri sio lazima mtukane, kweli, kama mnataka toeni ushauri amuche namna gani, aanzeje maisha mwenyewe n.k ila sio ooh sijui ulimuibia mwenzio, sijui ulimtesa, kwani aliwákuta kitandani wanafanyana akamvuta huyo baba au huyo baba ndio alivaa chupi yake na suruali akaenda kumtongoza, wanawake bwana ndio maana mtaendelea kusumbuliwa na hili jambo, halitaisha kwa sasa limekomaa kama ukoma.
Ikifika zamu yako mume yuko ndani we muhudumie utulie, akitoka, we omba mungu, maana huko aendako haujui, anaenda kupewa nini, so hata akuite Sweet, sijui Honey pie, we omba mungu tu, lakini kukufuru na kumtukana mwenzenu mnakosea. MamaLo umeongea point, hawajakuelewa tu watu, good MamaLo hiyo ndio njia peke ya kuishi sikuhizi kwa amani hapa duniani, sio kumuuliza mwanamke mwenzio eti unaona raha gani kushare mkuki, kwani wewe unaona raha gani kufichwa ukweli na kuchekwa usogoni na kudanganywa kama mtoto mdogo? Nyumba ndogo za sikuhizi ndio zingine unakuta mpaka wakwe wanamjua wanamualika kwenye shughuli zao, wanaenda kumtembelea kuona watoto, sasa hapo NANI ALAUMIWE?mapenzi ni magumu kama siasa.
Mmezaliwa mmeyakuta, mtakufa mtayaacha,we kama hupendi kushare mwaname mfundishe mwanao wa kike akikuwa ajitahidi kabisa asifanye hivyo, lakini sio kukaa kutukana watoto wa wenzio hapa, wenyewe nao wametongozwa kama wewe.Nyumba ndogo nyingi za siku hizi wala hazifuati matunzo na pesa, wana hela zao nzuri tu, tena wengine ndo wanawakopesha waume zenu pesa, mnakula nyie.Oooohh, kalagheni BAHO. SALINI TU MSIJE MKAINGIA MAJARIBUNI, huo ndio ushauri wangu kwenu.
Huyu ni mbaba uwiiiiii.
Haya sasa mengine loh
am starving lakini ngoja niende ulikozitoa hizi posts tu sasa
nimechoka