Mahakama ya wachawi

LUKAMA

JF-Expert Member
May 28, 2017
1,081
1,271
Nakumbuka 2007 kwenye gazeti la udaku la MAISHA nilikuwa nafuatilia sana ila sikuimalizia hadi mwisho.
Anaweza Ku share nasi jamani
Gazeti lilikuwa linatoka j5 kila week kama sikosei
 
Nani huyo aliyetunza gazeti tangia 2007 aje akupe muendelezo?
mimi hapa

jamaa aliendaga kufanya kazi kanda ya ziwa akitokea tanga akapata mke akaoa kumbe ni mtoto wa moja wa magwiji wa kichawi akatakiwa kutolewa kafara
kwao tanga ikajulikana kafa na hata kwa watu wa pembeni
sasa yeye kuna bibi mmoja anaitwa b BI NYANKONGO alikuwa rafiki yake sana wakawa wanapatana sasa kumbe huyo bibi ndo jaji mkuu katika hiyo mahakama akaea anapata wkt mgumu sana kutoa hukumu
mbele anatokea mtoto mwingne wa mchawi anatokea kumpenda jamaa hivyo anaplani master watoloke katika huo mji wa kichawi demu anaisaliti familia yake ya kichawi
misukomiuko inayowapata inafanya hii simulizi kuwa moto wa kuotea mbali
ni story ya kweli ilitokea miaka ua 60 to 70 huko mwanza kipindi hicho jamaa ni jank tu now anekuwa mzee ndo akawa anasimulia hiyo storyà
 
mimi hapa

jamaa aliendaga kufanya kazi kanda ya ziwa akitokea tanga akapata mke akaoa kumbe ni mtoto wa moja wa magwiji wa kichawi akatakiwa kutolewa kafara...
Shukrani mkuu nimekusoma umenikumbusha mbali sana aise japo kuwa nilikua Dogo kimtindo kila week ilikuwa inanitoka 200 ya kukununua gazet
 
Nakumbuka 2007 kwenye gazeti la udaku la MAISHA nilikuwa nafuatilia sana ila sikuimalizia hadi mwisho.
Anaweza Ku share nasi jamani
Gazeti lilikuwa linatoka j5 kila week kama sikosei
Hii story naikumbuka yote… ngoja Nita andika Kama ilivyo nikipata muda
 
Simulizi : Nilivyotolewa Kafara Kwa Sababu ya Utajiri

Mtunzi Juma Hiza

Sehemu ya 01.

Nilizaliwa Julai 27, 1982 katika hospitali ya Bombo mkoani Tanga, nikiwa mtoto wa pekee katika familia ya wazazi wangu.
Maisha yangu baada ya kuzaliwa, sikuyafahamu, lakini nilipoanza kuwa na akili, sikuhitaji kutumia akili nyingi kujua kuwa niliishi maisha ya ufukara sana.

Hilo lilishereheshwa na chumba kimoja tulichokuwa tukiishi na wazazi wangu pale Nguvumali. Lakini pia kazi ya baba yangu ya kukodisha baiskeli nayo ilikuwa ushahidi tosha wa maisha magumu niliyoishi na wazazi wangu.

Pamoja na ufukara huo, nikiwa nalala chumba kimoja na wazazi wangu, mimi nikilala kweny kochi kubwa na wao wakilala kitandani, nilikuwa nina ndoto kubwa ya kuwakomboa wazazi wangu katika maisha hayo magumu yanayonuka dhiki tupu.

_____________
Nilikuwa nina ndoto ambayo niliamini sana, njia pekee ya kuupata utajiri ilikuwa ni elimu tu!

Nakumbuka sana mwalimu wangu wa darasa la tatu, alikuwa kila anapoingia darasani kwetu asubuhi kufundisha somo la hisabati, alisisitiza “Elimu ndiyo ufunguo wa maisha”.

Niliamini sana kauli yake na niliamua kuitumia kwa nguvu zote nikiamini kwamba ndiyo njia pekee itakayonisaidia.

Nikaanza kusoma kwa bidii. Sikujali ufukara wa wazazi wangu, nikasoma kwa bidii sana. Kuanzia wakati huo, nilikuwa nashika nafasi ya kwanza katika kila muhula mpaka nilipofika darasa la saba.
___________
Ni kati ya siku ambazo haziwezi kufutika akilini mwangu. Siku ambayo nilijiuliza kama baba yangu ni mchawi.

Ilikuwa lazima nijiulize swali hilo gumu kichwani kwani mambo niliyomuona baba yangu akiyafanya alikuwa mazito sana.
Ilikuwa ni siku ya Alhamisi, nikiwa ndiyo nimetoka shuleni, begi langu mgongoni, njaa kali ikiwa inaniuma sana.

Nilipofika niliingia ndani bila kubisha hodi, nilifanya hivyo nikiwa nina uhakika kwamba baba yangu hawezi kuwa ndani muda huo. Kwa kawaida, muda huo baba huwa kijiweni kwake anapowasubiria abiria wa kuwakodishia baiskeli.

I

20210616_182412.jpg
 
Okay ilikuwa hivi… kuna kijana alikuwa anakaa singida na Kaka yake .. kwa muda huo alikuwa amemaliza darasa la saba .. sasa alikuwa anakaa tu nyumbani na Kaka yake Ila alibahatika na kipaji cha kutengeneza vitu… basi kuna siku pikipiki ya Kaka yake ilikuwa mbovu na alikuwa na safari kidogo basi yule mdogo wake akatoka nje akaifungua fungua ikawaka basi kutokea pale kaka yake akamuahidi atamtafutia kazi… basi siku zikaenda na siku moja kaka yake alivyorud kazini akamwambia amepata kazi ya kuchimba visima huko kanda ya ziwa.. yule kijana akafurahi Ila ikabidi akamuage bibi yake ambaye alikuwa anaishi Tanga na pia akamtambikie….

Basi siku ikafika yule Kijana akaenda Tanga kwa Bibi yake.. Bibi yake alimpokea akamtambikia na akamwambia huko unakoenda kuwa makini kuna imani za kishirikina sana na pia usipende wake za watu hata siku moja… pia uwe mtiifu una uwe unawaheshimu wakubwa Ana uwe na Tabia nzuri.. basi yule kijana akaitikia kwa utiifu baada ya siku mbili akarud kwa kaka yake singida.

siku ya kwenda kazini ikawadiA yule kijana akaondoka. Alivyofika huko akakutana Ana wenzake watano so jumla wakawa 6. Basi kazi ya kuchimba visima ikaanza… Ila kwenye makazi walitengeneza Kama mahema 3 so wakawa wanalala wawili wawili na kupika wakawa wanapika kwa zamu.. basi kazi ika endelea ya kuchimba visima.

sasa siku moja walimaliza kuchimba visima mapema.. jamaa haikuwa zamu yake kupikA hiyo siku akaona bora akatembee.. basi jua lilikuwa linakaribia kuzama .. jamaa akatoka akaanza kufuatisha kinjia huyo huyo mpka akafika mbali mbali alipoona amefika mbali akaamua ageuze arudi sasa alivyogeuka nyuma ile njia aliyokuja nayo haioni akatafuta njia wapi… muda huo giza limeshaingia sasa.. Tafuta njia wapi tafuta njia wapi… basi sasa kwa mbali akaona kataa kana waka… akaamua kufuata ule mwanga wa taa mwishowe akafika kwenye hako kajumba nje akakutana na pisi kali nyeupe ya kisukumA inapika ugali.. basi jamaa akauliza mim nafanya kazi pale kwenye visima Ila nimepotea naomba nielekeze niweze kurudi basi yule demu akamwambia mbona sio mbali hata Ila kaa ule alafu nikupeleke basi jamaa akapewa mkeka akapewa na maziwa akanywa mama yake yule demu alivyokuja akamsalimia NA akamtania a mtoto wangu mweupe huyu hapa nataka ng’ombe 50.. wakacheka wote… chakula kikaiva jamaa akapiga msosi baada ya kula yule msichana akamwambia mama yake Anamsindikiza jamaa basi wakaondoka ila cha ajabu wakatembea kidogo tu wakafika.. yule msichana akamuaga jamaa akarudi kwao.

NITAMALIZIA TENA BAADAE VIDOLE VINAUMA
 
Back
Top Bottom