Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #41
Mzee Mwanakijiji,
Haya mahojiano yanapatikana wapi?
Tayari yapo kwenye Mwanakijiji.com (Podcasts) au kwenye podomatic.. Asante kwa kuuliza.
Mzee Mwanakijiji,
Haya mahojiano yanapatikana wapi?
Majibu aliyoyatoa Mh. Dr. Mwakyembe, mbunge wa Kyela katika mahojiano yake na Mwanakijiji yamenifanya niamini 100% kuwa usanii ndani ya CCM na serikali umekomaa na unaambukiza. Kwamba kuna wapiganaji ndani ya CCM wanaoweza kuleta mabadiliko itabakia ndoto kama alivyodhihirisha Dr.
1. Huyu ndiye Dr. anayemtetea Mkapa na kumsifu kwa utendaji mzuri na kuwaomba watanzania waache kumhusisha na ufisadi.
2. Huyu ndiye kama mwenyekiti wa tume ya Richmond, kwa makusudi aliificha bunge sehemu ya ripoti kwa kuhofia kuiumbua serikali.
3. Huyu anatamka hadharani kuwa ukitaka maisha mazuri na wananchi wazidi kukusikiliza ubaki CCM - hata kama inanuka ufisadi.
4. Huyu huyu anamtetea Waziri Mkuu kwa matamshi ya hatari kwa kisingizio kuwa Pinda kama mwanasheria hawezi kutamka maneno kama hayo - labda waandishi wanafunzi ndio walichemka.
Haya ni baadhi tu ya mengi yanayonifanya nichukue kwa tahadhari kubwa yale yote yanayotamkwa na wale wanaoitwa eti wapiganaji ndani ya CCM. Asante MKJJ kwa kunifungua macho - huwezi kujifunika hilo hilo shuka lililo na wachafu halafu useme u msafi.