Nelson Jacob Kagame
JF-Expert Member
- Dec 26, 2022
- 9,473
- 12,861
Kama mwandishi wa habari huru nilikua nachunguza viini vya migogoro katika maeneo ya ukanda huu wa maziwa makuu.
Nilibahatika kufanya mahojiano ya kina na washirika wa iliyokua serikali ya Rwanda kabla ya kupinduliwa mwaka 1994.
Watu wengi hawawezi kujua kua,karibia majenerali wote wa iliyokua serikali ya Rwanda mwaka 1994 walikimbilia nchi ya Zaire kabla ya baadhi yao kwenda ughaibuni kuishi.
Nilibahatika kufanya nao mahojiano kuhusu kupinduliwa kwao na wanajisikia vipi kupinduliwa na kuishi ukimbizini.
Niliwauliza je wanajihisi vipi na wao kufukuzwa kwa mtutu wa bunduki hadi ukimbizini na wale watu waliokua nao wamekimbizwa ukimbizini kwa mtutu wa bunduki.
Niliwauliza kuhusu mauaji ya kimbari na kikabila dhidi ya watusi wengi na wahutu wachache.
Niliwauliza kuhusu chuki waliyokua wanaipandikiza kama watawala kwa wananchi ili kuleta machafuko.
Niliwauliza kuhusu ukabila baina ya watusi na wahutu na wakati wote wanaongea lugha moja kinyaruanda.
Niliwauliza kuhusu mipango yao baada ya kupinduliwa ipoje.
Niliwauliza kuhusu wanajisikiaje wanapotuhumiwa kama wapangaji wa mauaji ya kimbari dhidi ya binadamu wenzao. Niliwauliza kuhusu vikosi vya wanamgambo makatili na wauaji wa intarehamwe.
Niliwauliza kuhusu mahusiano yao kisiasa na nchi jirani.
Nitakua nawaletea kwa vipengele hayo mahojiano yangu yote na vizazi vya wanajeshi wa iliyokua RAF (Rwanda Armed forces) kabla ya kupinduliwa na RPF forces mnamo mwaka 1994.
Mahojiano yanajumuisha mambo mengi ya kiuchumi na kisiasa na kitamaduni.
Na kuna ukweli ambao watu wengi hawaufahamu na hata kama unafahamika basi watu hawapendi kuuzungumza.
KABLA YA MFULULIZO WA MAHOJIANO YANGU NA WASHIRIKA WA FDLR NITAANZA NA HISTORIA FUPI YA MUHUSIKA MMOJA KAMA ALIVYONIADITHIA.
June 16 saa tatu usiku kwenye eneo la Gatuna au kwa kinyarwanda Katuna mpakani mwa Uganda na Rwanda 1987.
Kulikua na mkutano wa nje ya kambi kwenye upande ule wa mlimani kwenye mji ule wa mpakani.Na mkutano wenyewe ulikua wa makanali wa jeshi na wanajeshi wa vyeo vya chini waliokua wanaifuatilia hali ya wasiwasi mpakani katika mji wa Gatuna upande wa mpaka wa Uganda.
Taarifa za kijasusi za jeshi la Rwanda zilikua zinasema kua,wakimbizi wa kinyarwanda waliokua upande wa nchi ya Uganda walikua wanajiandaa kuivamia nchi ya Rwanda.Taarifa zilisema kua wanyarwnda ambao wamesajiliwa katika jeshi la NRM la Uganda walikua wanaondoka jeshini kwa kasi na kuenda kuunda vikosi vya kijeshi ili kuishambulia Rwanda.
ITAENDELEA!
- Sehemu ya Pili
- Sehemu ya Tatu
Nilibahatika kufanya mahojiano ya kina na washirika wa iliyokua serikali ya Rwanda kabla ya kupinduliwa mwaka 1994.
Watu wengi hawawezi kujua kua,karibia majenerali wote wa iliyokua serikali ya Rwanda mwaka 1994 walikimbilia nchi ya Zaire kabla ya baadhi yao kwenda ughaibuni kuishi.
Nilibahatika kufanya nao mahojiano kuhusu kupinduliwa kwao na wanajisikia vipi kupinduliwa na kuishi ukimbizini.
Niliwauliza je wanajihisi vipi na wao kufukuzwa kwa mtutu wa bunduki hadi ukimbizini na wale watu waliokua nao wamekimbizwa ukimbizini kwa mtutu wa bunduki.
Niliwauliza kuhusu mauaji ya kimbari na kikabila dhidi ya watusi wengi na wahutu wachache.
Niliwauliza kuhusu chuki waliyokua wanaipandikiza kama watawala kwa wananchi ili kuleta machafuko.
Niliwauliza kuhusu ukabila baina ya watusi na wahutu na wakati wote wanaongea lugha moja kinyaruanda.
Niliwauliza kuhusu mipango yao baada ya kupinduliwa ipoje.
Niliwauliza kuhusu wanajisikiaje wanapotuhumiwa kama wapangaji wa mauaji ya kimbari dhidi ya binadamu wenzao. Niliwauliza kuhusu vikosi vya wanamgambo makatili na wauaji wa intarehamwe.
Niliwauliza kuhusu mahusiano yao kisiasa na nchi jirani.
Nitakua nawaletea kwa vipengele hayo mahojiano yangu yote na vizazi vya wanajeshi wa iliyokua RAF (Rwanda Armed forces) kabla ya kupinduliwa na RPF forces mnamo mwaka 1994.
Mahojiano yanajumuisha mambo mengi ya kiuchumi na kisiasa na kitamaduni.
Na kuna ukweli ambao watu wengi hawaufahamu na hata kama unafahamika basi watu hawapendi kuuzungumza.
KABLA YA MFULULIZO WA MAHOJIANO YANGU NA WASHIRIKA WA FDLR NITAANZA NA HISTORIA FUPI YA MUHUSIKA MMOJA KAMA ALIVYONIADITHIA.
June 16 saa tatu usiku kwenye eneo la Gatuna au kwa kinyarwanda Katuna mpakani mwa Uganda na Rwanda 1987.
Kulikua na mkutano wa nje ya kambi kwenye upande ule wa mlimani kwenye mji ule wa mpakani.Na mkutano wenyewe ulikua wa makanali wa jeshi na wanajeshi wa vyeo vya chini waliokua wanaifuatilia hali ya wasiwasi mpakani katika mji wa Gatuna upande wa mpaka wa Uganda.
Taarifa za kijasusi za jeshi la Rwanda zilikua zinasema kua,wakimbizi wa kinyarwanda waliokua upande wa nchi ya Uganda walikua wanajiandaa kuivamia nchi ya Rwanda.Taarifa zilisema kua wanyarwnda ambao wamesajiliwa katika jeshi la NRM la Uganda walikua wanaondoka jeshini kwa kasi na kuenda kuunda vikosi vya kijeshi ili kuishambulia Rwanda.
ITAENDELEA!
- Sehemu ya Pili
- Sehemu ya Tatu