MAHAKIMU nao njiani KUGOMA...

MAHAKIMU nao njiani KUGOMA...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Wale Mahakimu Wakaazi 300 walioajiriwa na Serikali mnamo mwezi wa sita na kusambazwa mikoani wako njiani kugoma.Taarifa nilizozipata zinaonesha kuwa Mahakimu hao,tangu kuajiriwa kwao hawajalipwa mshahara wowote au hata fedha za kujikimu. Taarifa zinaonesha kuwa hali zao sasa ni mbaya na wanateseka vya kutosha.

Kwakuwa wote wanajuana vyema,Mahakimu hao Wakaazi ambao wamepelekwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama za Mwanzo wamepanga kugoma ili kudai maslahi yao kwa Serikali 'sikivu'. Ifahamike kuwa Mahakimu wakaazi ni wale wenye elimu ya ngazi ya Shahada na kuendelea na hawakuwahi kuwepo katika Mahakama za Mwanzo.Kupelekwa kwao,kutaruhusu Mawakili Wasomi kujitokeza Mahakama za Mwanzo.

Wanasema 'liwalo na liwe'....
 
Liwalo na liwe... acha wagome, serikali itakwenda mahakamani
 
Samahan naomb kuuliza mwnye kujua anijuze,hiv hakimu wa mahakama ya mwanzo na hakimu mkazi mishahara yao inakuaje!?nsijekujuta uko mbele ya safari.
 
kwani siwanafanya kazi ya kusikiliza kesi huko mahakamani kila siku?? Sasa kwanini wanashindwa kuwa na pesa au wanashindwa kuongea vizuri na wateja wao(waalifu) ?? Wanaishia kuwatupa lumande na huku wao wanakufa na njaa vunjeni ukimya mahakimu? Ongeeni vizuri na wateja wenu ili life lisonge. Kila mmoja atakula kulingana na urefu wa kamba yake
 
Heeee! Mahakimu tena? si wamepandishiwa mishahara na marupu rupu kibao hao?
 
Mila, tamaduni na kanuni za mahakama na mahakimu/majaji sidhani kama zinaruhusu hili, ndio maana wanaitwa waheshimiwa bila kupigiwa kura
 
Ni vigumu sana kuwa mazingira ya kutoa haki wakati hakama na mahakimu hawalipwi ipasavyo. Kama mahakimu hawalipwi ni rahisi kupokea rushwa tena rushwa ya chini kabisa maana hana hata hela ya kujikimu!
 
wale mahakimu wakaazi 300 walioajiriwa na serikali mnamo mwezi wa sita na kusambazwa mikoani wako njiani kugoma.taarifa nilizozipata zinaonesha kuwa mahakimu hao,tangu kuajiriwa kwao hawajalipwa mshahara wowote au hata fedha za kujikimu. Taarifa zinaonesha kuwa hali zao sasa ni mbaya na wanateseka vya kutosha.

Kwakuwa wote wanajuana vyema,mahakimu hao wakaazi ambao wamepelekwa kwa mara ya kwanza katika mahakama za mwanzo wamepanga kugoma ili kudai maslahi yao kwa serikali 'sikivu'. Ifahamike kuwa mahakimu wakaazi ni wale wenye elimu ya ngazi ya shahada na kuendelea na hawakuwahi kuwepo katika mahakama za mwanzo.kupelekwa kwao,kutaruhusu mawakili wasomi kujitokeza mahakama za mwanzo.

wanasema 'liwalo na liwe'....

una utani na pinda wewe!!!!!!!!!!!

Mahakimu hawawezi kugoma, kwani hakimu kugoma ni sawa na wafanyakazi wa mizani tanroads au traffic police au wahasibu kugoma. Hawa watu hata siku moja huwa hawasikii njaa.
 
Liwalo na Liwe!
Riwaya hii itamtesa sana Rais Kikwete!
Riwaya yenye adabrakadabra na udhaifu wa kutosha
Riwaya ya kustaajabisha! Serikali isiyolipa mishahara!
Serikali sikivu! Serikali ya Chama cha Mapinduzi!
Serikali ya Nahau na mitaala ya kuzimu!
Serikali 'Legelege' inayoendesha mambo yake 'Hovyohovyo' chini ya Rais 'Dhaifu' wa chama 'Kipuuzi' cha CCM!.
Tanzania kwa kawaida bajeti ya wizara ya sheria ka katiba kuna Kasma ya Mishahara.. Kasma hii hutengewa fedha zote za mishahara ya wafanyakazi wote walio kwenye idara hii.. Kasma hiyo huwa inafanya kazi gani nyingine tofauti ya ile iliyoamuliwa na Bunge?. Serikali! Serikali! Serikali!
Serikali! Serikali!
Serikali!
 
Sasa serikali ikipeleka kesi mahakaman kupinga mgomo wa mahakimu,nani atasikiliza kesi ya awali?
 
Sasa serikali ikipeleka kesi mahakaman kupinga mgomo wa mahakimu,nani atasikiliza kesi ya awali?

Mkuu kingkong.

Magogoni si huwa ndio tunasema wanatoa hukumu? Watasema "Mgomo wa mahakimu wa mahakama ni batili na hata kesi iliyoopo mahakamani pia ni batili kwa hiyo ikulu kama muajiri mkuu ina waamuru mahakimu waache kutumiwa na chadema na waendele kuhukumu kesi nyingine kwa weledi na kufuata misingi ya haki"
 
Wale Mahakimu Wakaazi 300 walioajiriwa na Serikali mnamo mwezi wa sita na kusambazwa mikoani wako njiani kugoma.Taarifa nilizozipata zinaonesha kuwa Mahakimu hao,tangu kuajiriwa kwao hawajalipwa mshahara wowote au hata fedha za kujikimu. Taarifa zinaonesha kuwa hali zao sasa ni mbaya na wanateseka vya kutosha.

Kwakuwa wote wanajuana vyema,Mahakimu hao Wakaazi ambao wamepelekwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama za Mwanzo wamepanga kugoma ili kudai maslahi yao kwa Serikali 'sikivu'. Ifahamike kuwa Mahakimu wakaazi ni wale wenye elimu ya ngazi ya Shahada na kuendelea na hawakuwahi kuwepo katika Mahakama za Mwanzo.Kupelekwa kwao,kutaruhusu Mawakili Wasomi kujitokeza Mahakama za Mwanzo.

Wanasema 'liwalo na liwe'....
watuhumiwa kazi ipo kama nawaona mahakimu vijana watakuwa wanakula mpaka buku......dah bora mngewaacha majumbani kwao waendelee na msoto kuliko kuwapeleka mahali wakawe OMBA OMBA.....
 
mahakimu hawaruhusiwi kugoma kisheria.
labda hawa wapya hawajui ethics zao
hela watapelekewa fungu lao limeshatengwa.
waliendaje kwenye vituo vya kazi bila fedha za kujikimu na usafiri? inatia shaka.
 
Back
Top Bottom