Mahojiano na Dr. Harrison Mwakyembe

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
mwakyembe.jpg


Kesho siku ya Jumapili kuanzia majira ya saa saba za mchana (EST) sawa na saa tatu za usiku (Saa za Afrika ya Mashariki) tunatarajia kuwa na mahojiano na Dr. Harrison Mwakyembe Mbunge wa Kyela na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza kampuni ya Richmond. Ni matokeo ya Kamati hiyo ndiyo yaliyosababisha aliyekuwa Waziri Mkuu Mhe. Edward Lowassa kujiuzulu na hatimaye Baraza la Mawaziri kuvunjika.

Tutazungumza na Dr. Mwakyembe karibu mwaka mmoja kamili tangu matukio yale ya Februari 2008, matukio ambayo yalikuwa ni ya kihistoria. Tutazungumza naye pia mambo mengine ya kitaifa saa na wakati huu ambapo Taifa letu linapitia katika mabadiliko makubwa ya kifikra ambayo tumeyaasisi na kuyaongoza kwa umahiri mkubwa.

Utaweza kusikiliza mahojiano yetu kupitia KLHN kwenye MWANAKIJIJI.COM "live".

Wakati unasubiri, BONYEZA HAPA KUSIKILIZA MUZIKI
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Habari za siku?

Hivi utasave au lazima tusikilize moja kwa moja? Huku kanda ya ziwa mvua nyingi na umeme wa Tanesco shida tupu
 
Mkuu Habari za siku?

Hivi utasave au lazima tusikilize moja kwa moja? Huku kanda ya ziwa mvua nyingi na umeme wa Tanesco shida tupu

habari nzuri, natumaini mambo ni mazuri huko na mwaka mpya ni mwema na wa fanaka kwako na kwa familia. Nilifurahi kukutana nawe ulipokuja huku. Usiwe na wasiwasi.. kwa wale watakaokosa "live" au in case of unforeseen event tutaweza bado kurekodi na kuyacheza baadaye encore.
 
Dk. Mwakyembe awakatalia wapiga kura kuondoka CCM
Richard Kilumbo,Kyela

MBUNGE wa Jimbo la Kyela Dk Harrison Mwakyembe,amesema hana mpango na wala hafikirii kukiacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kujiunga vyama vya upinzani nchini.


DK. Mwakyembe alisema hakuna Chama chochote cha upinzani kinachoweza kufananishwa kwa ubora , umakini, uzuri wa sera na hata uwingi wa wanachama na CCM.


Kauli hiyo aliitoa juzi kwenye mkutano wake na wananchi wa jimbo lake uliofanyika viwanja vya Siasa mjini hapa ambapo baadhi ya wananchi walimtaka kuihama CCM ili afanye kazi ya kufichua mafisadi kupitia kambi ya upinzani.


Mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Erick Satta mkazi wa mjini hapa alisema wananchi wa jimbo lake wanamwamini mbunge huyo kwa kiwango kikubwa, lakini wanaingiwa na shaka na mahali aliko (CCM)ambako alisema wananchi wanaamini, mbunge wao anabanwa, na hawezi kusema lolote linalopingana na sera na itikadi ya Chama.


Satta alisema ili aweze kufanikisha azma ya kuwakomboa wananchi wa Tanzania mbunge huyo hana budi kubadilika na kujiunga na mageuzi ambako ataungwa mkono kutoka kwa wananchi na viongozi wenzake wa vyama vya upinzani.


Alimtaka mbunge huyo kukubaliana na matakwa ya wananchi wengi wanaomshinikiza kuihama CCM kwa madai kimejaa mafisadi wasiowezwa kushughulikiwa na kiongozi wa ndani ya Chama hicho.


" Tunakupenda,tuko nawe na tutakuchagua mwaka 2010, ukiwa ndani ya Chama kingine, cha Siasa na siyo CCM" alisema Satta.


Akijibu hoja kwa kupinga msimamo huo, Dk. Mwakyembe aliwabeza wale wote wanaomshinikiza kuihama CCM na kusisitiza kwamba, hapa nchini hakuna Chama cha siasa kilicho makini na chenye sera safi zinazotekelezeka na chenye wanachama wengi kuliko CCM.


Dk. Mwakyembe alisema, mtu yeyote anayetaka kupambana na maovu yanayofanywa na baadhi ya watu walio na nia mbaya na Taifa lao hana budi kuendelea kubaki ndani ya CCM.


"Ukitaka kufanya mambo yako vizuri,na unataka usikilizwe, uishi maisha marefu ni bora, ubaki CCM kuliko ukawa kwenye upinzani na kupayuka mambo bila ushahidi wa kutosha.


Alisema utetezi na uchungu wa mtu yoyote hauwezi kusikika, na kufanyiwa kazi kwa kina, kama utafanywa na wapinzani walio nje ya CCM.


Akitetea msimamo wake alisema ni lazima watu washindane na kubezana kwa hoja kuliko kuleta ubishi usio na manufaa.


"Fikiria ujasiri unaofanywa na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete , ni mkubwa mno, lakini wapo watu wanaobeza jambo ambalo hata CCM ingefanya nini, wapo watu ambao wataendelea kubeza tuu.


Alisema, Rais Kikwete amefanya mambo mengi na yenye ushujaa kwa kuweza kuwafikisha viongozi waandamizi aliowahi kufanya nao kazi katika awamu mbalimbali akiwa Waziri , lakini amefanikisha kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola wakituhumiwa kuitia hasara Serikali ya awamu ya tatu kwa kuruhusu msamaha wa kodi ya Sh 11 bilioni.


"Hivi, ni nani kati yenu, anayeweza kuruhusu rafiki yake wa karibu akamatwe, hata kama amekosea?, na ni Kiongozi gani katika awamu zote tatu zilizopita aliyeweza kuwa jasiri akaruhusu marafiki na viongozi wenzake wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya dola kama si Rais Kikwete"aliwauliza wananchi Dk.Mwakyembe.


Hata hivyo, pamoja na kusifia mafanikio mbalimbali yaliyoletwa na Serikali ya awamu ya nne, Dk Mwakyembe alizungumzia pia kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, ambaye alisema aliimarisha na kuinua Uchumi wa nchi.


Kuhusu sakata la kukatika katika kwa umeme wilayani Kyela , mbunge huyo alisema atayapeleka mawazo ya wananchi waliomtaka mbunge wao ayafikishe mambo hayo kwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngereja ya kuruhusu wananchi wa Kyela wautumie umeme unaozalishwa na Kiwira Coal Mine ili kuepuka na kero hiyo.
 
Na Isango Josephat Ng?imba
HUYU ndiye Dk. Harrison Mwakyembe au vyombo vya habari vimetudanganya? Soma kauli aliyonukuliwa akitoa na kukaririwa na gazeti la Mwananchi toleo la 14 Januari 2009:

"Ukitaka kufanya mambo yako vizuri, na unataka usikilizwe, uishi maisha marefu, bora ubaki CCM kuliko ukawa kwenye upinzani na kupayuka mambo bila ya ushahidi wa kutosha.”

Tumesoma kuwa Mwakyembe alitoa kauli hiyo kwenye mkutano na wananchi wa jimbo lake uliofanyika viwanja vya Siasa, mjini Kyela ambako baadhi ya wananchi walimtaka kuhama CCM ili afanye kazi ya kufichua mafisadi kupitia kambi ya upinzani.

Akijibu hoja za wananchi hao, Dk. Mwakyembe alitumia maneno niliyonukuu hapo juu ambayo ndio chanzo cha hofu yetu kuhusu “mpiganaji huyu.” Kauli hii inalenga kutuambia nini?

Hii ina maana hakuna usawa? Kwamba katika CCM utasikilizwa lakini katika upinzani utapuuzwa? Kumbe madai ya upinzani kuwa utawala huu hauna usawa ni sahihi?

Kwamba “maisha marefu” yanapatikana CCM peke yake? Kwamba walioko upinzani maisha yao mafupi kwa kuwa hawaungi mkono CCM? Hii ni kwa kuwa ni masikini, hawana chakula au ni maadui na hivyo watauawa na CCM?

Nadhani Mwakyembe alisema haya bila kujua kutakuwa na mwandishi wa habari kunukuu kauli yake. Vinginevyo anajua uwezo mkubwa wa wabunge wa upinzani na umma mkuu ulioko nje ya bunge na nje ya vyama.

Mikataba ya ovyo kama ule wa Buzwagi; kashfa ya Richmond iliyomwangusha Edward Lowassa katika uwaziri mkuu; wizi mkubwa Benki Kuu na mengine, yameibuliwa na wabunge hawa. Kwanza yalibezwa, baadaye yakakumbatiwa; CCM ikayadandia kutafuta umaarufu.

Mwakyembe anataka kusema nini kwa wananchi wa jimbo la Kyela wasiokuwa CCM? Je, yeye alichaguliwa na wana-CCM peke yao? Je, maadili ya kujua mema na mabaya yanatofautishwa kwa kutumia misingi ya uanachama wa vyama vya siasa?

Kama ni lazima kuwa CCM au kubaki humo ili ufanikiwe, ina maana wasio wanachama wa chama hicho ni watu wa kulaaniwa? Mwakyembe anatufundisha nini sisi tuliomwona mzalendo, aliyesimama bila kutetereka kutetea maslahi ya nchi katika sakata la Richmond?

Kama alivyonukuliwa ndivyo alivyo; kwa maana kwamba amekuwa akificha sura yake halisi, na kwamba anaona kuwa maisha nje ya CCM hayawezekani, basi amejipunguzia sana heshima tuliyowahi kumpa.

Ina maana uchungu wa mwana-CCM kwa nchi hii unatofautina na uchungu wa mwana wa chama kingine? Kwamba tatizo la mwana-CCM ni tatizo zaidi kuliko tatizo la raia mfuasi wa chama kingine? Tunawaweka wapi wale wasio wafuasi wa chama chochote?

Nakaribia kushawishika kwa kauli ya rafiki yangu kuwa raia wa Tanzania si “Watanzania” maana “Watanzania” wana maisha bora kama kauli mbiu ya “maisha bora” inavyosawiri kwao. Sisi tusio na maisha bora si Watanzania.

Nisingejisikia vibaya iwapo Mwakyembe angesema atafanyia kazi ilani ya CCM na kwamba hana mpango wa kuhama chama chake, kuliko kutoa kauli zinazolingana na vitisho.

Nimesadikishwa kuwa kwa mwanafalsafa hakuna tamko la bahati mbaya. Nami naona Mwakyembe alikusudia kusema hayo na ameyasema. Kwa kuwa kila kauli ina gharama, basi kauli ya Mwakyembe imemgharimu heshima.

Mwandishi ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu – ualimu – Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine, SAUT, anayepatikana kwa simu: 0786-426414 na baruapepe: joseisango@yahoo.com
 
Mwakyembe anapoficha mambo kulinda ?heshima ya serikali?

Chesi Mpilipili Julai 2, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

KUNA mambo kadhaa yanayofanywa na viongozi wa nchi hii ambayo ni kielelezo tosha cha jinsi kulivyo na ombwe la watu wanaostahili kweli kuwa na kuitwa viongozi wa wananchi.

Ni mambo ambayo ni kielelezo halisi cha jinsi viongozi wetu walivyo tayari kuweka kando maslahi ya waliowachagua kushika nyadhifa walizo nazo iwapo kwa kufanya hivyo watakuwa wanapalilia maslahi yao kwa kwa mamlaka za juu zenye nguvu zaidi kuliko wapiga kura wao.

Naomba nizungumzie matukio mawili tu ya hivi karibuni kama mifano hai. Matukio haya yametokea kwenye nyanja mbili tofauti; lakini zinazohusiana na maisha ya kila siku ya Watanzania. Siasa na michezo.

Tuanze na lile la michezo. Siku chache zilizopita kulikuwa na taarifa za mgogoro mdogo wa viongozi kwenye moja ya timu mbili kubwa za soka, ukubwa ambao sio lazima uwe ni kutokana na usakataji wa kabumbu mahiri wa timu hizo.

Mgogoro huu ulianza pale uongozi wa klabu hiyo ulipofanya kilichoelezwa kuwa ni kumsimamisha mweka hazina wa klabu hiyo kutokana na makosa ambayo hayakuwekwa wazi zaidi ya kusemwa kuwa ni ‘kuvunja kanuni za uongozi.’

Taarifa hii ya uongozi wa klabu ikafuatwa siku chache baadaye na taarifa kutoka kwa mweka hazina wa klabu ambaye pamoja na mambo mengi alisema kuwa anasubiri barua rasmi kutoka kwa viongozi ili na yeye ‘alipue mabomu’!

Kiongozi yule wa karne ya ishirini na moja wa klabu yenye mamilioni ya wanachama, wapenzi na mashabiki akasisitiza kwamba alikuwa na mengi tu ya kuyasema kuhusiana na viongozi wenzake na angeyasema mara tu baada ya kupata barua rasmi ya kusimamishwa!

Kama vile haitoshi, siku chache baadaye katika kile wengi walichoona kuwa ni kutafuta huruma ya wapenzi wa klabu hiyo, kiongozi huyo aliibuka tena na kudai kuwa alikuwa ameandika barua ya kuomba aruhusiwe kukarabati uwanja wa klabu hiyo ambao ulikuwa mahututi lakini alikuwa hajapata jibu kutoka kwa viongozi waliomsimamisha!

Kwangu mimi, na bila shaka kwa wapenzi wengi wa michezo nchini, hiki kilikuwa ni kilele cha unafiki. Huyu alikuwa ni kiongozi wa muda mrefu tu kwenye safu za uongozi za klabu hiyo ya soka na kama angekuwa na nia ya kweli ya kuukarabati uwanja wa klabu yao angeweza kufanya hivyo pengine bila hata kuhitaji kuomba ruhusa kwa mtu zaidi ya kutoa taarifa tu!

Lakini alikuwa amesubiri hadi wenzake walipomsimamisha uongozi ndipo akaona ule ndio ulikuwa muda muafaka si tu wa yeye kukarabati uwanja wa timu yake bali zaidi mno kuwatangazia wanachama jinsi alivyoandika barua kwa viongozi wenzake ili kupewa amana hiyo lakini alikuwa hajajibiwa!

Hilo ni moja. Kubwa zaidi lilikuwa lile la kuwaambia wanachama kuwa alikuwa na mambo mengi ya kusema kuhusiana na uozo uliomo kwenye uongozi uliomsimamisha lakini alikuwa anasubiri kwa hamu uongozi huo umpe rasmi barua ya kumsimamisha ili na yeye alipue mabomu!

Tatizo la viongozi wengi wa nchi hii ni kuwachukulia Watanzania kuwa ni maamuma wasiojua kuchanganua mambo. Haikuhitaji akili za ziada hapa kung’amua kuwa alichokuwa anafanya kiongozi huyu ni kutetea unga wake tu kwa kuwatingishia kibiriti viongozi wenzake na haikuwa kwa ajili ya manufaa ya klabu na wanachama wake.

Kwa maana nyingine, kiongozi huyu aliyechaguliwa na wanachama wa klabu alikuwa anamfahamu uozo uliokuwa ndani ya safu ya uongozi wa klabu yao lakini alikuwa anasubiri atofautiane na viongozi wenzake kwanza ndipo aone umuhimu wa kuwaambia wanachama juu ya uozo uliopo kwenye uongozi wa klabu yao!

Na hii pia iwe mpaka apewe barua ya kusimamishwa kazi kwanza ndio aumwage uozo huo hadharani. Bila barua, uozo huo ungeendelea kuwa siri yake! Hawa ndio viongozi wetu wa michezo.

Tuhamie kwenye siasa. Wakati kashfa ya EPA ilipoanza kushika kasi, taarifa za baadhi ya magazeti zilituambia kuwa kuna kiongozi ambaye alikuwa anasema kuwa iwapo angetajwa tu kuhusika na kashfa hiyo basi asingekubali kwenda na maji peke yake. Angekufa na mtu.

Kwa maana nyingine ni kwamba kiongozi huyu angetaja majina ya wahusika wa kashfa hiyo iwapo tu yeye angetajwa kuhusika. Kama wasingemtaja, basi, naye asingewataja na kwa maana hiyo Watanzania wanaosubiri kwa hamu kubwa majina ya wahusika hao, watasubiri mpaka wachoke.

Kwa vile hizi zilikuwa ni taarifa za magazeti ambazo hakuna jina lililotajwa, naomba tuziache kama zilivyo na badala yake tuhamie kwenye yale yaliyotokea majuzi pale mjini Dodoma kwenye kikao cha Bunge kinachoendelea huko sasa.

DK. Harrison Mwakyembe

Wakati anachangia hotuba ya bajeti ya ofisi ya waziri mkuu, mwenyekiti wa kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza utaratibu uliotumika hadi kampuni ya Richmond kupewa tenda ya kufua umeme, Mh. Dk. Harrison Mwakyembe ametoa kauli tete ambayo kwa hakika imewachanganya watu si haba.

Kwanza, Mh. Mwakyembe alieleza kushangazwa kwake na wabunge waliokuwa wanatoa hoja za kuwasafisha watuhumiwa wa kashfa ya Richmond na kuwataka kama hawakubaliani na uchunguzi wa kamati yake, basi, wavunje kanuni husika za Bunge ili mjadala wa Richmond urudishwe tena Bungeni kujadiliwa upya.

Akaenda mbali zaidi kwa kusema kuwa iwapo mjadala huo utafunguliwa tena, basi, kamati yake ingeyasema hata yale ambayo kamati yake ilikuwa imeficha kuyasema ili kulinda heshima ya Serikali iliyo madarakani!

Hii kwa hakika ilikuwa ni kauli nzito na ya kushitua kutoka kwa mtu ambaye Watanzania walio wengi wanamuona ni shujaa kutokana na kuongoza kamati iliyotoa taarifa iliyosababisha waziri mkuu na mawaziri watatu kujiuzulu kwa mpigo, ‘tetemeko’ ambalo halijawahi kutokea nchini.

Binafsi, nimejikuta nikiifananisha kauli hii na ile ya yule kiongozi wa timu kubwa nchini aliyesema kuwa anangoja apewe kwanza rasmi barua ya kusimamishwa uongozi na viongozi wenzake ndipo na yeye ataje uozo ulio kwenye uongozi huo!

Tungeelewa iwapo Mh. Mwakyembe angesema kuna mambo waliamua kuyaficha kwa vile kama wangeyasema yangeweza ‘kuhatarisha usalama wa taifa letu’. Hili tungekubaliana nalo. Lakini ‘ili kulinda heshima ya serikali’?

Ni kauli ya utata ambayo bado najitahidi kujipa matumaini kwamba pengine ilimtoka tu kwa bahati mbaya Mh. Mwakyembe kutokana na jazba aliyoonyesha kuwa nayo kama hotuba yake ilivyoonyesha na hakufikiria madhara yake pale wananchi watakapoanza kuichambua.

kwa hakika, kauli ya Mheshimiwa Mwakyembe imezua maswali mengi zaidi kuliko majibu miongoni mwa Watanzania wanaomchukulia kama shujaa wao. Ni mambo gani hayo makubwa zaidi ambayo kamati ya Mh. Mwakyembe iliyaacha kuyasema au kuyaweka katika ripoti yao ili ?kulinda heshima ya serikali??

Iweje wabunge wetu hawa waone kuifichia serikali yale ambayo yangeweza kusababisha heshima yake ipungue ni muhimu zaidi kuliko kutuwekea wazi kila kitu sisi waajiri wao na kutuacha tuamue wenyewe ni lipi ambalo litaitia aibu serikali na lipi halitaitia aibu?

Je, kwenye hadidu za rejea za kamati yao teule kulikuwa na kanuni inayowataka kuficha mambo ambayo wangeona ni mazito mno kiasi cha kuhatarisha heshima ya serikali? Ni kigezo gani walichotumia katika kuamua kuwa haya ni mambo mazito na yangeweza kuiaibisha serikali na haya sio mazito tuyaweke wazi?

Na baada ya kauli hii ya utata ni kipi sasa kitatufanya tusiamini maneno ya ‘majeruhi’ mmoja wa kisiasa aliyesema kuwa kama kamati hiyo ilikuwa na uwezo wa kuamua kutosema baadhi ya mambo, basi, pia ilikuwa na uwezo wa ‘kuchomekea’ baadhi ya mambo ili kuhalalisha makosa ya baadhi ya waheshimiwa waliotuhumiwa na kamati hiyo?

Tunadhani ni vizuri Mheshimiwa Mwakyembe na kamati yake akaharakisha kufafanua kauli tete yake hii. Yeye bado ni shujaa kwa Watanzania walio wengi.

Tusingependa Watanzania wafike mahali pa si tu kumfananisha na yule kiongozi wa klabu anayengoja apewe barua ya kusimamishwa uongozi na wenzake ndipo atuambie uozo wa uongozi wao; bali pia tusingependa tuanze kujiuliza ni upande gani wa kipande chake cha mkate Mheshimiwa Mwakyembe anachoona kimepakwa siagi. Upande wetu wapiga kura au upande wa serikali?
 
Dk. Mwakyembe anamlinda nani?

Tahariri
Tanzania Daima

KAULI ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kati ya Kampuni ya Richmond ya Marekani na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuwa Spika aruhusu kuvunja kwa kanuni za Bunge ili kutoa fursa ya kujadili kwa kina sakata hili, bado inaendelea kutufikirisha mbali.

Tulieleza mapema kuwa, tunakubaliana na kauli hiyo ya Dk. Mwakyembe baada ya kubaini kuwa kumbe kulikuwa na mambo yaliyofichwa katika ripoti hiyo kwa sababu alizoeleza kuwa ni kulinda heshima ya serikali. Jambo hili bado linatufanya kujiuliza maswali mengi pasipo kupata majibu sahihi.

Kikubwa tunachojiuliza ni nani aliyelindwa katika ripoti ya kamati hiyo, ambaye kutajwa kwake hadharani kuwa naye alihusika katika sakata hilo kunaweza kuondoa heshima ya serikali?

Katika ripoti ya kamati hiyo iliyosomwa bungeni na Dk. Mwakyembe, kulikuwa na mambo mazito yaliyoivua nguo serikali kwa kuhusishwa kwa baadhi ya watendaji wake wa ngazi za juu kwa namna moja au nyingine na sakata hilo. Jambo lililolazimisha wajiuzulu.

Waliolazimika kuachia nyadhifa zao kutokana na kutajwa katika ripoti hiyo ni aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa pamoja na mawaziri wengine, Nazir Karamagi aliyekuwa Wizara ya Nishari na Madini wakati huo na Dk. Ibrahim Msabaha aliyekuwa Wizara ya Afrika Mashariki. Dk. Msabaha ndiye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati mkataba huo unasainiwa.

Ikumbukwe kwamba, baada tu ya Lowassa kutajwa katika ripoti hiyo, aliposimama bungeni hakutaka kujitetea, bali alieleza masikitiko kwa kile kilichoelezwa na kamati hiyo juu yake kuwa kilimfedhehesha sana, kulimdhalilisha na sana na alikuwa ameonewa sana. Kisha akatangaza kuachia ngazi.

Kwa maana nyingine ni kwamba, Lowassa hakuwa anakubaliana moja kwa moja na ripoti ile.

Kama Lowassa, Karamagi naye hakukubaliana moja kwa moja na ripoti hiyo, alikubali kuachia ngazi kwa shingo upande, na mpaka sasa amekuwa akieleza wazi kuwa kamati ya Dk. Mwakyembe ilimuonea na anataka iundwe tume huru ya wanasheria kuchunguza utata huo.

Mbali na hao, hata Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ambaye pia alitajwa katika ripoti ya kamati ya Dk. Mwakyembe naye amesikika mara kadhaa akieleza kuwa kilichofanywa na kamati hiyo ya Bunge si sahihi. Zaidi kwamba zipo tetesi za muda mrefu sasa za kuwepo kwa ripoti mbili zilizoandaliwa na kamati hiyo.

Ingawa madai ya kuwepo kwa ripoti mbili yalionekana kupuuzwa na wengi, lakini mwenendo wa mambo ulivyo sasa unaashiria kuwa waliokuwa wakidai hivyo ni wale waliojua kuwa Dk. Mwakyembe hakueleza kila kitu kilichogunduliwa na kamati yake, kuna watu aliwalinda.

Tunajiuliza, kama ripoti hiyo ilimtaja aliyekuwa Waziri Mkuu naye akalazimika kuachia ngazi kwa fedheha, kigogo mwingine aliye juu ya Waziri Mkuu ambaye kamati iliamua kumhifadhi ili kuilinda serikali ni nani?

Viongozi walio juu ya Waziri Mkuu wanafahamika kuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano na Makamu wa Rais kwa Tanzania Bara na kwa Tanzania Visiwani ni rais wa visiwa hivyo.

Kama Waziri Mkuu alitajwa, ni wazi kuwa anayefichwa katika ripoti ya kamati hiyo ni mzito kuliko Waziri Mkuu ambaye kutajwa kwake kunaweza kuchafua heshima ya serikali.

Tunapenda wajumbe wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata huo watambue kuwa, viongozi wote wa kisiasa waliopo madarakani ni kwa ridhaa ya wananchi ambao wanakamuliwa jasho lao ili kuhakikisha wanaishi maisha yenye heshima na hadhi ya juu. Hivyo kama wanahusika na kashfa ya aina yoyote, hasa ya kufuja mali za waliotoa fedha zao kuwatunza, jamii ina haki ya kuwafahamu hata kama haitawahukumu.

Vinginevyo, kama jamii itanyimwa haki hiyo, tutalazimika kusadiki kwamba ripoti ya Dk. Mwakyembe ina upungufu mwingi, na yanayolalamikiwa na waathirika wa ripoti hiyo yana msingi.
 
Ninavyojua na kuamini hakuna anelindwa ila kuna ushahidi zaidi na wa wazi dhidi ya EL katika kashfa ile na alivyokuwa anahaha kutaka asitajwe ......pia ushawishi mke wa EL kwa kamati kuhUsu kufukiamashimo ili angalau kulinda ka heshima kidogo kalikobia ka EL la sivyo ilitakiwa atolewe leo kesho yk kizimbani.....aibuuu
 
greetings Mzee mwanakijiji.

Kama mazungumzo yenu ni katika hali ya maswali na majibu, naomba umuulize ana mkakati gani wa kupunguza tatizo la njaa na kipato hafifu la wakazi wa jimbo lake hasa wa vijijini.
 
tuko live sasa hivi kwenye countdown ya mahojiano na Dr. Mwakyembe.. kama mnamaswali hapa ndipo mahali pa kuanza kuyaweka...
 
Acha miyeyusho, yaani unampigia simu mhojiwa halafu unamwambia ukiwa tayari nikupigie wakati hajakwambia hayuko tayari, no wonder simu ikakatwa. Hata ingekuwa mimi ningekuambia kwamba siko tayari!!!
 
Last edited by a moderator:
Tatizo redio yako umeweka high bandwidth so kwa sisi wenye connection zenye speed ndogo hususani wa hapa tz husikiki vizuri....unakwama kwama.....
 
Tatizo redio yako umeweka high bandwidth so kwa sisi wenye connection zenye speed ndogo hususani wa hapa tz husikiki vizuri....unakwama kwama.....

bila ya shaka tutaweza kuhakikisha tunasikika vizuri wiki ijayo baada ya kubadilisha settings zetu. Hata hivyo mahojiano haya yataweza kuwadownloaded kwenye KLH News au kwenye mwanakijiji.com

shukrani for observation.
 
Mtu hata ukiongea point huku unakimbia asili yako ni ujinga, ana-twang kiswahili? mwanzo nilifikiri ni mzungu anayezungumza kiswahili baadae naona alisahau kuendelea na igizo. Tujivunie asili zetu jamani!!
 
Back
Top Bottom