Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Mahita amshtaki msichana anayedai ni bintiye
Na Ummy Muya
ALIYEKUWA mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Omary Mahita amekumbwa na msukosuko mwingine baada ya binti wa miaka 15 kuibuka na kudai kuwa ni mtoto wake, jambo lililomfanya mstaafu huyo kumfikisha mahakamani kwa kosa la kuingia nyumbani kwake kijinai.
Tayari Mahita ameshashindwa katika kesi nyingine iliyofunguliwa na Rehema Shaaban, ambaye alidai kupewa mimba na mkuu huyo wa polisi na baadaye kumzaa mtoto anayejulikana kwa jina la Juma Omari Mahita. Alidai kuwa alipata ujauzito huo wakati akiwa mfanyakazi wa ndani wa Mahita.
Kesi mpya ya kamanda huyo wa zamani wa polisi mkoani Kilimanjaro ilitajwa kwa mara ya kwanza jana mbele ya Hakimu Mary Matoi kwenye Mahakama ya Mwanzo Kinondoni.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa binti huyo ambaye ni mkazi wa Sanya Juu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro alifika nyumbani kwa Mahita Oysterbay jijini Dar es Salaam na kumweleza kuwa yeye ni mwanaye aliyezaa na polisi mwenzie, Ester Lyatuu.
Karani wa mahakama hiyo, Fatuma Hatibu alimwambia Hakimu Matoi kuwa mtuhumiwa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Sophia Mahita, alifika nyumbani kwa mkuu huyo mstaafu wa Jeshi la Polisi Machi 22 mwaka huu, majira ya saa 5:00 usiku.
Mtuhumiwa huyo alikiri kufika nyumbani kwa Mahita na kusisitiza kuwa alifanya hivyo kwa kuwa ni baba yake mzazi.
Baada ya maelezo hayo ya awali Hakimu Matoi aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 12 mwaka huu itakapotajwa tena huku mtuhumiwa huyo akienda rumande kwa kukosa dhamana.
TAMWA NA WENGINEO MPO JAMANI
Na Ummy Muya
ALIYEKUWA mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Omary Mahita amekumbwa na msukosuko mwingine baada ya binti wa miaka 15 kuibuka na kudai kuwa ni mtoto wake, jambo lililomfanya mstaafu huyo kumfikisha mahakamani kwa kosa la kuingia nyumbani kwake kijinai.
Tayari Mahita ameshashindwa katika kesi nyingine iliyofunguliwa na Rehema Shaaban, ambaye alidai kupewa mimba na mkuu huyo wa polisi na baadaye kumzaa mtoto anayejulikana kwa jina la Juma Omari Mahita. Alidai kuwa alipata ujauzito huo wakati akiwa mfanyakazi wa ndani wa Mahita.
Kesi mpya ya kamanda huyo wa zamani wa polisi mkoani Kilimanjaro ilitajwa kwa mara ya kwanza jana mbele ya Hakimu Mary Matoi kwenye Mahakama ya Mwanzo Kinondoni.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa binti huyo ambaye ni mkazi wa Sanya Juu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro alifika nyumbani kwa Mahita Oysterbay jijini Dar es Salaam na kumweleza kuwa yeye ni mwanaye aliyezaa na polisi mwenzie, Ester Lyatuu.
Karani wa mahakama hiyo, Fatuma Hatibu alimwambia Hakimu Matoi kuwa mtuhumiwa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Sophia Mahita, alifika nyumbani kwa mkuu huyo mstaafu wa Jeshi la Polisi Machi 22 mwaka huu, majira ya saa 5:00 usiku.
Mtuhumiwa huyo alikiri kufika nyumbani kwa Mahita na kusisitiza kuwa alifanya hivyo kwa kuwa ni baba yake mzazi.
Baada ya maelezo hayo ya awali Hakimu Matoi aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 12 mwaka huu itakapotajwa tena huku mtuhumiwa huyo akienda rumande kwa kukosa dhamana.
TAMWA NA WENGINEO MPO JAMANI