Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Na Hellen Mwango
20th November 2009
Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Kitengo cha Ardhi, imetoa amri ya kuzuia kwa muda hatua yoyote ya kuwaondoa wakazi 22 waliolipwa fidia eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo imekuja kutokana na Mamlaka ya Uwanja wa Ndege (TAA) kutoa siku 45 kwa wakazi hao wawe wamehama baada ya kulipwa, lakini wao wanasema hazitoshi kuwawezesha kuhamia katika viwanja walivyotengewa eneo la Pugu.
Wakazi hao pia wanasema kuwa sio rahisi kwao kuhama kwa kuwa baadhi yao hawajapokea hata hizo hundi zenyewe za malipo ya fidia.
Katika kufikia uamuzi wa kusitisha uhamishwaji kupitia maombi yao ya dharura, mahakama hiyo pia imezingatia kesi ya wakazi hao ambao wanapinga malipo yao kufanyiwa tathmini kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya mwaka 1967 badala ya sheria ya sasa ya mwaka 1997.
Shauri hilo lilisikilizwa na Hakimu Mkazi, Laurian Hemed.
CHANZO: NIPASHE
20th November 2009
Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Kitengo cha Ardhi, imetoa amri ya kuzuia kwa muda hatua yoyote ya kuwaondoa wakazi 22 waliolipwa fidia eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo imekuja kutokana na Mamlaka ya Uwanja wa Ndege (TAA) kutoa siku 45 kwa wakazi hao wawe wamehama baada ya kulipwa, lakini wao wanasema hazitoshi kuwawezesha kuhamia katika viwanja walivyotengewa eneo la Pugu.
Wakazi hao pia wanasema kuwa sio rahisi kwao kuhama kwa kuwa baadhi yao hawajapokea hata hizo hundi zenyewe za malipo ya fidia.
Katika kufikia uamuzi wa kusitisha uhamishwaji kupitia maombi yao ya dharura, mahakama hiyo pia imezingatia kesi ya wakazi hao ambao wanapinga malipo yao kufanyiwa tathmini kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya mwaka 1967 badala ya sheria ya sasa ya mwaka 1997.
Shauri hilo lilisikilizwa na Hakimu Mkazi, Laurian Hemed.
CHANZO: NIPASHE